UKWELI USIOUJUA KUHUSU BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA

Marehemu huwa haongelewi kwa mabaya, Lakini matendo yao hapa duniani hayatufungi mikono kuyajadili kwa ajili ya mafundisho ya vizazi vijavyo.

80% ya Madawa ya kulevya yanayopatikana Tanzania, Si kwa ajili ya watumiaji wa ndani.

Naam!

Madawa haya si kwa ajili ya soko la Tanzania ingawa yanapatikana kwa wingi nchini kwetu.

Tanzania ni kama lango tu(Corridor) kwa ajili ya kupitisha madawa haya mpaka kwenye soko lililokusudiwa (Target Market)

Ni kwa nini yasitumike ndani wakati walaji wapo hapa hapa?

Jibu ni jepesi sana,

Gharama!

Yes , Gharama!

Madawa haya huwa ni very expensive kwa watumiaji wa ndani kuweza kuyamudu. Ni watanzanzia wachache wenye uwezo wa kumudu gharama za madawa haya.

Ni kwa sababu hii walaji wengi wa ndani huishia kula makapi (by products) aka “Ngada”

Makapi haya ndio huwa na madhara makubwa kwa mtumiaji kuliko wale wanaotumia kitu “pure” kabisa.

Ok.Tumejua kuwa Tanzania ni njia tu!

Je “Mzigo” hutoka wapi na kwenda wapi?

Here we are!

Nifatilie taratiiibu nikielezea habari hii kwa kunuu Chanzo.

“Mzigo huwa unatoka either “Kwa Pele” au “Kwa Musharaf”

Ndugu Msomaji, Popote litakapotumika neno “Kwa Pele” jua ni Brazil na “Kwa Musharaf” Jua ni Pakistani.

Hizi nchi huitwa kwa Codes hizo ndani ya Ulimwengu wa wasafirishaji.

Kwa hiyo mzigo unatoka Brazil au Pakistani

“Mzigo ukitoka huko anapewa mbebaji mmoja ambaye husafirisha kwa kuyameza mpaka Dubai.

“Hasafiri bila mipango kuwa imesukwa tangu anakotoka mpaka Dubai”

“Akifika Dubai Safari yake inaishia pale na analipwa kabisa Chake pale pale.”

“Anaishia pale kwa Sababu Passport ikisomeka imegongwa mihuri ya Kwa Pele au Musharaf basi maafisa Ukaguzi viwanja vya ndege huwa makini sana na mzigo wowote uliobeba”

“Ili kuepusha mzigo kudakwa inabidi mtu wa kwa pele au Musharaf aishie Dubai”

“Tangu mzigo unapotoka shambani, tayari anakuwa ameshaandaliwa “punda” mwingine ambaye atameza ule mzigo pale Dubai na kuuvusha mpaka Msumbiji”

“Huyu naye ataishia Msumbiji tu na kulipwa Chake”

“Kutokea Tanzania, Punda mwingine atavuka mpaka Msumbiji kwa kukata passport ya masaa 24 tu”

“Si rahisi maafisa usalama kumshtukia mtu huyu ambaye kavuka tu Kuingia Msumbiji na baada ya Masaa katoka”

“Punda huyu ndiye atakayemeza mzigo wa Msumbiji na kuuingiza Mtwara/Lindi”

So ndugu Msomaji Umeona “Triangle of Custody” ya Mzigo kuanzia shambani mpaka umefika mikoa ya Kusini.

Njia unavyokuja haiachi traces zozote kwa yule aliyefanikiwa kuufikisha kwenye point aliyoelekezwa.

Huwa kuna Viapo na binadamu anawezwa kutumika kama “bond” ya kiapo.

Mzigo Ukifika kusini, Sio mwisho wa safari, Mzigo ule hukutana na wakemia wenye uwezo wa kucheza na Molecular formula ya fawa zile kuzifanya zisomeke kama raw materials ya dawa zilizokubalika kwa matumizi ya binadamu. (Refer HYDROCARBONS)

Naam!

Wanageuza nyekundu kuwa Njano.

Kuanzia hapa sasa ndio matawi ya Kusambaza mzigo huu yanapoanzia either kwenda nchi kama Congo, Nigeria, South Africa mpaka kwa watumiaji wenyewe kabisa Marekani, China etc.

Leo nashuka na Mkasa wa mabinti wawili walioingia kwenye biashara hii mwaka 2013.

Katika mkasa huu ndipo ilipoonekana kuwa mapambano dhidi ya biashara hii ni sawa na kujichimbia kaburi lako Mwenyewe.
SUBSCRIBE HAPO CHINI ILI KUPATA MKASA HUU NA MINGINE MINGI KWA MWEZI MZIMA click here to unlock the post

KUTOWEKA KWA WAUZA SIMU CHINA PLAZA

Kuna wakati unaweza unaweza kushindwa kusafiri kwa sababu tu basi ulilopanga kusafiria limekuacha baada ya kuchelewa.

Hupaswi kujilaumu kama hili litakutokea.

Mara nyingine Mungu huwa anaingilia kati ili kukuepusha na baya ambalo lingeweza kukutokea endapo ungekuwa ndani ya basi hilo.

Ni mara ngapi tumesikia watu wakitoa shuuda kuwa gari fulani lilimuacha na kisha mbeleni gari hilo likapata ajali?

Hili ndilo lililomtokea Moses John miaka miwili iliyopita.

kijana huyu ni muuza simu katika jengo la CHINA PLAZA lililoko mtaa wa Aggrey Kariakoo.
Tarehe 26 December mwaka 2021, vijana kadhaa ambao wote wanajishughurisha kuuza simu kwenye jengo hilo, walikubaliana waende wakasherehekee sikukuu ya Christmas katika fukwe za Kigamboni.

Majira ya saa 6 mchana, Kijana mwingine aitwaye Rajab Mdoe aka Choiya akampigia simu mama yake mlezi aitwa Taabu Said Banga (Rajabu ni mtoto wa marehemu mdogo wake na Taabu)

Haya ndio yalikuwa maongezi yao

Rajab: Mama, utatumia gari lako leo?

Bi Taabu: Hapana, Kwa nini unaniuliza hivi?

Rajab: Nataka kulitumia…Leo tunataka kwenda beach Kigamboni na rafiki zangu

Bi Taabu: Hakuna shida. Unaweza kulitumia.

Bi Taabu anaishi Tabata Kinyerezi wakati mwanae anaishi Bonyokwa.
Majira ya saa 8 mchana, Rajabu akafika Kinyerezi akiwa ameambata na rafiki yake aitwaye Tawfiq Mohamed.

Baada ya mazungumzo na mama yake, wakachukua gari aina ya Toyota IST jeusi kwa rangi.

Wakaeleza kuwa wanampitia tena rafiki yao mwingine aitwaye Hemed Abass

Wakaondoka.

Makutano (RV) baina ya vijana hawa na wengine walionuia kwenda Kigamboni, ilikuwa ni Kariakoo wanakofanyia kazi.

Mpaka gari inafika kariakoo waliwakuta vijana wenzao ambao ni Edwin Kunambi na Seif Swala

Ambaye hakuwa amefika ni Moses John ambaye alichelewa kufika walipokubaliana wampitie hivyo wakamuacha.

This was a lucky accident to Moses!

Kwa nini nasema hivi?
Ni kwa sababu vijana wale hawakuonekana tena kwa macho ya kibinadamu as the became microscopic.

Walipotea kama sindano!

Neno la mwisho kutoka kwao ulikuwa ni ujumbe ambao Edwin alimtumia Moses kuwa wamekamatwa wakiwa eneo la Kamata na wanapelekwa kituo cha polisi cha kati.
Rafiki zao wa Kariakoo, wakaenda kuwafatilia central polisi lakini majibu yakawa ni hawajafikishwa pale.

Jitihada zikahamishiwa kwenye vituo vya Oysterbay, Msimbazi, Salender Bridge lakini nako wakaambulia patupu.

Hadi wakati huu, ndugu wa wazazi hawa hawakuwa na taarifa kuwa watoto wao wamekamatwa.
Majira ya saa 4 usiku, Bi Taabu alimpigia mwanae simu kumuuliza kama amesharudi.

Simu ile iliita bila kupokelewa.

Majira ya saa 6 usiku alipojaribu tena kumpigia mwanae, simu ilikuwa haipatikani.

