Thread by Fortunatus Buyobe- CHINA PLAZA

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
MAFUNDI SIMU CHINA PLAZA
Kuna wakati unaweza unaweza kushindwa kusafiri kwa sababu tu
basi ulilopanga kusafiria limekuacha baada ya kuchelewa.
Hupaswi kujilaumu kama hili litakutokea.
Mara nyingine Mungu huwa anaingilia kati ili kukuepusha na baya
ambalo lingeweza kukutokea endapo ungekuwa ndani ya basi hilo.
Ni mara ngapi tumesikia watu wakitoa shuuda kuwa gari fulani
lilimuacha na kisha mbeleni gari hilo likapata ajali?
Hili ndilo lililomtokea Moses John miaka miwili iliyopita.
kijana huyu ni muuza simu katika jengo la CHINA PLAZA lililoko
mtaa wa Aggrey Kariakoo.
Tarehe 26 December mwaka 2021, vijana kadhaa ambao wote wanajishughurisha kuuza simu kwenye jengo hilo, walikubaliana waende wakasherehekee sikukuu ya Christmas katika fukwe za
Kigamboni.
Majira ya saa 6 mchana, Kijana mwingine aitwaye Rajab Mdoe aka Choiya akampigia simu mama yake mlezi aitwa Taabu Said Banga (Rajabu ni mtoto wa marehemu mdogo wake na Taabu)
Haya ndio yalikuwa maongezi yao
Rajab: Mama, utatumia gari lako leo?
Bi Taabu: Hapana, Kwa nini unaniuliza hivi?
Rajab: Nataka kulitumia…Leo tunataka kwenda beach Kigamboni
na rafiki zangu
Bi Taabu: Hakuna shida. Unaweza kulitumia.
Bi Taabu anaishi Tabata Kinyerezi wakati mwanae anaishi
Bonyokwa
Majira ya saa 8 mchana, Rajabu akafika Kinyerezi akiwa
ameambata na rafiki yake aitwaye Tawfiq Mohamed.
Baada ya mazungumzo na mama yake, wakachukua gari aina ya Toyota IST jeusi kwa rangi.
Wakaeleza kuwa wanampitia tena rafiki yao mwingine aitwaye
Hemed Abass
Wakaondoka.
Makutano (RV) baina ya vijana hawa na wengine walionuia kwenda Kigamboni, ilikuwa ni Kariakoo wanakofanyia kazi.
Mpaka gari inafika kariakoo waliwakuta vijana wenzao ambao ni
Edwin Kunambi na Seif Swala
Ambaye hakuwa amefika ni Moses John ambaye alichelewa kufika
walipokubaliana wampitie hivyo wakamuacha.
This was a lucky accident to Moses!
Kwa nini nasema hivi?
Ni kwa sababu vijana wale hawakuonekana tena kwa macho ya
kibinadamu as the became microscopic.
Walipotea kama sindano!
Neno la mwisho kutoka kwao ulikuwa ni ujumbe ambao Edwin alimtumia Moses kuwa wamekamatwa wakiwa eneo la Kamata na
wanapelekwa kituo cha polisi cha kati.
Rafiki zao wa Kariakoo, wakaenda kuwafatilia central polisi lakini majibu yakawa ni hawajafikishwa pale.
Jitihada zikahamishiwa kwenye vituo vya Oysterbay, Msimbazi, Salender Bridge lakini nako wakaambulia patupu.
Hadi wakati huu, ndugu wa wazazi hawa hawakuwa na taarifa kuwa
watoto wao wamekamatwa.
Majira ya saa 4 usiku, Bi Taabu alimpigia mwanae simu kumuuliza kama amesharudi.
Simu ile iliita bila kupokelewa.
Majira ya saa 6 usiku alipojaribu tena kumpigia mwanae, simu ilikuwa haipatikani.
Akaamini labda imeishiwa chaji akaamua kwenda kulala.
Hali hii ilikuwa pia kwa mzee Longili Martin baba wa Edwin Kunambi
Yeye hakujishughurisha kabisa kumpigia mwanae kwani alishaongea na mwanae alipompigia kumtaka ajumuike naye
kusherehekea sikukuu ya Noel nyumbani kwake Gongolamboto.
Edwin akamjibu hataweza kufika kwani ametingwa na shuguri
lakini akamwambia baba yake atajumuika naye kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya.
Hivyo Mzee Longili naye hakuwa na fununu juu ya yaliyomsibu mwanae Edwin
Siku ikapinduka...SUBSCRIBE HAPO CHINI KUENDE;EA KUSOMA MAKALA click here to unlock the post

NANI ALIAGIZA MAUAJI YA BARKE?

