Fortunatus Buyobe @Buyobe
Thread by Fortunatus Buyobe- CHINA PLAZA
A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
MAFUNDI SIMU CHINA PLAZA
Kuna wakati unaweza unaweza kushindwa kusafiri kwa sababu tu
basi ulilopanga kusafiria limekuacha baada ya kuchelewa.
Hupaswi kujilaumu kama hili litakutokea.
Mara nyingine Mungu huwa anaingilia kati ili kukuepusha na baya
ambalo lingeweza kukutokea endapo ungekuwa ndani ya basi hilo.
Ni mara ngapi tumesikia watu wakitoa shuuda kuwa gari fulani
lilimuacha na kisha mbeleni gari hilo likapata ajali?
Hili ndilo lililomtokea Moses John miaka miwili iliyopita.
kijana huyu ni muuza simu katika jengo la CHINA PLAZA lililoko
mtaa wa Aggrey Kariakoo.
Tarehe 26 December mwaka 2021, vijana kadhaa ambao wote wanajishughurisha kuuza simu kwenye jengo hilo, walikubaliana waende wakasherehekee sikukuu ya Christmas katika fukwe za
Kigamboni.
Majira ya saa 6 mchana, Kijana mwingine aitwaye Rajab Mdoe aka Choiya akampigia simu mama yake mlezi aitwa Taabu Said Banga (Rajabu ni mtoto wa marehemu mdogo wake na Taabu)
Haya ndio yalikuwa maongezi yao
Rajab: Mama, utatumia gari lako leo?
Bi Taabu: Hapana, Kwa nini unaniuliza hivi?
Rajab: Nataka kulitumia…Leo tunataka kwenda beach Kigamboni
na rafiki zangu
Bi Taabu: Hakuna shida. Unaweza kulitumia.
Bi Taabu anaishi Tabata Kinyerezi wakati mwanae anaishi
Bonyokwa
Majira ya saa 8 mchana, Rajabu akafika Kinyerezi akiwa
ameambata na rafiki yake aitwaye Tawfiq Mohamed.
Baada ya mazungumzo na mama yake, wakachukua gari aina ya Toyota IST jeusi kwa rangi.
Wakaeleza kuwa wanampitia tena rafiki yao mwingine aitwaye
Hemed Abass
Wakaondoka.
Makutano (RV) baina ya vijana hawa na wengine walionuia kwenda Kigamboni, ilikuwa ni Kariakoo wanakofanyia kazi.
Mpaka gari inafika kariakoo waliwakuta vijana wenzao ambao ni
Edwin Kunambi na Seif Swala
Ambaye hakuwa amefika ni Moses John ambaye alichelewa kufika
walipokubaliana wampitie hivyo wakamuacha.
This was a lucky accident to Moses!
Kwa nini nasema hivi?
Ni kwa sababu vijana wale hawakuonekana tena kwa macho ya
kibinadamu as the became microscopic.
Walipotea kama sindano!
Neno la mwisho kutoka kwao ulikuwa ni ujumbe ambao Edwin alimtumia Moses kuwa wamekamatwa wakiwa eneo la Kamata na
wanapelekwa kituo cha polisi cha kati.
Rafiki zao wa Kariakoo, wakaenda kuwafatilia central polisi lakini majibu yakawa ni hawajafikishwa pale.
Jitihada zikahamishiwa kwenye vituo vya Oysterbay, Msimbazi, Salender Bridge lakini nako wakaambulia patupu.
Hadi wakati huu, ndugu wa wazazi hawa hawakuwa na taarifa kuwa
watoto wao wamekamatwa.
Majira ya saa 4 usiku, Bi Taabu alimpigia mwanae simu kumuuliza kama amesharudi.
Simu ile iliita bila kupokelewa.
Majira ya saa 6 usiku alipojaribu tena kumpigia mwanae, simu ilikuwa haipatikani.
Akaamini labda imeishiwa chaji akaamua kwenda kulala.
Hali hii ilikuwa pia kwa mzee Longili Martin baba wa Edwin Kunambi
Yeye hakujishughurisha kabisa kumpigia mwanae kwani alishaongea na mwanae alipompigia kumtaka ajumuike naye
kusherehekea sikukuu ya Noel nyumbani kwake Gongolamboto.
Edwin akamjibu hataweza kufika kwani ametingwa na shuguri
lakini akamwambia baba yake atajumuika naye kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya.
Hivyo Mzee Longili naye hakuwa na fununu juu ya yaliyomsibu mwanae Edwin
Siku ikapinduka...SUBSCRIBE HAPO CHINI KUENDE;EA KUSOMA MAKALA
click here to unlock the post
Fortunatus Buyobe @Buyobe
NANI ALIAGIZA MAUAJI YA BARKE?