Akaamini labda imeishiwa chaji akaamua kwenda kulala.
Hali hii ilikuwa pia kwa mzee Longili Martin baba wa Edwin Kunambi

Yeye hakujishughurisha kabisa kumpigia mwanae kwani alishaongea na mwanae alipompigia kumtaka ajumuike naye kusherehekea sikukuu ya Noel nyumbani kwake Gongolamboto.

Edwin akamjibu hataweza kufika kwani ametingwa na shuguri lakini akamwambia baba yake atajumuika naye kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya.

Hivyo Mzee Longili naye hakuwa na fununu juu ya yaliyomsibu mwanae Edwin

Siku ikapinduka.

Tarehe 27 Dec 2021 bila fununu

Bi Taabu ndiye alikuwa wa kwanza kupata taarifa.

Majira ya mchana tarehe 27 Dec, walifika nyumbani kwake vijana wawili waliopakiwa mshikaki kwenye bodaboda

Vijana hao walijitambulisha kama Babu Ally na Musa (Moses)

Wakaeleza kuwa kija Rajabu walikamatwa tangu jana lakini wanawatafuta bila mafanikio.

Wakaeleza wamefika pale baada ya kutoka kuwaulizia kituo cha Stakishari bila mafanikio pia.

Kwa mtindo huu taarifa zikawafikia ndugu wa Tawfiq, Seif, Edwin na Hemedi.

Then the men-hunt was launched

Hakuna Hospitali, Vyumba vya maiti na vituo vya polisi ambavyo hawakutembelea jijini Dar bila mafanikio.

Hili lilifanyika kwa wepesi kwa kuwa walijigawa kwa timu tano tofauti.

Habari hii ikaanza kuenea kwenye mitandao ya kijamii “like a bushfire in harmattans”.

Nikawa nausoma mchezo kutokea benchi

Let me declare my Interest…

Kaka wa mmoja wa vijana hawa used to be a friend to me.

Kaka huyu ni maarufu kwa jina la DJ Mario ambaye enzi hizo alikuwa ni DJ wa Club ya Rainbow jijini Dodoma (sijui kwa sasa)

Mdogo wake aliyepotea kama sindano ndiye Tawfiq Mohamed
Niweke angalizo mapema wakati nikiwaletea kisa hiki kuwa mjua mtu aliyekaribu na victims hakunifungi mikono kwa vyovyote kueleza “nothing but truth”

Na pia navikumbusha vyombo husika kuwa kuna watu are being killed softly kwa trauma ambayo imebaki nyuma ya mkasa huu.

Just try to imagine mama wa Tawfiq (Sylvia Quentin) ambaye ni si Mkristu anashiriki misa ya Mwamposa online akiomba Mungu amtendee muujiza mwanae arudi mchungaji huyu akipanda madhabauni.

Hli linafanyika mwaka mzima ukiwa umepita bila mwanae kupatikana.

Anaeleza kuwa anaugua maradhi ya moyo tangu kupotea kwa mwanae anashidwa kutoka kujihangaikia.

Pia Naima Ndyanabo, mama wa Hemed Abass anaeleza kuwa sasa amebaki akimtumaini Mungu pekee ndiye atakayeweza kumrejesha mwanae na imani yake kwa jeshi la polisi imetoweka.

Kwa hiyo however how serious the crimes these youngsters have committed, kitendo tu cha kuwaona mahakamani huku wakinyimwa dhamana kitawapa relief ndugu zao.

Yafuatayo ndio yamechipuka nilipoanza kuufatilia mkasa huu.

Katika kuchunguza maisha binafsi ya watu hawa, imesemekana vijana hawa walikuwa watu wa “bata” sana!

Walikuwa wanapenda kujirusha kidimbwi, Small planet etc ambako huko pombe zinaletwa huku ukiwa umewashiwa mishumaa inayotoa cheche ndongo kama baruti

Gharama za vinywaji na chakula maeneo haya huwa zimechangamka sana.

Kwa “winga” wa kuuza simu tu pale China Plaza, kumudu kufanya haya mara kwa mara kuna “invite a strong suspicion” ingawa unaweza unaweza kuwa na kipato kingine kukuwezesha

Wengine wakidai nje ya kuuza simu, walikuwa pia ni madalali wa kuuza magari Ilala.
Katika kuchimba zaidi, likaibuka swala la IMEI za simu

Hapa ndipo picha zikaanza kufunguka
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

License to kill

Baada mashambulizi ya September 11, 2001 nchini Marekani, mkurugenzi wa idara ya ujasusi Marekani (CIA) bwana George Tenet alikuwa kwenye kitimoto.

Hii ni baada kubainika uzembe mkubwa mkubwa ambao idara yake iliufanya.

Kuna mambo watendaji wa chini yake walikuwa wanayajua na hayakuwa yamefikishwa kwake hadi tukio linatekelezwa.

Alipobaini jinsi taarifa zile zilivyo nyeti, mkurugenzi huyu aligonga kwa nguvu meza yake na kutukana;

“We’re Fu..ed”

Mkuu wa idara ya kupambana na ugaidi CIA (counter-terrorism Center) ampako lilikuwepo dawati maalumu la Osama bin Laden ilimbidi awe akilala ofisi ya CIA kwa siku tano mfululizo akijibu hoja juu ya uzembe ule.

Mkuu huyu bwana Coffer Black alijiona na hatia ya kushusha hadhi ya shirika hilo.

Pengine CIA wangefanya kazi yao kwa kushirikiana na FBI, mashambulio haya yasingeweza kutokea baada ya kuzuiliwa mapema.

Lakini kulikuwa na mahusiano mabovu sana baina ya idara hizi mbili kutokana na kila idara kujiona ni ya muhimu kuliko nyingine.

CIA waliamini FBI ndio waliokuwa wanawajibika kuwapatia taarifa zao zote za kiintelejensia na wao kuzichakata, wakati wao CIA wakichagua nini cha kuwapa au kutowapa FBI

Ingawa CIA walikuwa sahii, lakini walikuwa wanajikuta wanamzigo mkubwa wa taarifa ambazo ziliwashinda kuchakata zote.

Hivyo wangeshirikiana vizuri na FBI inawezekana sambulio la September 11 lingeweza kuzuilika.

Kwa nini naandika haya?

Nisome!

Baada ya shambulio la sept 11, wataalamu wa tehama walipopitia taarifa mbalimbali ndani ya mifumo ya makao makuu ya CIA jijini Virginia, walibaini taarifa za kushtua.
Ni kwamba kumbukumbu mbalimbali zilibainisha kuwa, CIA walikuwa wanawafatilia kwa muda mrefu watu wawili.

Watu hao walikuwa ni kati ya waliohusika na shambulizi la september 11

Ni kwamba CIA ilikuwa inawafatilia watu wale tangu walipotoka hadi walipoingia Marekani lakini mwaka 2000 wakaachana na swala hilo.

Naam!

Kwa zaidi ya mwaka mmoja watendaji wa CIA walikuwa wanafahamu watu hawa walikuwa ndani ya Marekani lakini hawakuwajulisha FBI

Issue inaanzia mbali tangu wakati wa shambulizi za balozi za Marekani Tanzania na Kenya mwaka 1998

Balozi hizi ziliposhambuliwa, ilitumwa timu ya FBI kuja kupeleleza.

Jijini Nairobi, mmoja ya watu waliohusika na ulipuaji wa ubalozi alikamatwa siku 20 tu baada ya tukio.

Huyu alikuwa ni Mohammed Rashed Daoud al-Owhali.

In fact alipaswa kujitoa mhanga kwenye tukio lile, lakini alipofika kwenye ubalozi alishuka na kumrushia mlinzi kitu kama bomu la kurushwa kwa mkono na kukimbia.

Dereva aliyebaki kwenye gari lenye bomu ndio akajilipua na bomu badala yake.

Hata hivyo mtu huyu anayekimbia aliweza kuunguzwa mgongoni na mkononi kwa bomu lililolipuka nyuma yake.

Mtu huyu akakimbilia hospitali za uchochoroni kutibiwa ambapo madaktari waliompokea waliyashuku majeraha yake wakatoa taarifa polisi.

Polisi wakamkamata na kumkabidhi kwa FBI

So the guy was now going to help the FBI with investigations.