Usiku wa kuukaribisha mwaka 2022 ulianza kwa sherehe, lakini ukamalizika kwa fumbo la kutisha. Barke alionekana akiondoka Kitambaa Cheupe akiwa kwenye bodaboda pamoja na mwanaume aliyejulikana kama “John Cena”—siku iliyofuata mwili wake ukapatikana katika nyumba ya wageni. Kamera za CCTV zilizofutwa, picha zilizopigwa kwa siri, rafiki aliyetoweka na madai ya muuaji kukodiwa vinaacha swali moja kubwa: Ni nani hasa aliyekuwa nyuma ya mpango huu—na kwa nini? SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

THE BAG KILLER

9th Feb 2009

JKN International Airport

19:30 HRS

Giza likiwa limeshaanza kuumeza mji wa Dar Es salaam, majira ya saa moja na nusu usiku, wanaingia watu wawili kwenye kwenye kaunta ya wa abiria waendao nje ya nchi ( International Departures)

Uingiaji wao ukawavutia wanausalama

Ni kwamba askari hawa waliweza kubaini wasiwasi mkubwa aliokuwanao mmoja wa abiria mwenye asili ya Asia ambaye alikuwa ameambatana na mkewe uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKN

Mwanzoni walihisi labda ni mtu aliyebeba madawa ya kulevya

Ukaongezeka umakini juu yao

Abiria hawa wakaongoza kwenye dirisha la shirika la ndege la India.

Kwa mujibu wa ratiba iliwapasa wawe angani nusu saa tu ijayo kuelekea Bombay India

Wakati wa ukaguzi (Check inn), manjagu waliimulika kwa “jicho la tai” mizigo yao bila kubaini lolote

Hata walipowakagua wao ilikuwa vile vile

Lakini wasiwasi mkubwa haukuondoka machoni mwa yule abiria wa kiume.

Wakaomba nyaraka zao za kusafiria

Majina yao ndiyo yaliwafumbua macho sababu ya mwanaume yule kuwa na wasiwasi wakati wote.

Let’s pause at this Juncture,

Tarehe 8 February 2009, vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam, viliripoti habari mpasuko (Breaking news)

Hii ni kutokana na ugunduzi fulani uliokuwa umefanyika kwenye moja wapo ya jengo katika viunga vya mitaa ya Posta, barabara ya Samora.

Haukuwa ugunduzi mzuri!

Naam!

Wanafaa kuitwa vijana kwa sababu mmoja alikuwa na miaka 23 na mwingine miaka 21

Vijana wawili wenye asili ya Asia walikuwa wameonyeshana “usmart”

Ambao ndio hasa ulisababisha habari hii mpasuko click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE — FBI IN TANZANIAN SOIL

Tarehe 7 August 1998 jiji la Dar lilitikisika.

Majira ya saa 4:45 asubuhi, Maafisa wawili wa Polisi wakiwa katika kituo cha polisi Salender Bridge, walishtuliwa na Kishindo Kikubwa. Maafisa hawa ni SSP Mohamed Stambuli na ASP Valentino Mlowola.

Naam! Fuatana nami!

Kwa maelezo ya SSP Stambuli, alieleza kwamba majira hayo alisikia kishindo kikubwa ambacho kililifanya anga kuwa jeusi kwa wangu mazito ya moshi, vumbi na vyuma vikiruka angani kutoka majengo ya jirani na ofisini kwake.

Haikuchukua muda mrefu kwa maafisa hawa kubaini kuwa, kishindo kile kilitokea katika jengo la ubalozi wa Marekani ambalo halikuwa mbali toka pale kituoni mwao.

Ilikuwa ndio mara ya kwanza kwa taifa hili kuonja machungu ya uhalifu mpya kwa jina la "Ugaidi". Achana na ugaidi wa mchongo wa Kina Mbowe au ule wa Kibiti, Amboni na Mkuranga! Huu ndio ulikuwa ugaidi ambao ulilenga moja kwa moja kwa aliyeanzisha vita vya ugaidi yaani Taifa la Marekani.

Magaidi hawakujali kama wanapambana na Mmarekani nje ya ardhi yake. They didn't care!

Tukio hili lililikuta taifa letu likiwa halijajiandaa kabisa kukabiliana na janga hili. Hii ni baada ya Idara yetu ya "Crime Investigation Department" CID kubaini kuwa wasingeweza kufua dafu kupeleleza kisa kile kilichohitaji wataalamu wa Forensic science na Engineering.

Yes! Kwa wakati ule idara yetu haikuwa imepiga hatua kwenye mambo ya Forensic science au kutatua uhalifu wa kiinjinia. Kutokana na hilo Idara yetu ilibidi isalimu amri na kuwaomba wataalamu wa FBI wasaidie upelelezi ule.

Sote tunajua jinsi ilivyo vigumu kwa taifa moja kuruhusu wapelelezi wa nje kuchunguza visa vya ndani. Katika sakata hili hakukuwa na njinsi. Ombi la Tanzania kwa FBI likapokelewa kwa furaha kubwa kwani taifa la Marekani lilikuwa lina maslahi kwenye tukio lile.

Kwa upande wa Tanzania ikaundwa timu maarumu ya kikachero wakiwemo SSP Stambuli, ASP Mlowola, SSP Samson Kassala na wengineo. Hawa walikuwa wakipokea maelekezo kutoka kwa maafisa wa FBI moja kwa moja.

Timu hii ikasogela eneo la tukio ambapo walikuwata RPC RCO na wengineo. Pale kazi ya kwanza ilikuwa ni kuwapeleka majeruhi Muhimbili, kuopoa maiti 11 na kupunguza taharuki.

Mpaka muda huo hakuna yeyote aliyekuwa na tetesi yoyote juu ya nani hasa anaweza kuwa mshukiwa/washukiwa wa tukio lile.