Usiku wa kuukaribisha mwaka 2022 ulianza kwa sherehe, lakini ukamalizika kwa fumbo la kutisha. Barke alionekana akiondoka Kitambaa Cheupe akiwa kwenye bodaboda pamoja na mwanaume aliyejulikana kama “John Cena”—siku iliyofuata mwili wake ukapatikana katika nyumba ya wageni. Kamera za CCTV zilizofutwa, picha zilizopigwa kwa siri, rafiki aliyetoweka na madai ya muuaji kukodiwa vinaacha swali moja kubwa: Ni nani hasa aliyekuwa nyuma ya mpango huu—na kwa nini? SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI
click here to unlock the post
Fortunatus Buyobe @Buyobe
Thread by Fortunatus Buyobe click here to unlock the post
Fortunatus Buyobe @Buyobe
A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
THE FIXER
Tarehe 17 May 2012, taifa letu lilishuhudia tukio ambalo limetokea mara moja tu kwenye
historia na bado halijajirudia hadi sasa.
Majira ya saa 4 na dk 45 asubuhi msafara wa rais mkapa ulionekana ukiingia kwenye
viunga vya mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Wananchi walihisi ni kama mzaha waliposoma gazeti la Mwanahalisi la April 14 mwaka
mmoja nyuma, gazeti hilo lilipovujisha kiapo cha rais Mkapa alichokitoa mbele ya
wakili Mabere Marando.
Pia hata gazeti la Mwananchi lilipovujisha barua ya wakili Marando kwenda kwa katibu
mkuu kiongozi Philemon Luhanjo, watu bado walichukulia ni mzaha
Wakili Marando alikuwa amemwandikia Philemoni Luhanjo kumuandaa rais Kikwete
kufika mahakamani kama shaidi wa utetezi.
Barua ile kwenda kwa Kikwete haikujibiwa pamoja na jitihada za wakili Marando
kukumbushia
Sasa watu wakiwa na ile hali ya kutoamini, ndipo Mkapa anaonekana hapa mahakani
muda huu, siku hii
Waandishi wa habari walihaha kupata picha za Mkapa na walinzi walifanya jitihada
kuzuia
Mkapa aliongozwa moja kwa moja katika chumba maalumu cha hadhi yake pale
mahakamani akisubiri muda wake wa kutoa ushaidi
Naam, Rais Mkapa alikuwa ni shaidi dhidi ya mtuhumiwa Prof. Costa
Mahalu,aliyekuwa balozi Italia, pamoja na Grace Martin aliyekuwa afisa utawala wa
ubalozi
Ni kwamba, January 22 mwaka 2007, Mahalu alipandishwa mahakamani na kusomewa
shitaka la kuhujumu uchumi katika kesi No. 1 ya mwaka 2007
Balozi akituhumiwa kutumia vibaya madaraka na kuisababishia hasara ya bilioni 2.9
serikali ya Tanzania
Ilidaiwa kuwa balozi Costa alitenda hayo akiwa ni balozi wa Tanzania nchini Italia Sept
22 mwaka 2002 ambapo alinunua jengo la ubalozi wa Tanzania na malipo kuingizwa
kwenye akaunti mbili tofauti za mlipwaji kwa nia ya kumuibia muajiri wake.
Majira ya saa 5 na Dk 32 rais Mkapa akawa tayari mbele ya hakimu mkazi Ilvin Mgeta
akitoa ushaidi wake.
Mkapa, akiongozwa na wakili Alex Mgongolwa aliyekuwa akimtetea Mahalu alitoa
ushaidi ufuatao.
Mgongolwa: Mwaka 1995 hadi 2005 ulikuwa wapi?
Mkapa: Nilikuwa Dar Es Salaam nikishika wadhifa wa urais wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania
Mgongolwa: Unafahamu nini kuhusu ununuzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini
Italia
Mkapa: Nafahamu balozi wetu alifanya ununuzi wa jengo hilo kwa Euro 3,098,741.40
kwa maelekezo ya serikali ya Tanzania
Mgongolwa: Mlipewa masharti yoyote kwenye ununuzi?
Mkapa: Ndiyo! Muuzaji alitaka aingiziwe malipo kwenye akaunti mbili tofauti, zote
zikiwa na majina yake.
Mgongolwa: Mlipata malalamiko yoyote kutoka kwa mnunuzi au serikali ya Italia?
Mkapa: Hapana
Wakili Alex Mgongolwa akaanza kusomea rais Mkapa maelezo ya rais Kikwete
aliyoyatoa bungeni wakati huo akiwa ni waziri wa mambo ya nje.
Kikwete alitoa maelezo haya wakati anachangia bajeti ya wizara yake ya mwaka
2001/2002
Maelezo ya Kikwete yalieleza kuwa “Serikali imenunua jengo la ubalozi Italia kwa Euro
3,098,741.40 baada ya kufata ushauri wa wizara ya ardhi na Ujenzi hivyo utaratibu wote
ulifuatwa.”