The phrase “helping with investigations” doesn’t necessarily mean that yo sit with the FBI on a sofa coach, sipping juice while giving your views to what might’ve actually transpired on the crime scene

Totally wrong,

You will simply see one colorless and clueless person approaching your hairy tennis balls with a ‘burdizzo’ ready to perform a free testicles surgery on your balls if you are uncooperative.

It is in this way, Afisa wa FBI bwana Daniel J Coleman alimfanyia mtu huyu ‘a gentle interrogation’

Mtu huyu akaanza kurap

Jinsi alivyosafiri kutoka Pakistan mpaka Kenya

Hadi jinsi alivyotoroka kuwa tarishi wa Mungu (rasul Allah) kwa kujilipua kwa bomu na kwenda kutibiwa hospitali.

Akaeleza hadi alivyoficha bafuni funguo za kufuli la gari lililokuwa na bomu kwenye hospitali aliyokuwa akitibiwa pamoja na risasi moja.

Kuna kosa kubwa sana mtu huyu alilifanya…

Ni kwamba, alipokuwa hospitali alipiga namba moja Yemen kuomba atumiwe pesa ili ajitibie na nauli ya kuondoka Nairobi

Naam

Namba 967-1-200578

Namba hii alipiga kabla na baada ya tukio la ulipuaji wa ubalozi wa Nairobi.
Aliwapa FBI namba hii baada ya FBI kukubali ombi lake la kuomba akashitakiwe Marekani na sio nchini Kenya

(I think he believed that Kenyans would’ve brought him back to circulation of beatings like a rented mule)

All in all FBI got the number

Pamoja na haya mtu huyu hakuacha kuwaambia FBI kitu cha muhimu sana

Aliwaa mbia hivi;

“We have a plan to attack th U.S., but we’re not ready yet.”

“We need to hit you outside the country in a few places so you won’t see what is going on inside”.

“The big attack is coming. There’s nothing you can do to stop it.”

Kuwa wana mpango mkubwa wa kuishambulia Marekani lakini mpango bado haujakamilika.

Kuwa kwa wakati ule wanaishambukia Marekani kwenye sehemu chache nje ya nchi ili wasijue kinaendelea ndani

Kitu kikubwa kitawafata na hawataweza kukizuia.

FBI hawakupuuzia taarifa ile.

Wakampatia namba ile station chief wa CIA Nairobi na pia wakaituma NSA (National Security Agency) Marekani

Kama kuna msomaji hajui kazi za NSA hawa wanausika na maswala mazima ya ujasusi wa Tehama.

Idara hii ina radar kubwa sana ya ardhini nchini Austaria iitwayo Pine gap ambayo hufanya kazi ya kukusanya habari za mitandao ya simu, satelite nk na kuachunguza kama kuna habari yoyote hatarishi kwa Marekani.

Kifupi idara hii ndio kinara wa kuvunja sheria ya faragha kwenye mawasiliano kwani ndio inafanya udukuzi wa hali ya juu.

Snowden, aliyekuwa contractor wa Computer wa CIA na NSA alishatoa siri hii kwenye Wiki leaks.

Tuendelee,

NSA walitumia mwaka mzima na miezi nane kuidukua namba ile ya simu.

NSA kazi yake huishia kudukua na kutuma “Transcripts” kwa CIA ili wao ndio wachakate kilichomo.

CIA wakagundua mmiliki wake anaitwa Ahmed Al Hada raia wa Yemen

Pia CIA wakafanikiwa kujua kupitia namba ile kuwa kulikuwa kuna mkutano wa Alqaeda uliopangwa ufanyike January 5, mwaka 2000 mjini Kuala Lumpur Malyasia.

Afisa wa CIA aliyechakata taarifa hii akaandika kimemo kikisema;

‘Something more nefarious was at foot”

Akimaanish kuna harakati za kihalifu zilikuwa zinawanyemelea

Kimemo hiki alikituma kwa bosi wake pamoja na taarifa alizochakata

Kwa wakati ule CIA walikuwa na majina ya kwanza tu bila ubini wa Alqaeda watatu ambao wangeshiriki mkutano ule.

Lakini haikuwachukua muda kujua majina kamili ya mmoja wao kuwa ni Khalid Al Mihdhar

CIA wakabaini huyu ni mkwe wa mmiliki wa namba ile ya simu

CIA wakafanikiwa kumfatilia tangu anatoka Yemen hadi Dubai ili aunganishe ndenge ya kwenda Kuala Lumpur kwenye kikao

Maafisa wa CIA makao makuu wakawajulisha watu wao wa Dubai station.

CIA Dubai wakawaomba maafisa usalama wa uwanja wa ndege wa Dubai wawasaidie kumkagua vizuri abiria huyu akifika dubai.

Alipofika wakati anatacheck inn ili kupanda ndege ya Malaysia, begi lake likakaguliwa kwa siri na passport yake ikatolewa copy

Copy hii wakapewa CIA wa Dubai Station

Maafisa wa CIA walipopata passport ile walishtushwa kukuta ilikuwa na Visa hai inayomwezesha kuingia Marekani na ilionesha safari yake ya mwisho kwenda marekani itakuwa ni jijini New York.
Maafisa wa CIA dubai wakarudisha taarifa zile makao yao makuu Virginia kwenye dawati maalumu la Osama bin Laden

Wale nao wakawaomba maafisa usalama wa Malyasia wawasaidie kupeleleza nini kinazungumzwa kwenye mkutano wao.

Wakawapatia na tarehe ya mkutano

Lakini Malyasia walishindwa kupandikiza microphone kwenye eneo walilokutania ili kuwasikiliza (eavesdropping)

Hivyo hawakusikia lolote lakini walifanikiwa kuwapiga picha kwa siri.

Picha zile zikatumwa CIA
Baada ya kikao, watu watatu baina yao wakapanda ndege kwenda Bangkok Thailand

Mmoja wao akiwa yule Khalid Al Mihdhar aliyetoke Yemen

Makosa yalianzia hapa!

Ni kwamba CIA walichelewa kuwajuza watu wao wa Thailand station

Hadi wanawapa taarifa hii, tayari nyayo zao zilishafutika Thailand kwani walitafutwa bila mafanikio.

Hadi kufika hapa CIA walikuwa wanamjua mtu mwingine kwa jina moja tu la Hazmi.

Mwezi March mwaka ule ule wa 2000 ikimaanisha baada ya miezi miwili tangu CIA wapoteze nyayo za watu hawa, kituo cha CIA Malyasia wakawaambia CIA Thailand wapanue wigo wa msako
Haikuchukua muda kujua kuwa huyu Nawaf al Hazmi na Khalid al Mihdhar, wote kwa pamoja waliondoka kwa ndege ile ile, siku ilele waliyofika Thailand

Ndege ile ilikuwa inaelekea Los Angels.

Hii inamaanisha nini?
Inamaanisha kuwa magaidi hawa walifanikiwa kujipenyeza Marekani kwa zaidi ya mwaka na miezi nane kabla ya shambulizi la september 11

Muda wote huu, CIA hawakuwajulisha lolote idara ya uhamiaji ambao wangeweza kufatilia taarifa zao za kusafiri viwanja vya ndege wala FBI ambao waliwajibika na kuzuia ugaidi ndani ya Marekani.

Hata hivyo ndani ya muda huu, kuna wakati idara ya CIA ya kupambana na ugaidi iliazima maafisa kadhaa wa FBI wawasaidie kazi fulani.

Pale CIA akaenda special agent Doug Miller akitokea FBI

Afisa huyu alipokuwa anafanya kazi zake, akafanikiwa kuona nyaraka zinazoelezea uwepo wa magaidi wawili ndani ya Marekani.

Taarifa hii ilimshtua na akaandaa ripoti ili aitume kwa wenzake wa FBI

Lakini alipoomba ruhusa kwa aliyekuwa msimamizi wake pale CIA aliishia kuambiwa aache kwani bado ni ‘classified’ ndani ya CIA
Wakati haya yanaendelea, ndani ya Marekani Nawaf Al Hazmi aliweza hadi kununua gari kwa jina lake

Ni muda huu ndipo CIA wakawa kama wameamka kutoka usingizini na kuanza kutuma taarifa kwa Rais Bush na mshauri wake wa mambo ya ulinzi Condoleza Rice kuwa Marekani ipo kwenye hatari kubwa ya mashambulizi ya kigaidi.