Baada ya hali kutulia, ikaanza Crime scene Investigation. Maafisa hawa wakashuhudia uharibifu ulioachwa na kishindo cha mlipuko ule. Magari mengi yakiwa yameharibiwa "beyond repair". Moto ulikuwa bado ukiwaka na askari mmoja wa kitete akasikika akisema "Hili ni bomu la Hiroshima". Hii ni kutokana na jinsi Bomu lilivyochimba ubalozi.

Vitu vingi vikaokotwa eneo la tukio na kuanza kuchunguzwa kwa umakini. Maafisa wa FBI wakavutiwa na kipande kimoja cha Chuma. Kipande hiki cha Chuma ndicho kilikuja kuwa muongozo wa muhimu sana katika kutatua fumbo la juu ya nani hasa alilipua bomu lile.

Kipande kile cha Chuma, kiliaminika kuwa ni cha Chassis ya gari iliyotumika kubeba bomu lililolipuka kwenye ubalozi ule. Baada ya uchunguzi wa kimaabara wa maafisa wa FBI kwa Laboratory Photographic Enlargement, walifanikiwa kupata namba fulani kutoka kwenye chuma kile. Namba hiyo ilikuwa ni MH40-06050 (Kielelezo namba 6 cha FBI).

Msako ukaanza kwa kuyahoji Makampuni mbalimbali yanayohusika na kuingiza Magari nchini kama walishaingiza gari lenye ile namba ya Chassis. Wakafanikiwa kuipata kampuni moja!

Naam! It was JABA MOTORS COMPANY!

Ndiyo! Kampuni ile ndiyo iliingiza nchini gari aina ya NISSAN ATLAS, ya tani mbili, yenye Model namba MH40, Engine namba ED 33-50626 na Chassis No. MH40-06050.

Naam! Gari ile ilisajiliwa kwa namba TZH 6134 na iliuzwa kwa AMANI JUMA KASINYA.

Mnunuzi wa gari ile akakamatwa na kuwekwa Makwaya. And upon a gentle interrogation that involved a promise of free testicles surgery, Mnunuzi akaeleza mambo kinagaubaga!

Alieleza kuwa ni kweli alinunua gari ile, lakini alishaiuza. Akaeleza kuwa gari ile ilikuwa ina friji kubwa kwa nyuma ambayo alikuwa akiitumia kusafirishia samaki kutoka Tanga mpaka Dar. Akatoa mkataba wa Mauziano wa tarehe 17 June 1998 kuwa alimuuzia mtu aitwaye Mohamed Sultan Said kwa bei ya Tshs milioni 3.5.

Ikawa ni msako wa nyani ngedere haponi! Na yamkutayo Mamba na Boko yatamkuta. A manhunt now launched towards the said Mohammed Sultan Saidi.

Naye Mohamed Sultan alipodakwa akaeleza jinsi alivyouza gari ile kwa watu wawili wenye asili ya Kiharabu kupitia kwa dalali SLEIYUM SULEIMAN SALUMU JUMA.