Mgongolwa: Maelezo haya ni sahihi
Mkapa: Ni sahihi
Mgongolwa: Mbona katibu mkuu wako kiongozi bwana Marten Lumbanga ambaye ni
shahidi wa kwanza wa Jamuhuri anadai hakujua manunuzi haya?
Mkapa: Nimeshangaa kusikia anasema hajui. Rais siwezi kujua juu ya kitu na katibu
mkuu kiongozi asijue.
Mkapa akaendelea kueleza kwamba ameshangaa kuona Mahalu akishitakiwa kwa
jambo hilo na hajui nani aliyeagiza upelelezi juu ya jambo hilo hadi kumshitaki.
Mkapa akaeleza hajui kama upelelezi ulianza akiwa madarakani au ameshataafu.
Alishtukia tu Mahalu anapandishwa kizimbani
Baada ya Alex Mgongolwa kumaliza kumuongoza Mkapa, ikafata zamu ya upande wa
mashitaka kum”cross-examine”
Akaingia ulingoni wakili wa serikali Ponsiano Lukosi
Lukosi: Huoni kama dai la muuzaji kutaka kulipwa kwenye akaunti mbili tofauti
ulikuwa ni ukwepaji wa kodi?
Mkapa: Hilo si tatizo langu. Ni tatizo la nchi yake. Mimi nimepata jengo nililotaka...,
Alhamdulilah.
Lukosi : Huu sio wizi wa mshtakiwa?
Mkapa: Nitashangaa sana Mahalu kuwa mwizi, na nitakushangaa wewe. Mahalu ni
msomi mzuri, na mtumishi mwaminifu sana.
Mkapa akataka kusema kitu kisha akasita
Akamwambia Lukosi asimchokoze asije akasema mangine yasiyohitajika.
Majira ya saa 7 na Dk 8 rais Mkapa alikuwa ameshamaliza kutoa ushaidi wake
Ina maada Mkapa alitoa ushaidi kwa zaidi ya muda wa saa moja na Dk 30
akimpambania balozi wake Mahalu.
Mahalu hakukutwa na hatia kwenye kesi kesi hivyo aliachiwa huru.
Wakati anatoa hukumu, Hakimu mkazi Irvin Mgeta alitumia nadharia ya Principal na
Agent
Kuwa Principal (Serikali) ilimpa “Power of attorney” Agent (Balozi) kufanya kila kitu
ubalozini akiiwakilisha Jamuhuri ya Tanzania kisha baadaye analalamikia Power
aliyompa
Mgeta alifananisha hali hiyo ni sawa na mtu aliyeijaza bastola risasi, akaikoki,
akajielekezea na kuifyatua
Kisha mtu huyo alalamile risasi imemuua
Baadaye katika uzinduzi wa kitabu chake, rais Mkapa alieleza kuwa aliamua kumtetea
Mahalu kwa kuwa aliona anaonewa.
Naam!
Rais Kikwete aliingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa October 2005 alipoibuka
kidedea.
Sera yake ya kasi mpya, nguvu mpya na hari mpya, ikimbeba dhidi ya wapinzani wake
kwenye uchaguzi huo.
Miaka miwili tangu ushindi wa Kikwete, tukaanza kushuudia kesi kubwa dhidi ya
viongozi wakubwa wa iliyokuwa serikali ya mtangulizi wake ambaye yeye alimtumikia
kama waziri.
Kesi ya kwanza ilikuwa ni hii ya Mahalu iliyofunguliwa mwaka 2007
Mahalu alikuja kutoa ushaidi uliokuja kuichanganya vibaya kambi ya mashtaka
Takukuru waliokuwa wakitumia kama ushaidi barua ya Mahalu aliyoandikia serikali
Feb 2, 2002 kuijulisha kuwa amefikia hatua ya ununuzi wa jengo, walishtushwa na
nyaraka alizoibua Mahalu mahakamani
Mahalu alikubali kweli ile ni barua aliyoandaa mwenyewe na aliituma kwa mabosi wake
Katibu mkuu na Waziri wa mambo ya nje (Kikwete)
Pia aliwanukuu Katibu Mkuu (Lumbaga) Kiongozi, Waziri wa fedha (Mramba) na
Kamishina wa bajeti wa wizara ya mambo ya nje.
Mahalu akaeleza barua ile waliyonayo TAKUKURU ilikuwa na viambatanisho 11
ambavyo hajui ni kwa nini hawajavitumia kwenye ushaidi
Sasa Mahalu akawa anashambulia kwa ngumi za “below the belt” kuusambaratisha
upande wa mashtaka
Mahalu akatoa mahakamani ripoti ya ....Subscribe hapo chini kuendelea kusoma makala hii na nyingine nyingi
click here to unlock the post