Kama walivyopuuzia wao, rais Bush naye akapuuzia taarifa zile
Ni mpaka ambapo gari hili alilolinunua Hazmi lilipokuja kukutwa limepaki uwanja wa ndege wa Dulles jijini Boston ndani yake kukiwa na risiti ya kuegeshwa saa 1 na Dk 25 asubuhi ya tarehe 11 september 2001

Ndani yake kukiwa na notices za masomo ya urubani aliokuwa akifanya Nawaf al Hazmi nchini Marekani

It was already too late to catch a flight!

Lakini wakati hii hakikuwa habari kwa wakati huo..

Uliihisi nimemaliza?

Story ndio inaanzia hapa!

Sanaa, Yemen

17th September 2001

Tupo ndani ya chumba chenye kuta kuta chakavu ndani na mahabusu moja kitongoji cha Al-Ghaydah nchini Yemen katika mji mkuu wa Sanaa.

Chumba hiki ni kojawapo ya vyumba vingi vya mahabusu za siri za CIA maarufu kwa jina la Black sites.

Wanaoshikiliwa katika mahabusu hizi, hawapewi nafasi ya kuwasiliana (incommunicado) na mtu yeyote isipokuwa na anayewachukua maelezo.

Pembeni yake mtu huyu anayewahoji washukiwa anakuwa amezungukwa na askari wenye silaha madhubuti wakiwa wamefunika nyuso zao.

Kuta za mahabusu hizi hazina maandishi yoyote au kalenda ambayo itamfanya mahabusu walau kujua yuko wapi.

Kulikuwa na njia mbalimbali za kuwaharibu kisaikolojia wanaoshikiliwa ndani ya mahabusu hizi ili kukusanya taarifa za intelejensia kutoka kwao.

Mojawapo ya njia hizi ilihusisha mateso kama waterbody, kunyimwa usingizi kwa kulazwa vyumba vyenye spika zinazotoa sauti kubwa kwa usiku mzima huku taa za vyumba vyao zikiwaka muda wote.

Haya yalifanyika washukiwa wakiwa uchi wa mnyama kwenye vyumba vyenye baridi kali.

Don’t forget the free testicles surgery with the famous burdizzo

Mahabusu hii baadae ilikuja kuwa makazi ya mtu mmoja aliyekamatwa Tanzania Muhamad Al Asad aliyekamtwa jijini Dar es salaam

Leo ndani ya chumba hiki cha mahabusu, kimepata ugeni wa Ali H. Soufani

Huyu ni chotara wa kilebanoni na kimarekani na ni kachero mwandamizi wa FBI anayehusika na kesi kubwa za ugaidi.

Kachero huyu yupo hapa kufanya mahojiano na mahabusu aliyekaa kwenye kiti cha chuma

Kinachowayenganisha ni meza pana ya pembe nne

Pembeni yake yupo komandoo wa kimarekani aliye tayari tayari ‘kutoa dozi’ kwa maabusu anayetakiwa kuhojiwa na kachero huyu

Mahabusu huyu ni Nasser Al-Bahri raia wa Yemen mwenye asili ya Saudia

Mwenyewe alipenda kujiita jina la mtu aliyekuwa karibu na Mtume Mohammed la Abu Jandal (Ibn Suhayl)

Abu Jandal inamaanisha “Baba wa Kifo”

Nasser Al-Bahri alikuwa ni mlinzi wa Osama bin Laden alipokuwa Afghanistan.

Mtu huyu alikamatwa na CIA kupitia gaidi mwingine aitwaye Fahd Al Quso ambaye alihusika kushambulia manowari ya kivita ya Marekani USS Cole ilipokuwa ikijaza mafuta kwenye ghuba ya Yemen mwaka 2000

Katika mahojiano baada ya kukamatwa, Al Quso alioneshwa picha ya mtu fulani kama anaitambua.

Akakili kuitambua picha ile kuwa ni ya Marwani Al- Shehhi aliyekuwa mmmoja wa marubani wa ndege zilizotekwa kwenye shambulio la September 11

Kwa kuwa mahojiano yaliambatana na kibano, akakili tena kuwa rubani yule alikuwa akiifadhiwa Afghanstan kwenye nyumba inayomilikiwa Abu Jabal (Nasser Al-Bahr) huyu ambaye sasa hivi ndio yupo hapa kwa ajili ya kuhojiwa.

Viongozi wa juu wa Marekani walikuwa wakisubiri kwa hamu kusikia taarifa za kiintelejensia zitakazopatikana toka kwa gaidi huyu.

Macho yao yote yalikuwa Yemen
Kwenye mahojiano Nasser akamwambia kachero yule wa FBI ifuatavyo

“You can’t stop the mujahideen”

Kachero yule akamwangalia komandoo aliye pembeni yake.

Komandoo yule akampiga kope akitabasamu huku akimwangalia Abu Jabal

Ni mafunzo tu ya kijeshi waliyopitia maafisa hawa ndio yaliwafanya waonekane hawajapanic

Really jibu hilo liliwapandisha hasira,

“You’ll find that you have underestimated America,” (utakuja kufahamu kuwa ‘umeichukulia Marekani poa’ tofauti na ilivyo)

Kachero akamjibu kwa kiarabu

Kisha kachero akaongeza , “but tell me, why do you think you’ll be victorious?” (Kwa nini mnafikiri mtaishinda Marekani)

“You want to know why?” Aliuliza Abu Jandal

“Sure,” akajibiwa

I’ll tell you why,” Jandal akajibu na kuendelea..

“The hadith says, : “‘If you see the black banners coming from Khurasan, join that army, even if you have to crawl over ice; no power will be able to stop them”

Ndugu msomaji, Hadith ni kitabu cha kiimani ambacho kilijumuisha yote ambayo Mtume Mohammed SAW alielekeza na kuyatenda katika siku zake duniani. Kitabu hiki kiliandikwa miaka zaidi ya 100 baada ya kifo chake na ni kitabu kikubwa baada ya Quran tukufu.

Kwa hiyo hapa Abu Jabal ananukuu maneno kutoka kwenye Hadith ambayo yanaelezea ishara zitakazotokea nyakati za mwisho wa ulimwengu zitakapowadia.

Kuwa wataona ishara ya watu wakiwa na bendera nyeusi (bendera nyeusi ilikuwa ni bendera aliyobebwa na Mtume na wafuasi wake kwenye uwanja wa mapambano)

Watu hawa wenye bendera nyeusi watatokea Khorasan ambako ni sehemu ya kiistoria mashariki mwa Irani kati ya Magharibi (europe) na Central Asia ambako ndio jua huchomoza.

Kwa hiyo Hadith inaeleza wakionekana watu hao inabidi waungane nao hata kwa kutambaa juu ya barafu kwani hakuna atakayewashida…(Kwa kuwa watu hawa ni ma Khalifa wa Mtume)

Haya ndio maneno aliyoyasema Abu Jandal kisha akapumzika ili kuvuta pumzi ili amalizie kunukuu..
Kabla Abu Jandal hajaanza kuongea kumalizia kunukuu Hadith, yule kachero wa FBI akamalizia kipande kilichobaki kwa lugha ya kiharabu..

“…and they will finally reach Baitul Maqdis [Jerusalem], where they will erect their flags.’”

Kuwa mwishoni wataufikia mji mtakatifu wa Yerusalemu na kusimika bendera yao

Abu Jandal akashindwa kuficha mshangao wake na kuuliza…

“You know the hadith? Do you really work for the FBI?”

Akajibiwa

“Of course I know that hadith. It’s narrated by Abu Hurairah, although it’s questionable whether that actually was said by the Prophet,”

(Najua huo mstari ulielezewa na Abu Hurairah ingawa bado kuna mashaka kama kweli hayo yalisemwa na mtume”

Kachero akaendelea ..