Dalali naye akadakwa. Katika mahojiano, dalali huyu akaeleza kuwa tarehe 27 July 1998 akiwa katika hotel ya AL-NOOR mnazi mmoja alifatwa na vijana wawili mmoja mrefu na mwingine mfupi wenye asili ya kiarabu wakitaka awauzie gari ambayo ilishapelekwa kwake kutafuta mnunuzi...Subscribe hapo chini kusoma makala kamili click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
THE FIXER
Tarehe 17 May 2012, taifa letu lilishuhudia tukio ambalo limetokea mara moja tu kwenye
historia na bado halijajirudia hadi sasa.
Majira ya saa 4 na dk 45 asubuhi msafara wa rais mkapa ulionekana ukiingia kwenye
viunga vya mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Wananchi walihisi ni kama mzaha waliposoma gazeti la Mwanahalisi la April 14 mwaka
mmoja nyuma, gazeti hilo lilipovujisha kiapo cha rais Mkapa alichokitoa mbele ya
wakili Mabere Marando.
Pia hata gazeti la Mwananchi lilipovujisha barua ya wakili Marando kwenda kwa katibu
mkuu kiongozi Philemon Luhanjo, watu bado walichukulia ni mzaha
Wakili Marando alikuwa amemwandikia Philemoni Luhanjo kumuandaa rais Kikwete
kufika mahakamani kama shaidi wa utetezi.
Barua ile kwenda kwa Kikwete haikujibiwa pamoja na jitihada za wakili Marando
kukumbushia
Sasa watu wakiwa na ile hali ya kutoamini, ndipo Mkapa anaonekana hapa mahakani
muda huu, siku hii
Waandishi wa habari walihaha kupata picha za Mkapa na walinzi walifanya jitihada
kuzuia
Mkapa aliongozwa moja kwa moja katika chumba maalumu cha hadhi yake pale
mahakamani akisubiri muda wake wa kutoa ushaidi
Naam, Rais Mkapa alikuwa ni shaidi dhidi ya mtuhumiwa Prof. Costa
Mahalu,aliyekuwa balozi Italia, pamoja na Grace Martin aliyekuwa afisa utawala wa
ubalozi
Ni kwamba, January 22 mwaka 2007, Mahalu alipandishwa mahakamani na kusomewa
shitaka la kuhujumu uchumi katika kesi No. 1 ya mwaka 2007
Balozi akituhumiwa kutumia vibaya madaraka na kuisababishia hasara ya bilioni 2.9
serikali ya Tanzania
Ilidaiwa kuwa balozi Costa alitenda hayo akiwa ni balozi wa Tanzania nchini Italia Sept
22 mwaka 2002 ambapo alinunua jengo la ubalozi wa Tanzania na malipo kuingizwa
kwenye akaunti mbili tofauti za mlipwaji kwa nia ya kumuibia muajiri wake.
Majira ya saa 5 na Dk 32 rais Mkapa akawa tayari mbele ya hakimu mkazi Ilvin Mgeta
akitoa ushaidi wake.
Mkapa, akiongozwa na wakili Alex Mgongolwa aliyekuwa akimtetea Mahalu alitoa
ushaidi ufuatao.
Mgongolwa: Mwaka 1995 hadi 2005 ulikuwa wapi?
Mkapa: Nilikuwa Dar Es Salaam nikishika wadhifa wa urais wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania
Mgongolwa: Unafahamu nini kuhusu ununuzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini
Italia
Mkapa: Nafahamu balozi wetu alifanya ununuzi wa jengo hilo kwa Euro 3,098,741.40
kwa maelekezo ya serikali ya Tanzania
Mgongolwa: Mlipewa masharti yoyote kwenye ununuzi?
Mkapa: Ndiyo! Muuzaji alitaka aingiziwe malipo kwenye akaunti mbili tofauti, zote
zikiwa na majina yake.
Mgongolwa: Mlipata malalamiko yoyote kutoka kwa mnunuzi au serikali ya Italia?
Mkapa: Hapana
Wakili Alex Mgongolwa akaanza kusomea rais Mkapa maelezo ya rais Kikwete
aliyoyatoa bungeni wakati huo akiwa ni waziri wa mambo ya nje.
Kikwete alitoa maelezo haya wakati anachangia bajeti ya wizara yake ya mwaka
2001/2002
Maelezo ya Kikwete yalieleza kuwa “Serikali imenunua jengo la ubalozi Italia kwa Euro
3,098,741.40 baada ya kufata ushauri wa wizara ya ardhi na Ujenzi hivyo utaratibu wote
ulifuatwa.”
Mgongolwa: Maelezo haya ni sahihi
Mkapa: Ni sahihi
Mgongolwa: Mbona katibu mkuu wako kiongozi bwana Marten Lumbanga ambaye ni
shahidi wa kwanza wa Jamuhuri anadai hakujua manunuzi haya?
Mkapa: Nimeshangaa kusikia anasema hajui. Rais siwezi kujua juu ya kitu na katibu
mkuu kiongozi asijue.
Mkapa akaendelea kueleza kwamba ameshangaa kuona Mahalu akishitakiwa kwa
jambo hilo na hajui nani aliyeagiza upelelezi juu ya jambo hilo hadi kumshitaki.
Mkapa akaeleza hajui kama upelelezi ulianza akiwa madarakani au ameshataafu.
Alishtukia tu Mahalu anapandishwa kizimbani
Baada ya Alex Mgongolwa kumaliza kumuongoza Mkapa, ikafata zamu ya upande wa
mashitaka kum”cross-examine”
Akaingia ulingoni wakili wa serikali Ponsiano Lukosi
Lukosi: Huoni kama dai la muuzaji kutaka kulipwa kwenye akaunti mbili tofauti
ulikuwa ni ukwepaji wa kodi?
Mkapa: Hilo si tatizo langu. Ni tatizo la nchi yake. Mimi nimepata jengo nililotaka...,
Alhamdulilah.
Lukosi : Huu sio wizi wa mshtakiwa?
Mkapa: Nitashangaa sana Mahalu kuwa mwizi, na nitakushangaa wewe. Mahalu ni
msomi mzuri, na mtumishi mwaminifu sana.
Mkapa akataka kusema kitu kisha akasita
Akamwambia Lukosi asimchokoze asije akasema mangine yasiyohitajika.
Majira ya saa 7 na Dk 8 rais Mkapa alikuwa ameshamaliza kutoa ushaidi wake
Ina maada Mkapa alitoa ushaidi kwa zaidi ya muda wa saa moja na Dk 30
akimpambania balozi wake Mahalu.
Mahalu hakukutwa na hatia kwenye kesi kesi hivyo aliachiwa huru.
Wakati anatoa hukumu, Hakimu mkazi Irvin Mgeta alitumia nadharia ya Principal na
Agent
Kuwa Principal (Serikali) ilimpa “Power of attorney” Agent (Balozi) kufanya kila kitu
ubalozini akiiwakilisha Jamuhuri ya Tanzania kisha baadaye analalamikia Power
aliyompa
Mgeta alifananisha hali hiyo ni sawa na mtu aliyeijaza bastola risasi, akaikoki,
akajielekezea na kuifyatua
Kisha mtu huyo alalamile risasi imemuua
Baadaye katika uzinduzi wa kitabu chake, rais Mkapa alieleza kuwa aliamua kumtetea
Mahalu kwa kuwa aliona anaonewa.
Naam!
Rais Kikwete aliingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa October 2005 alipoibuka
kidedea.
Sera yake ya kasi mpya, nguvu mpya na hari mpya, ikimbeba dhidi ya wapinzani wake
kwenye uchaguzi huo.
Miaka miwili tangu ushindi wa Kikwete, tukaanza kushuudia kesi kubwa dhidi ya
viongozi wakubwa wa iliyokuwa serikali ya mtangulizi wake ambaye yeye alimtumikia
kama waziri.
Kesi ya kwanza ilikuwa ni hii ya Mahalu iliyofunguliwa mwaka 2007
Mahalu alikuja kutoa ushaidi uliokuja kuichanganya vibaya kambi ya mashtaka
Takukuru waliokuwa wakitumia kama ushaidi barua ya Mahalu aliyoandikia serikali
Feb 2, 2002 kuijulisha kuwa amefikia hatua ya ununuzi wa jengo, walishtushwa na
nyaraka alizoibua Mahalu mahakamani
Mahalu alikubali kweli ile ni barua aliyoandaa mwenyewe na aliituma kwa mabosi wake
Katibu mkuu na Waziri wa mambo ya nje (Kikwete)
Pia aliwanukuu Katibu Mkuu (Lumbaga) Kiongozi, Waziri wa fedha (Mramba) na
Kamishina wa bajeti wa wizara ya mambo ya nje.
Mahalu akaeleza barua ile waliyonayo TAKUKURU ilikuwa na viambatanisho 11
ambavyo hajui ni kwa nini hawajavitumia kwenye ushaidi
Sasa Mahalu akawa anashambulia kwa ngumi za “below the belt” kuusambaratisha
upande wa mashtaka
Mahalu akatoa mahakamani ripoti ya ....Subscribe hapo chini kuendelea kusoma makala hii na nyingine nyingi click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
AXIS OF EVIL
DISCLAIMER:
Marehemu huwa haongelewi kwa mabaya, Lakini matendo yao
hapa duniani hayatufungi mikono kuyajadili kwa ajili ya
mafundisho ya vizazi vijavyo.