“and I know lots of hadith. As I told you before, the image you have of America and of her people, like me, is all wrong.” (Najua sura nyingi za hadith na kama nilivyokuambia mwanzo.. nyinyi taswira mliyonayo juu ya Marekani ni tofauti kabisa)

Mmarekani akamwambia haya yote anayoyaeleza yapo ndani ya vitabu vitakatifu vya Kiyahudi kwenye agano la kale na jipya kama ilivyo kwenye Quran

Lakini vita vinavyoongelewa ndani ya vitabu hivi vilikuwa ni vya kihistoria kabla hata ya Mitume Mohammed na Isa bin Mariam

Kachero akamuuliza gaidi,

“naweza kukuuliza swali”

Akajibiwa “Sawa”

“Let me first ask you whether Christians and Jews are allowed in Mecca and Medina.” (Wakristu na wayahudi wanaruhusiwa kukanyaga Makka na Madina)

Abu Jandal akajibu

“Of course not, that’s a silly question. Everyone knows they’re forbidden. Even the Saudi Arabian monarchy, which welcomed infidels into the Arabian Peninsula, wouldn’t dare allow them in Mecca and Medina.” (Haiwezekani, hilo ji swali la kipuuzi.. kila mtu anajua hawaruhusiwi.. Hata falme za Saudi Arabia ambao wamewaruhusu makafiri kwenye ardhi yao hawataweza kuwaruhusu wafike Makka na Medina)

“Kwa nini hawaruhusiwi”? Akaulizwa

“Kwa sababu ni mahali patakatifu”
Abu Jandal akajibu

“Are you familiar with the hadith where the Prophet has dealings with
his Jewish neighbor?” (Unajua kuwa kwenye Hadith inasemwa Mtume alikuwa anashirikiana na majirani wa Kiyahudi?) Akaulizwa tena

Akajibu “Ndiyo”

Alikutana nao wapi? Akaulizwa tena

Abu Jandal akajibu “Meddina”

“Je mtume alitenda dhambi kwa kuruhusu wayahudi wakae jirani naye Medinna”?

Gaidi huyu akapiga makelele makubwa

“Mtume hajawahi Kutenda dhambi”

Akawa anavuta minyororo iliyoshika mikono na miguu yake kutaka kumvaa kachero wa FBI

Ni katika muda huu umeme ulizimika ndani ya chumba kile huku king’ora cha hatari kikilia.

Zikaanza kusikika kelele za mlango wa chumba cha mahojiano ukigongwa kwa nguvu.

Abu Jandal akafanya kitendo cha ajabu sana…

Punde tu Kachero Ali Soufani alipogeuka kupokea simu ikiyokuwa ikiita kwa fujo wakati ule.. click here to unlock the post

KELVIN OMWENGA
BY FORTUNATUS BUYOBE

Ilikuwa ni vigumu, kumuanisha mkazi wa Sirari, mpaka wa Tanzania na
Kenya, kuwa Kevin sio mtanzania wa kabila la wakulya.

Lakini alikuwa ni Mkisii kutokea Kenya ambaye alinufaika na utambulisho
wa ukulya.

Kelvin Omwenga alikuwa na umri mdogo tu wa miaka 28 wakati jeraha la
risasi lilipoupokonya uhai wake usiku wa August 21, 2020
Taarifa za kifo chake, ziliibua hisia mbalimbali mitandaoni huku wengi
wakikihusisha na kudhulumiana kwenye biashara.

Wengi waliohoji maisha ya Kelvin ambaye hakuwa na kazi inayojulikana
hata ghafla kuishi maisha ya kimilionea
Zaidi ya kuwa dalali wa magari wa kampuni ya Lystra Motors huko
Lavington, Nairobi, kwa malipo ya commissions ndogo Kevi aliwashangaza
watu alipoiacha ghafla kazi hiyo.

Naam!
Kevi akahamia barabara ya Galana na kwenda kupanga kwenye
appartement ya kifahari namba 703 ghorofa ya Saba akinayokadiliwa
kugharimu malipo ya Ksh 150,000/= kwa mwezi.

Kevi akabadili pia marafiki na kuonekana akishirikiana na marafiki wapya
wa hadhi yake.
Haikuchukua muda mrefu Kevi ikasambaa mtandaoni video ikimuonesha
Kevi akipongezwa na mtu wa kampuni iliyomuuzia Kevi gari la kifahari
aina ya Porsche Panamera wiki tatu kuelekea ya kifo chake.

Kwenye Video ile Kevi akanukuliwa akisema:-
“Asante.. Hii ni motisha kwa vijana wote watafutaji”
Gari hilo lilisemekana kumgharimu Kevi si chini ya shilingi za Kenya
milioni 14.

Swali likiwa, dalali aliyefanya kazi kwa commissions kwa miezi michache,
alipiga wapi mshindo uliompatia pesa hizi?
Nje ya hapo, Kelvin akawa mtu wa matanuzi na kujipostisha.

Akijirusha na mastaa mbalimbali jijini Nairobi na akiandaa party
mbalimbali kwenye appartement ya kifahari aliyokuwa akiishi.
Wakati bado wambea wakiyafatilia maisha ya Kevi bila majibu, ikafahamika
kuwa Kevi anatarajia kwenda Dubai, for a business trip.

Laiti angejua....
Kuwa marafiki wapya anaojihusisha nao ni watu wa aina gani, hakika
asingethubutu kucheza nao.
Marafiki hao walikuwa ni wakora haswa, wenye kesi nzitonzito kwenye
vituo mbalimbali vya polisi lakini kesi zao zilikuwa zinaisha kimyakimya.

3rd March 2011
Jomo Kenyatta International Airport
Nairobi, Kenya

Alhamisi mchana wa siku hii, rais wa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo,
Joseph Kabila alionekana akishuka kwenye dege lake katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Aliingia nchini Kenya kwa dharula bila hata kutoa taarifa ya awali juu ya
ujio wake.

Tangu anakwea dege lake, nchini Kongo, hakuna msaidizi wake yeyote
aliyejua anapoelekea.
Rubani pekee ndiye aliyekuja kufahamu anapotaka kwenda bosi wake
baada ya walinzi wake kumtaka kuomba clearance ya kutua kwenye uwanja
wa Jomo Kenyatta.

Wakati anashuka, sura yake ilionekana kuvimba kwa hasira karibu kuangua
kilio akiwa mbali kabisa na mzaha wa aina yoyote.

Kabila akapokelewa na waziri wa mambo ya ndani na moja kwa moja akaongozwa hadi Ikulu ya Mwai Kibaki. Kisha waziri mkuu Raila Odinga akatakiwa kufika pale Ikulu na watatu wale wakajifungia kwenye ofisi ya rais kwa zaidi ya masaa mawili.

Mle ndani kabila alikuwa akimlalamikia rais Kibaki juu ya kuibiwa kwa dhahabu zake zaidi ya kilo 400 na kuingizwa nchini Kenya. Akionekana kuwa anajua anachokiongea, akamtajia orodha ya majina 15 ya wanaotorosha dhahabu kutoka Kongo kuziingiza Kenya.

Katika list ile walikuwemo raia wa Kongo waishio Kenya ambao ni mmiliki WA timu ya Sofapaka Elly Mboni Kalekwa, Benoit Muke Katumbi na muasi wa Kongo Jean Mundeke Kabamba aka General Dako. In fact huyu General Dako alikuwa ni mshirika wa Johnbosco Ntaganda, mwanajeshi wa zamani wa Rwanda na kamanda wa kikosi cha waasi wa M23 kilichokuwa kinaendesha vita Kivu kaskazini.

Eneo hili la Kivu Kaskazini kuna migodi mingi ya dhahabu hivyo waasi huuza kwa magendo madini haya ili kununua silaha. Mwezi January 2011, rais Kabila alishapiga marufuku uchumbaji na uuzaji wa dhahabu kutoka maeneo hayo. Lakini kabila akaeleza biashara hiyo inaendelea kinyemela huku raia hao wa Kongo wakipewa msaada mkubwa na raia wa Kenya ambae saa nyingine hujitambulisha kama mkongoman.

Huyo hakuwa mwingine zaidi ya Paul Kobia aka Paul Ilunga Ngoei ikitokea anatakiwa awe mkongo kazini. Vijiweni akijulikana kama Paul Choma Mtanzania hakukosa kuingia pichani.. Kabila akasema Paul Kobia anashirikiana bega kwa bega na mtanzania Abunuwasi T Lubambura. Taarifa hii ya Kabila, Ikawalazimu Kibaki na Odinga kufanya ufatiliaji wa haraka.

Yumkini ukawa unajiuliza, Kabila alitoa wapi taarifa hizi, Kaa kwa kutulia, hapa ndio mwisho wa magari mabovu... Inatulazimu kurudi nyuma muda wa mwezi mmoja kisha tusafiri mpaka kwenye mbuga ya Virunga nchini Kongo 3rd Feb 2011 Goma International Airport Norh Kivu Province, DRC Majira ya jijini, ndege aina ya Gulfstream V Jet yenye namba za usajili N886DT inaonekana ikishuka chini la anga na kukamata runway ya uwanja wa Goma.

Ndani ya ndege Ile, ukimuondoa rubani, kuna abiria wawili raia wa Marekani. Mmoja ni Mukaila Lawal mwenye uraia pacha wa Marekani na Nigeria. Huyu ni kaka wa Kase Lawal rafiki wa karibu wa rais Obama. In fact Kase ni mfanyabiasha mkubwa na mwanasiasa wa Marekani ambaye amehudumu kama mshauri wa marais Bush na Clinton kuhusu ukanda wa Afrika.

Hata leo hii wakati ndege hii anayoimiliki kupitia kampuni ya CAMAC ambayo kaka yake ni mmoja wa abiria, Kase alikuwa akihudumu kama mshauri wa Obama ambaye alimteua kuwa mjumbe wa kamati ya biashara na majadiliano. Abiria mwingine ndani ya ndege hii ni Edward Carlos St.Marry, mhitimu wa chuo cha kijeshi cha West point pia mmiliki wa kampuni ya Axiom Trading company limited.

Pale uwanjani ikaonekana gari moja aina ya Land cruiser pickup mkonga ikiisogelea ndege ile. Siti ya mbele ya gari ile upande wa abiria, ilikuwa imekaliwa na Johnbosco Ntaganda. Mambo ya Kongo yanastaajabisha sana. Huyu kiongozi wa waasi ina maana alikuwa yupo kwenye uwanja wa ndege ambao pia hutumiwa na wanajeshi wa Kongo pamoja na MONUSCO bila wasiwasi wowote. Ndio maana unaona vita haviishi kwani watu wazito kama abiria hawa wapo ndani ya biashara hiyo.

Gari ile ilipoifikia ikafungua body ya nyuma na kuanza kushusha mzigo fulani. Naam! Zilikuwa kilo 475 za dhahabu safi kabisa. Kutoka kwenye ndege ukashushwa mzigo wa dola za kimarekani yapata milioni 22.5 Pesa ile akaichukua Ntaganda na gari lake likatokomea haraka. Huku nyuma wakati ndege ile ikijiandaa kutua, ikavamiwa na wanajeshi wa serikali ikiwa bado haijamaliza runway. Wazungu wale wakasachiwa na kukutwa na ule mzigo. Wakapelekwa Kinshasa kwa kabila. Kule wakaeleza kila kitu.

Kuwa walitua uwanjani pale baada ya mtu mmoja aitwaye David kuwashawishi kuwa kuna biashara nzuri ya dhahabu wanaweza kuifanya nchini Kenya. Ushawishi ukazidi baada ya wamarekani hawa kutua Kenya na kukutanishwa na mtu aliyejitambulisha kwao kama Michelle D Malonga Mtu huyu aliwaambia anaweza kuwauzia kilo 475 ya dhahabu kutoka Kongo yenye thamani ya dola za Marekani milioni 23.

Ili kuwaonesha kuwa hatanii, akawapeleka mpaka kwenye moja ya godown akawaambia wachukue sample moja wakaipime. Majibu yakatoka mazuri. Wamarekani wakalipia pesa za usafiri, bima, vibari na kodi ya mzigo ule kuingia Kenya. Naam! Wakalipa dola laki 5 mbele ya mwanasheria Punit Vadgama wa kampuni ya mawakili Shapley Barrett and Co. Advocates ya nchini Kenya Bila kujua kuwa Paul Choma alikuwa behind the scene akiuchora mchezo wote.

Baada ya malipo haya wamarekani wakarudi nchini kwao kusubiri mzigo. Mzigo haukutumwa. Walipouliza ni kwa nini ? Wakajibiwa mazingira ya kuutoa ni magumu. Kukaibuka mabishano baina yao wakitaka wapelekwe ulipo mzigo. Hii ndio ilikuwa sababu ya ndege hii kutua hapa leo baada ya kuunganishwa na watu wa Goma.

Baada ya wiki tatu (Mwezi February mwishoni 2011) ukapigwa mzigo mwingine kwenda Kenya. Safari hii ilikuwa ni tani mbili na nusu ambao ulipitishwa kwa gari mpakani mwa Uganda na Kenya kwenye miji ya Busia na Malaba. Hakukaa sawa naye mzigo wake wa kilo 400 ukapigwa.

KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA). click here to unlock the post

MAUAJI YA POLISI MBANDE.
By, Fortunatus Buyobe

Mbwana ni mfanyakazi wa duka la jumla mali ya Tariq Makame maarufu kwa jina la "Mpemba"
Duka hili lipo maeneo ya Mbagala Zakhiem wilayani Temeke
Mbwana ni mtu wa kuzingatia sana swala
Naam!
Kila ufikapo muda wa kuswali hufunga duka na kwenda masjid

Ingawa Mbwana anaishi Mbagala Kuu, mara chache, majira ya usiku henda Mkuranga mkoani Pwani kijijini Kisiju "kwa Mnyabudu"
Ilikuwa ni vigumu sana kutabiri tabia za Mbwana
Mara nyingine saa 12 jioni angeenda Mbande kwa bodaboda kuangalia ratiba fulani inayojurudia.
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA). click here to unlock the post

LICENSE TO KILL .
By Fortunatus Buyobe

(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA). click here to unlock the post

THE FIXER -

Tarehe 17 May 2012, taifa letu lilishuhudia tukio ambalo limetokea mara moja tu kwenye historia na bado halijajirudia hadi sasa. Majira ya saa 4 na dk 45 asubuhi msafara wa rais mkapa ulionekana ukiingia kwenye viunga vya mahakama ya hakimu mkazi kisutu.

Wananchi walihisi ni kama mzaha waliposoma gazeti la Mwanahalisi la April 14 mwaka mmoja nyuma, gazeti hilo lilipovujisha kiapo cha rais Mkapa alichokitoa mbele ya wakili Mabere Marando. Pia hata gazeti la Mwananchi lilipovujisha barua ya wakili Marando kwenda kwa katibu mkuu kiongozi Philemon Luhanjo, watu bado walichukulia ni mzaha Wakili Marando alikuwa amemwandikia Philemoni Luhanjo kumuandaa rais Kikwete kufika mahakamani kama shaidi wa utetezi.

Barua ile kwenda kwa Kikwete haikujibiwa pamoja na jitihada za wakili Marando kukumbushia Sasa watu wakiwa na ile hali ya kutoamini, ndipo Mkapa anaonekana hapa mahakani muda huu, siku hii Waandishi wa habari walihaha kupata picha za Mkapa na walinzi walifanya jitihada kuzuia Mkapa aliongozwa moja kwa moja katika chumba maalumu cha hadhi yake pale mahakamani akisubiri muda wake wa kutoa ushaidi Naam, Rais Mkapa alikuwa ni shaidi dhidi ya mtuhumiwa Prof.

Costa Mahalu,aliyekuwa balozi Italia, pamoja na Grace Martin aliyekuwa afisa utawala wa ubalozi Ni kwamba, January 22 mwaka 2007, Mahalu alipandishwa mahakamani na kusomewa shitaka la kuhujumu uchumi katika kesi No. 1 ya mwaka 2007 Balozi akituhumiwa kutumia vibaya madaraka na kuisababishia hasara ya bilioni 2.9 serikali ya Tanzania Ilidaiwa kuwa balozi Costa alitenda hayo akiwa ni balozi wa Tanzania nchini Italia Sept 22 mwaka 2002 ambapo alinunua jengo la ubalozi wa Tanzania na malipo kuingizwa kwenye akaunti mbili tofauti za mlipwaji kwa nia ya kumuibia muajiri wake.

Majira ya saa 5 na Dk 32 rais Mkapa akawa tayari mbele ya hakimu mkazi Ilvin Mgeta akitoa ushaidi wake. Mkapa, akiongozwa na wakili Alex Mgongolwa aliyekuwa akimtetea Mahalu alitoa ushaidi ufuatao. Mgongolwa: Mwaka 1995 hadi 2005 ulikuwa wapi?