80% ya Madawa ya kulevya yanayopatikana Tanzania, Si kwa
ajili ya watumiaji wa ndani. Naam! Madawa haya si kwa ajili ya
soko la Tanzania ingawa yanapatikana kwa wingi nchini kwetu.

Tanzania ni kama lango tu(Corridor) kwa ajili ya kupitisha
madawa haya mpaka kwenye soko lililokusudiwa (Target
Market)

Ni kwa nini yasitumike ndani wakati walaji wapo hapa hapa?
Jibu ni jepesi sana, Gharama! Yes , Gharama!

Madawa hayahuwa ni very expensive kwa watumiaji wa ndani kuweza
kuyamudu. Ni watanzanzia wachache wenye uwezo wa
kumudu gharama za madawa haya. Ni kwa sababu hii walaji
wengi wa ndani huishia kula makapi (by products) aka
“Ngada” Makapi haya ndio huwa na madhara makubwa kwa
mtumiaji kuliko wale wanaotumia kitu “pure” kabisa.

Ok.Tumejua kuwa Tanzania ni njia tu! Je “Mzigo” hutoka wapi
na kwenda wapi? Here we are! Nifatilie taratiiibu nikielezea
habari hii kwa kunuu Chanzo.

“Mzigo huwa unatoka either “Kwa Pele” au “Kwa Musharaf”
Ndugu Msomaji, Popote litakapotumika neno “Kwa Pele” jua ni
Brazil na “Kwa Musharaf” Jua ni Pakistani.

Hizi nchi huitwa kwa Codes hizo ndani ya Ulimwengu wa wasafirishaji. Kwa
hiyo mzigo unatoka Brazil au Pakistani
“Mzigo ukitoka huko anapewa mbebaji mmoja ambaye
husafirisha kwa kuyameza mpaka Dubai. “Hasafiri bila
mipango kuwa imesukwa tangu anakotoka mpaka Dubai”
“Akifika Dubai Safari yake inaishia pale na analipwa kabisa
Chake pale pale.”

“Anaishia pale kwa Sababu Passport
ikisomeka imegongwa mihuri ya Kwa Pele au Musharaf basi
maafisa Ukaguzi viwanja vya ndege huwa makini sana na
mzigo wowote uliobeba” “Ili kuepusha mzigo kudakwa inabidi
mtu wa kwa pele au Musharaf aishie Dubai”
“Tangu mzigo unapotoka shambani, tayari anakuwa
ameshaandaliwa “punda” mwingine ambaye atameza ule
mzigo pale Dubai na kuuvusha mpaka Msumbiji” “Huyu naye
ataishia Msumbiji tu na kulipwa Chake”

“Kutokea Tanzania, Punda mwingine atavuka mpaka Msumbiji
kwa kukata passport ya masaa 24 tu” “Si rahisi maafisa
usalama kumshtukia mtu huyu ambaye kavuka tu Kuingia
Msumbiji na baada ya Masaa katoka” “Punda huyu ndiye
atakayemeza mzigo wa Msumbiji na kuuingiza Mtwara/Lindi”

So ndugu Msomaji Umeona “Triangle of Custody” ya Mzigo
kuanzia shambani mpaka umefika mikoa ya Kusini. Njia
unavyokuja haiachi traces zozote kwa yule aliyefanikiwa
kuufikisha kwenye point aliyoelekezwa. Huwa kuna Viapo na
binadamu anawezwa kutumika kama “bond” ya kiapo.

Mzigo Ukifika kusini, Sio mwisho wa safari, Mzigo ule
hukutana na wakemia wenye uwezo wa kucheza na Molecular
formula ya fawa zile kuzifanya zisomeke kama raw materials
ya dawa zilizokubalika kwa matumizi ya binadamu. (Refer
HYDROCARBONS) Naam! Wanageuza nyekundu kuwa Njano.

Kuanzia hapa sasa ndio matawi ya Kusambaza mzigo huu
yanapoanzia either kwenda nchi kama Congo, Nigeria, South
Africa mpaka kwa watumiaji wenyewe kabisa Marekani, China
etc.

Leo nashuka na Mkasa wa mabinti wawili walioingia kwenye
biashara hii mwaka 2013. Katika mkasa huu ndipo
ilipoonekana kuwa mapambano dhidi ya biashara hii ni sawa
na kujichimbia kaburi lako Mwenyewe.

Melisa Edward alikuwa ni mfanyakazi katika mgahawa mmoja
maaarufu sana karibu na yule askari “aliyepanga “jab” kama
Mandonga” Naweza kuthibitisha kuwa Mgahawa ule ulikuwa
unamilikiwa na Jamaa flani ambaye alikuwa karibu na mtoto
wa mkuu mmoja wa kisiwa.

Kuishi mjini kwa kujichanganya kuna raha yake. Nilikuwa
napenda sana kupata lunch karibu na mgahawa fulani hivi
mjini kati. Mama mmiliki wa mgahawa ule tukazoeana
tukajenga ukaribu wa kindugu hadi nikawa mshikaji sana wa
mtoto wake mmoja.

Mtoto wake was a so Connected Man.
Siku Moja akanipa Mwaliko Oyaaa!
“Fortu Shika Card hii, Leo jioni njoo kuna lounge ya mshkaji
inafunguliwa Usikose”
Siku hiyo kulikuwa kuna fainali ya UEFA Chelsea Vs Bayern
Munich ilikuwa mtoto hatumwi dukani.

Nilipofika pale
nilishangaa ulinzi wa kutisha uliokuwa pale nje plus magari ya
kifahari yaliokuwa yameegeshwa. Mpaka unaingia ndani
upekuzi sio wa mchezo. Naam!
Kule ndani nikakuta “wenye mji wao” kweli wameenea.
Nikajiangalia mimi kweli wa kupewa mwaliko huu? Lakini si
unajua wabongo wengi ni “Washamba Shapu”?, hivyo
nikaficha mshangao nikavaa uenyeji.

Kwa nini napiga story hii? Fatana nami.
Pale ndani nilijithibitishia kuwa yule jamaa anayefungua
mgahawa lazima ana ukaribu sana hata kumfanya “somebody”
aje pale kushiriki tukio la uzinduzi.
Sasa Miezi kadhaa mbele Kukatokea tukio lililomuhusisha
huyu binti aliyekuwa mhudumu kwenye huu mgahawa. Ilikuwa
hivi