Mkapa: Nilikuwa Dar Es Salaam nikishika wadhifa wa urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

Mgongolwa: Unafahamu nini kuhusu ununuzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini Italia

Mkapa: Nafahamu balozi wetu alifanya ununuzi wa jengo hilo kwa Euro 3,098,741.40 kwa maelekezo ya serikali ya Tanzania

Mgongolwa: Mlipewa masharti yoyote kwenye ununuzi?

Mkapa: Ndiyo! Muuzaji alitaka aingiziwe malipo kwenye akaunti mbili tofauti, zote zikiwa na majina yake.

Mgongolwa: Mlipata malalamiko yoyote kutoka kwa mnunuzi au serikali ya Italia?

Mkapa: Hapana

Wakili Alex Mgongolwa akaanza kusomea rais Mkapa maelezo ya rais Kikwete aliyoyatoa bungeni wakati huo akiwa ni waziri wa mambo ya nje. Kikwete alitoa maelezo haya wakati anachangia bajeti ya wizara yake ya mwaka 2001/2002 Maelezo ya Kikwete yalieleza kuwa

“Serikali imenunua jengo la ubalozi Italia kwa Euro 3,098,741.40 baada ya kufata ushauri wa wizara ya ardhi na Ujenzi hivyo utaratibu wote ulifuatwa.”

Mgongolwa: Maelezo haya ni sahihi

Mkapa: Ni sahihi

Mgongolwa: Mbona katibu mkuu wako kiongozi bwana Marten Lumbanga ambaye ni shahidi wa kwanza wa Jamuhuri anadai hakujua manunuzi haya?

Mkapa: Nimeshangaa kusikia anasema hajui. Rais siwezi kujua juu ya kitu na katibu mkuu kiongozi asijue.

Mkapa akaendelea kueleza kwamba ameshangaa kuona Mahalu akishitakiwa kwa jambo hilo na hajui nani aliyeagiza upelelezi juu ya jambo hilo hadi kumshitaki. Mkapa akaeleza hajui kama upelelezi ulianza akiwa madarakani au ameshataafu.

Alishtukia tu Mahalu anapandishwa kizimbani Baada ya Alex Mgongolwa kumaliza kumuongoza Mkapa, ikafata zamu ya upande wa mashitaka kum”cross-examine” Akaingia ulingoni wakili wa serikali Ponsiano Lukosi Lukosi: Huoni kama dai la muuzaji kutaka kulipwa kwenye akaunti mbili tofauti ulikuwa ni ukwepaji wa kodi?

Mkapa: Hilo si tatizo langu. Ni tatizo la nchi yake. Mimi nimepata jengo nililotaka..., Alhamdulilah.

Lukosi : Huu sio wizi wa mshtakiwa?

Mkapa: Nitashangaa sana Mahalu kuwa mwizi, na nitakushangaa wewe. Mahalu ni msomi mzuri, na mtumishi mwaminifu sana. Mkapa akataka kusema kitu kisha akasita Akamwambia Lukosi asimchokoze asije akasema mangine yasiyohitajika.

Majira ya saa 7 na Dk 8 rais Mkapa alikuwa ameshamaliza kutoa ushaidi wake Ina maada Mkapa alitoa ushaidi kwa zaidi ya muda wa saa moja na Dk 30 akimpambania balozi wake Mahalu. Mahalu hakukutwa na hatia kwenye kesi kesi hivyo aliachiwa huru.

Wakati anatoa hukumu, Hakimu mkazi Irvin Mgeta alitumia nadharia ya Principal na Agent Kuwa Principal (Serikali) ilimpa “Power of attorney” Agent (Balozi) kufanya kila kitu ubalozini akiiwakilisha Jamuhuri ya Tanzania kisha baadaye analalamikia Power aliyompa Mgeta alifananisha hali hiyo ni sawa na mtu aliyeijaza bastola risasi, akaikoki, akajielekezea na kuifyatua Kisha mtu huyo alalamile risasi imemuua Baadaye katika uzinduzi wa kitabu chake, rais Mkapa alieleza kuwa aliamua kumtetea Mahalu kwa kuwa aliona anaonewa.

Naam! Rais Kikwete aliingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa October 2005 alipoibuka kidedea. Sera yake ya kasi mpya, nguvu mpya na hari mpya, ikimbeba dhidi ya wapinzani wake kwenye uchaguzi huo. Miaka miwili tangu ushindi wa Kikwete, tukaanza kushuudia kesi kubwa dhidi ya viongozi wakubwa wa iliyokuwa serikali ya mtangulizi wake ambaye yeye alimtumikia kama waziri.

Kesi ya kwanza ilikuwa ni hii ya Mahalu iliyofunguliwa mwaka 2007 Mahalu alikuja kutoa ushaidi uliokuja kuichanganya vibaya kambi ya mashtaka Takukuru waliokuwa wakitumia kama ushaidi barua ya Mahalu aliyoandikia serikali Feb 2, 2002 kuijulisha kuwa amefikia hatua ya ununuzi wa jengo, walishtushwa na nyaraka alizoibua Mahalu mahakamani Mahalu alikubali kweli ile ni barua aliyoandaa mwenyewe na aliituma kwa mabosi wake Katibu mkuu na Waziri wa mambo ya nje (Kikwete) Pia aliwanukuu Katibu Mkuu (Lumbaga) Kiongozi, Waziri wa fedha (Mramba) na Kamishina wa bajeti wa wizara ya mambo ya nje. Mahalu akaeleza barua ile waliyonayo TAKUKURU ilikuwa na viambatanisho 11 ambavyo hajui ni kwa nini hawajavitumia kwenye ushaidi Sasa Mahalu akawa anashambulia kwa ngumi za “below the belt” kuusambaratisha upande wa mashtaka Mahalu akatoa mahakamani ripoti ya bwana Kimweri aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa majengo katika wizara ya ujenzi Akaeleza kuwa Kimweri alisafiri hadi Roma Italia July 15 hadi 26 mwaka 2001 ili kwenda kutathimini majengo matatu aliyokuwa ameyapendekeza yanunuliwe na wizara Majengo hayo yalikuwa ni (SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MWENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

IFAHAMU BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA .

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE.

DISCLAIMER:

Marehemu huwa haongelewi kwa mabaya, Lakini matendo yao hapa duniani hayatufungi mikono kuyajadili kwa ajili ya mafundisho ya vizazi vijavyo.

80% ya Madawa ya kulevya yanayopatikana Tanzania, Si kwa ajili ya watumiaji wa ndani.

Naam!

Madawa haya si kwa ajili ya soko la Tanzania ingawa yanapatikana kwa wingi nchini kwetu.

Tanzania ni kama lango tu(Corridor) kwa ajili ya kupitisha madawa haya mpaka kwenye soko lililokusudiwa (Target Market)

Ni kwa nini yasitumike ndani wakati walaji wapo hapa hapa?

Jibu ni jepesi sana,

Gharama!

Yes , Gharama!

Madawa haya huwa ni very expensive kwa watumiaji wa ndani kuweza kuyamudu. Ni watanzanzia wachache wenye uwezo wa kumudu gharama za madawa haya.

Ni kwa sababu hii walaji wengi wa ndani huishia kula makapi (by products) aka “Ngada”

Makapi haya ndio huwa na madhara makubwa kwa mtumiaji kuliko wale wanaotumia kitu “pure” kabisa.

Ok.Tumejua kuwa Tanzania ni njia tu!

Je “Mzigo” hutoka wapi na kwenda wapi?

Here we are!

Nifatilie taratiiibu nikielezea habari hii kwa kunuu Chanzo.

“Mzigo huwa unatoka either “Kwa Pele” au “Kwa Musharaf”

Ndugu Msomaji, Popote litakapotumika neno “Kwa Pele” jua ni Brazil na “Kwa Musharaf” Jua ni Pakistani.

Hizi nchi huitwa kwa Codes hizo ndani ya Ulimwengu wa wasafirishaji.

Kwa hiyo mzigo unatoka Brazil au Pakistani

“Mzigo ukitoka huko anapewa mbebaji mmoja ambaye husafirisha kwa kuyameza mpaka Dubai.

“Hasafiri bila mipango kuwa imesukwa tangu anakotoka mpaka Dubai”

“Akifika Dubai Safari yake inaishia pale na analipwa kabisa Chake pale pale.”