Jioni ya tarehe 4 July 2013 binti huyu alikuwa kazini lakini
akiwa kwenye mazungumzo nyeti na boss wake. Ni kama
walikuwa wanaelekezana “rehearsals” za mwisho mwisho
kwani usiku huo binti alitakiwa kujipanga kwa Safari. Baadaye
akaingia jamaa mwingine anayetumia jina la shujaa maarufu
aliyepotosha wanajeshi wenzie kuita risasi maji. Naye akaingia
kwenye mazungumzo yale. Usiku ule ule dada wa Muhudumu
yule akifanya tambo mitandaoni kwa kupost akiwa na pesa
ndefu. Tayari walishapewa Chao!
Baadae kwa msaada wa Closed Circuit Camera Television
(CCTV) footage iliyopo uwanja wa ndege Dar Es Salaam ya
Muda wa dakika 65 mambo yalikuwa ifuatavyo
Majira ya Saa 10:15 Usiku Yule Mhudumu, Dada yake na yule
mwenye mgahawa wakaonekana waliingia kwenye eneo la
Uwanja wa ndege Dar Es salaam.
Lakini kabla ya ujio wao saa 9:45 anaonekana Polisi kwenye
camera akizunguka zunguka nje ya chumba cha ukaguzi kama
anayesubiria mtu Polisi huyu anafahamika kuwa ni Corporal
Ernest
Camera inamwoshesha pia Mbeba Mizigo akiangalia saa na
kuongea na simu kama anapokea maelekezo fulani. Huyu
mbeba mizigo (porter) wachawi wakamtmbua kuwa ni Zahoro
Mohamedi Selemani.
Mara Paap, Wale mademu na bosi wao wanaonekana
wakisogelea dawati la Ukaguzi. Wakiwa sasa na Mabegi tisa
yanayofanana.
Yule askari (Corporal Ernest) anaanza kusaidia abiria kuweka
mizigo yao kwenye Scanner. Kumbuka hii haikuwa kazi yake!
Pale pale anaonekana afisa mmoja wa Mamlaka ya Viwanja vya
ndege (TAA) ambaye anajulikana kwa jina la Yusuph Daniel
Issa akimtoa mwenzie aitwaye Jackson Manyonyi kwenye
scanner na yeye kujiposition pale.
Anatumia dakika sita kuyapitisha mabegi 9 kwenye Scanner
kuanzia saa 10:16 mpaka 10:22 usiku Anapomaliza kuyapitisha
anatoka kumruhusu afisa wa mwanzo aendelee na kazi.
Kazi yake Mola haina makosa, Lakini kazi ya binadamu ina
makosa. Yakafanyika makosa matatu yaliyowagharimu.
Kwanza afisa yule wa TAA aliyemtoa mwenzake ili apitishe
yale mabegi hakujiandikisha katika kitabu (Screeners
Logbook) kama utaratibu ulivyomtaka. Alipomaliza kuyavusha
mabegi yale akatoka na kwenda kunong’ona jambo na yule
polisi( Ernest) ambaye pale halikuwa eneo lake la kazi na
baada ya hapo akaenda tena kunong’ona na afisa mwenzake
wa TAA (Jacksoni Manyonyi) ambaye sasa alisharudi kwenye
Scanner. Kumbe Wachawi wanaangalia tu.
Pili, Yule afisa wa TAA mvusha mabegi alikuwa akizungumza
na simu muda wote wakati pale simu haziruhusiwi lakini
incharge wake aitwaye Juliana Thadei alionekana kwenye
Camera akiwa katulia bila kuzua hayo yasitendeke. Sio yeye tu,
hata Security officer mwingine wa TAA aitwaye Mohamed
Kalungwa naye anaona mchezo wote ukiendelea lakini
akauchuna tu.
Tatu, Yule Boss wa wale mademu alikuwa ameingia eneo la
Ukaguzi (Checking Inn) bila ya kuwa amekata ticketi hivyo
hakutakiwa kabisa kuwa eneo lile.
Tuendelee, Baada ya mizigo ile kupitishwa, Yule boss na wale
mabinti wakasogea na mizigo yao mpaka kwenye Kaunta ya
shirika la ndege la Afrika Kusini.
Mabegi matatu kati ya yale tisa yalikuwa na uzito
unaoruhusiwa kwa abiria kupanda nao ndani ya ndege (20
Kgs) Sasa hapa kumbuka abiria wenye ticketi walikuwa wawili
tu, hivyo begi moja halikupaswa kupitishwa lakini lilipita. Si
unajua tayari njia ilishasafishwa?
Mabegi sita yaliyobaki uzito wake ulikuwa ni zaidi ya Kilo 20
hivyo hayo abiria hakuwa anaruhusiwa kupanda nayo bali
yangewekwa kwenye chumba cha mizigo ndani ya ndege.
Wakati ule kila kilo inayozidi ilikuwa inatozwa USD 5 na kwa
mujibu wa risiti ambayo wachawi waliidaka ni kuwa mabegi
yale yalipaswa kulipia USD 600 yaani kwa wastani kila begi
lilizidi kilo 12.
Sijui kama hapa unaelewa Mzigo unaoruhusiwa bila tozo ni kilo
20, Kilo yoyote inayozidi inatozwa dola 5 kwa hiyo kama kila
begi lilipaswa kulipia dola 100 ina maana lilikuwa na uzito wa
ziada wa kilo 20. Ukijumlisha na uzito unaoruhusiwa ina
maana kila begi lilikuwa na jumla ya kilo 40. Kwa mabegi 6 ni
jumla ya Kilo 240
Hizi hesabu sizipigi ili kukuchosha. La Hasha! Nafanya hivi
makusudi ili kadiri unavyozidi kusoma upate uchungu kwa
kuona ni jinsi gani vijana ambao ni nguvu kazi
wanavyoteketezwa kwa hili janga la madawa ya kulevya.
Sasa bwana huwezi kuamini! Mabegi haya hayakulipiwa dola
600 za mzigo uliozidi, bali yalilipiwa dola 94 pekee. Jamaa
hawataki kupoteza bali kupata tu!
Sasa kiutaratibu Mzigo ambao unapaswa kupelekwa kwenye
chumba cha mizigo ndani ya ndege huwa inapitishwa kwenye
ukaguzi mwingine bila abiria kujua. Ukaguzi huu huushisha
mbwa. Kama nilivyosema, Kwa kuwa alfajiri hii njia
ilishasafishwa, Mbwa hawa wa kunusa walicheleweshwa
makusudi kupelekwa kwenye ukaguzi mpaka kwanza mizigo ile
Ipande ndege. Wachawi wanatizama tu!
Yule kibosile baada ya kuona mambo yote yameenda vizuri
akabadili wazo! Badala ya kuwa msindikizaji naye akaona ni
bora akwee nao pipa. Akakata ticketi pale pale fasta. Yani kama
yupo stand ya Magufuri yaani. Yaani jamaa aliweza kuingia
kwenye Ukumbi wa Departures (lounge) bila hata ya kuwa na
Boarding pass Kama alivyoweza kucheck inn bila kuwa na
ticket.
Utamweleza nini? Unamjua yeye nani? Yote haya yaliwezekana.
Lakini hili nalo lilikuwa kosa lake kubwa !
Wachawi wakanukuu namba ya hati yake ya Kusafiria kuwa ni
AB426496 Naam! Wakapata jina lake kuwa anaitwa.. click here to unlock the post