“Anaishia pale kwa Sababu Passport ikisomeka imegongwa mihuri ya Kwa Pele au Musharaf basi maafisa Ukaguzi viwanja vya ndege huwa makini sana na mzigo wowote uliobeba”

“Ili kuepusha mzigo kudakwa inabidi mtu wa kwa pele au Musharaf aishie Dubai”

“Tangu mzigo unapotoka shambani, tayari anakuwa ameshaandaliwa “punda” mwingine ambaye atameza ule mzigo pale Dubai na kuuvusha mpaka Msumbiji”

“Huyu naye ataishia Msumbiji tu na kulipwa Chake”

“Kutokea Tanzania, Punda mwingine atavuka mpaka Msumbiji kwa kukata passport ya masaa 24 tu”

“Si rahisi maafisa usalama kumshtukia mtu huyu ambaye kavuka tu Kuingia Msumbiji na baada ya Masaa katoka”

“Punda huyu ndiye atakayemeza mzigo wa Msumbiji na kuuingiza Mtwara/Lindi”

So ndugu Msomaji Umeona “Triangle of Custody” ya Mzigo kuanzia shambani mpaka umefika mikoa ya Kusini.

Njia unavyokuja haiachi traces zozote kwa yule aliyefanikiwa kuufikisha kwenye point aliyoelekezwa.

Huwa kuna Viapo na binadamu anawezwa kutumika kama “bond” ya kiapo.

Mzigo Ukifika kusini, Sio mwisho wa safari, Mzigo ule hukutana na wakemia wenye uwezo wa kucheza na Molecular formula ya fawa zile kuzifanya zisomeke kama raw materials ya dawa zilizokubalika kwa matumizi ya binadamu. (Refer HYDROCARBONS)

Naam!

Wanageuza nyekundu kuwa Njano.

Kuanzia hapa sasa ndio matawi ya Kusambaza mzigo huu yanapoanzia either kwenda nchi kama Congo, Nigeria, South Africa mpaka kwa watumiaji wenyewe kabisa Marekani, China etc.

Leo nashuka na Mkasa wa mabinti wawili walioingia kwenye biashara hii mwaka 2013.

Katika mkasa huu ndipo ilipoonekana kuwa mapambano dhidi ya biashara hii ni sawa na kujichimbia kaburi lako Mwenyewe.

Melisa Edward alikuwa ni mfanyakazi katika mgahawa mmoja maaarufu sana karibu na yule askari “aliyepanga “jab” kama Mandonga”

Naweza kuthibitisha kuwa Mgahawa ule ulikuwa unamilikiwa na Jamaa flani ambaye alikuwa karibu na mtoto wa mkuu mmoja wa kisiwa.

Kuishi mjini kwa kujichanganya kuna raha yake.

Nilikuwa napenda sana kupata lunch karibu na mgahawa fulani hivi mjini kati.

Mama mmiliki wa mgahawa ule tukazoeana tukajenga ukaribu wa kindugu hadi nikawa mshikaji sana wa mtoto wake mmoja.

Mtoto wake was a so Connected Man.

Siku Moja akanipa Mwaliko

Oyaaa!

“Fortu Shika Card hii, Leo jioni njoo kuna lounge ya mshkaji inafunguliwa Usikose”

Siku hiyo kulikuwa kuna fainali ya UEFA Chelsea Vs Bayern Munich ilikuwa mtoto hatumwi dukani.

Nilipofika pale nilishangaa ulinzi wa kutisha uliokuwa pale nje plus magari ya kifahari yaliokuwa yameegeshwa.

Mpaka unaingia ndani upekuzi sio wa mchezo.

Naam!

Kule ndani nikakuta “wenye mji wao” kweli wameenea.

Nikajiangalia mimi kweli wa kupewa mwaliko huu?

Lakini si unajua wabongo wengi ni “Washamba Shapu”?, hivyo nikaficha mshangao nikavaa uenyeji.

Kwa nini napiga story hii?

Fatana nami.

Pale ndani nilijithibitishia kuwa yule jamaa anayefungua mgahawa lazima ana ukaribu sana hata kumfanya “somebody” aje pale kushiriki tukio la uzinduzi.

Sasa Miezi kadhaa mbele Kukatokea tukio lililomuhusisha huyu binti aliyekuwa mhudumu kwenye huu mgahawa.

Ilikuwa hivi

Jioni ya tarehe 4 July 2013 binti huyu alikuwa kazini lakini akiwa kwenye mazungumzo nyeti na boss wake.

Ni kama walikuwa wanaelekezana “rehearsals” za mwisho mwisho kwani usiku huo binti alitakiwa kujipanga kwa Safari.

Baadaye akaingia jamaa mwingine anayetumia jina la shujaa maarufu aliyepotosha wanajeshi wenzie kuita risasi maji.

Naye akaingia kwenye mazungumzo yale.

Usiku ule ule dada wa Muhudumu yule akifanya tambo mitandaoni kwa kupost akiwa na pesa ndefu.

Tayari walishapewa Chao!

Baadae kwa msaada wa Closed Circuit Camera Television (CCTV) footage iliyopo uwanja wa ndege Dar Es Salaam ya Muda wa dakika 65 mambo yalikuwa ifuatavyo

Majira ya Saa 10:15 Usiku Yule Mhudumu, Dada yake na yule mwenye mgahawa wakaonekana waliingia kwenye eneo la Uwanja wa ndege Dar Es salaam.

Lakini kabla ya ujio wao saa 9:45 anaonekana Polisi kwenye camera akizunguka zunguka nje ya chumba cha ukaguzi kama anayesubiria mtu

Polisi huyu anafahamika kuwa ni Corporal Ernest

Camera inamwoshesha pia Mbeba Mizigo akiangalia saa na kuongea na simu kama anapokea maelekezo fulani.

Huyu mbeba mizigo (porter) wachawi wakamtmbua kuwa ni Zahoro Mohamedi Selemani.

Mara Paap, Wale mademu na bosi wao wanaonekana wakisogelea dawati la Ukaguzi.

Wakiwa sasa na Mabegi tisa yanayofanana.

Yule askari (Corporal Ernest) anaanza kusaidia abiria kuweka mizigo yao kwenye Scanner.

Kumbuka hii haikuwa kazi yake!

Pale pale anaonekana afisa mmoja wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege (TAA) ambaye anajulikana kwa jina la Yusuph Daniel Issa akimtoa mwenzie aitwaye Jackson Manyonyi kwenye scanner na yeye kujiposition pale.

Anatumia dakika sita kuyapitisha mabegi 9 kwenye Scanner kuanzia saa 10:16 mpaka 10:22 usiku

Anapomaliza kuyapitisha anatoka kumruhusu afisa wa mwanzo aendelee na kazi.

Kazi yake Mola haina makosa,

Lakini kazi ya binadamu ina makosa.

Yakafanyika makosa matatu yaliyowagharimu.

Kwanza afisa yule wa TAA aliyemtoa mwenzake ili apitishe yale mabegi hakujiandikisha katika kitabu (Screeners Logbook) kama utaratibu ulivyomtaka.

Alipomaliza kuyavusha mabegi yale akatoka na kwenda kunong’ona jambo na yule polisi( Ernest) ambaye pale halikuwa eneo lake la kazi na baada ya hapo akaenda tena kunong’ona na afisa mwenzake wa TAA (Jacksoni Manyonyi) ambaye sasa alisharudi kwenye Scanner.

Kumbe Wachawi wanaangalia tu.

Pili, Yule afisa wa TAA mvusha mabegi alikuwa akizungumza na simu muda wote wakati pale simu haziruhusiwi lakini incharge wake aitwaye Juliana Thadei alionekana kwenye Camera akiwa katulia bila kuzua hayo yasitendeke.

Sio yeye tu, hata Security officer mwingine wa TAA aitwaye Mohamed Kalungwa naye anaona mchezo wote ukiendelea lakini akauchuna tu.

Tatu, Yule Boss wa wale mademu alikuwa ameingia eneo la Ukaguzi (Checking Inn) bila ya kuwa amekata ticketi hivyo hakutakiwa kabisa kuwa eneo lile

(Subscribe hapo chini kupata muendelezo wa mkasa huu na nyingine nyingi kwa mwezi mzima.) click here to unlock the post