Katika ulimwengu wa Ujasusi, Mole ni mtu ambaye amekuwa spotted kuwa
anafaa kwa kazi ya ujasusi, akapewa mafundisho yote ya kijasusi (Techno craft)
lakini bado hajapewa access ya taarifa za siri za kijajusi.
Si vibaya ukimuita tena mtu huyu kama Sleeper Agent, Penetration officer au
Deep cover agent
Watu hawa huwekwa kwenye taasisi za serikali au balozi za nchi inayotakiwa
kupelelezwa.
Mole anayepelekwa kuishi nje ya nchi huitwa “Resident designate”
Leo nawapa mikasa miwili
Nina uhakika kila mtu amesikia mkasa wa hivi karibuni kuwa askari wa jeshi la
anga Marekani, kijana mdogo bwana Jack Teixeira alivyoweza kuvujisha siri za
idara ya ulinzi (Pentagon) kuhusu mikakati ya Marekani kwenye vita vya Russia
na Ukraine.
Si hivyo tu!Kijana huyu ambaye ni rubani daraja la kwanza alivujisha pia siri za
kijasusi za marekani dhini ya China,North Korea, Iran na United Arab Emirates.
Siri hizi zilianza kupatikana baada ya kutafsiriwa kwa lugha ya kirusi
Hii ikimaanisha Urusi ilishanyaka taarifa hizo
Siri hizo pia zilihusu mazungumzo ya vikao baina ya rais Joe Bidens na “Joint
Chiefs of Staffs”
Wakati unashangaa juu ya hili, yumkini bado unakumbuka kuwa miaka 10
iliyopita, Mwaka 2013 Mkandarasi wa Kompyuta ndani ya CIA na NSA bwana
Edward Snowden aliitikisa dunia.
Ni kwamba alivujisha siri nyeti kabisa za idara hizo na kukimbilia Urusi baada ya
Marekani kumfutia passport yake.
Rais Putin wa Urusi akampatia uraia wa Urusi anakoishi mpaka hivi sasa.
Visa hivi ni vidogo sana katika ulimwengu wa “Espionage and
Counterintelligence”
Sunday 18th Feb 2001
Foxtone Park, Vienna, Virginia
Washington DC.
Naam!
Ni Majira ya baridi mjini hapa yanayoelekea mwishoni,
Anaonekana Agent mwandamizi wa FBI akishuka kwenye gari yake katika
maegesho ya magari jirani na mbuga ya Foxtone (Mile moja toka nyumbani
kwake)
Afisa huyu alikuwa anatumia jina la uficho la “Ramon” akiwa anafanya kazi
zake kama “Mole” idara ya ujasusi ya Urusi KGB
I repeat!
Kama hujanielewa,ni kwamba afisa huyu wa FBI alikuwa anafanya kazi kama
“Mole” wa KGB
Hadi leo hii wakati anaenda kuegesha gari katika maegesho haya, hakujua
kama kwa miaka 11 iliyopita alikuwa under surveillance ya FBI na CIA baada ya
kwanza, kuuzwa na shemeji yake ambaye naye alikuwa ni afisa wa FBI, na pili
baada ya kunaswa sauti zake kwenye tape recorder
Kuna wakati fulani machale yalimcheza afisa huyu baada ya kuwa anasikia
kelele zisizo za kawaida kila akiwasha radio ya gari yake, lakini akapuuzia.
Ni kwamba alishakuwa amewekewa “bugs” zilizokuwa zinarekodi mazungumzo
yake kwenye gari na kwenye simu zake bila yeye kujua.
Unaweza ukajiuliza ni kwa nini ilifikia hatua hii?
Ni kwamba CIA na FBI walikuwa kwenye mashaka mazito kuwa kuna mtu ndani
yao anawauza kutokana na kuvuja kwa taarifa zao fulani.
Mwaka 1977 ubalozi wa Urusi (Soviety Embassy) ulihamia katika mji wa
Washington DC,
Baada ya kuhamia hapa, FBI wakawa na mashaka kuwa ubalozi huu unaweza
ukawa unadukua taarifa za white House na jengo la Bunge.
Ikaandaliwa mission ya kufatilia nyendo za ubalozi huu
Ikaamuliwa uchimbwe mfereji chini kwa chini kwenda kwenye ubalozi ule na
FBI wakanunua nyumba mkabala na ubalozi ule ili iwe kama ofisi ya kijasusi
dhidi ya ubalozi ule ikipokea signals kutoka mferejini
Taarifa ya kujengwa mferejei huu ilivuja kwa maafisa wa KGB baada ya kuuzwa
na “Code Name” Ramos
Huu ulikuwa ni mwanzo tu wa security breaches
Ni kwamba Tarehe 1 October mwaka 1985 Shirika la Ujasusi Urusi (KGB)
lilipokea barua toka ...Subscribe hapo chini kuendelea kusoma makal hii click here to unlock the post