A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
MAUAJI BILIONEA MSUYA
Usiku wa manane kuamkia 26 july 2013,ndugu WILLY MUSHI ONESMO
anapigwa risasi na kufariki akiwa kazini
WILLY MUSHI ONESMO alikuwa ni mfanyakazi wa mgodi wa madini
TANZANITE ONE huko MIRERANI Simanjiro.
Kulikuwa kuna tabia ya wachimbaji wadogo wanaouzunguka mgodi
huo,kuingia chini kwa chini na kwenda kuiba madini mgodi wa Tanzanite
Wenyewe wanaita "MTOBOZANO" au "KUTEKA NJIA"
Siku ya tukio bwana WILLY ONESMO MUSHI akiwa na wafanyakazi
wenzake KENEDY na LEONARD walishuka shimoni kufanya patroal ndipo
akakutana na wateka njia ambapo alifyatuliwa risasi kifuani na kufikwa na
mauti.(inasemekana aliombwa “suruhu wayamalize” akakataa).
Baada ya kifo cha ONESMO wafanyakazi wa TANZANITE ONE wakafanya
mgomo hatua zichukuliwe kwa waliohusika.
TETESI zikimtaja mmiliki wa mgodi wa jirani bwana JOSEPH DISMAS
MWAKIPESILE aka CHUSA kuhusika na sakata hilo.
Kufuatia mgomo huo na madai hayo,Serikali,iliifunga migodi minne
inayozunguka mgodi wa Tanzanite one
Hatua hii iliibua tena maandamano ya wachimbaji wadogo mkoani
Manyara chini ya chama chao cha MAREMA.
Kwa ufupi Kifo cha WILLIAM ONESMO kilizua kizaazaa Mirelani.
Tarehe 29 July 2013,Onesmo alizikwa kijijini kwao Uswaa,Machame,
wilayani Hai
Kufuatia makelele mengi yaliyotaka haki itendeke,aliyetuhumiwa kwa
mauaji hayo JOSEPH DISMAS MWAKIPESILE aka CHUSA akakamatwa.
Chusa akawekwa mahabusu ya Babati na kipindi fulani akapelekwa
Hospitali ya Mrali akiwa chini ya ulinzi.
Haikupita hata wiki tangu CHUSA akamatwe,huko mtaani Arusha
“kikaumana” tena..
Ikiwa ni mchana wa jua kali
Yes!
In a broad daylight, mfanyabiashara mmoja wa madini, akapokonywa uhai.
Si mwingine, bali ni Elasto Msuya
Msuya anasemwa alirithishwa mgodi na baba yake (Block B) ambao
haukumtoa kivilee,
Kupitia mgodi wake wa Karo akapiga “Mawe ya lemakoo” (watu wa chuga
tu ndo watanielewa)
Msuya akafungua SG PREMIUM RESORT HOTEL.
Baadaye “mawe ya bomu” ndio yakampa heshima Arusha nzima.
Inasemekana Erasto Msuya kuwa karibu sana na mfanyakazi wa
TANZANITE ONE aliyeuwawa(WILLIAM ONESMO MUSHI) ambaye
alikuwa anamuuzia madini kutoka mgodi anaofanyia kazi.
Madini haya ya deal ndio yaliitwa “Mawe ya bomu”.
Kuuwawa kwa ONESMO lilikuwa pigo kwa Msuya.
Ilinong’onwa kuwa, washindani wa Msuya hawakupenda kitendo cha
Onesmo kuwa anamuuzia Msuya peke yake mawe ya bomu.
Kibaya zaidi,wao “Wakiteka njia” wakikutana na ONESMO kwenye
“MTOBOZANO” anakuwa hataki kusomeshwa.
Ina maana Onesmo "alipigwa bomba" na aliowakamata wakipenya chini
kwa chini kutoka kwenye mashimo yao na kuingia kitalu cha Tanzanite
One.
waliokuwa wananufaika na Onesmo wakamchomesha Chusa kuwa
anahusika
Chusa akiwa bado mahabusu Babati, ndipo mshirika wa Onesmo
anauwawa.
Naam!
Tukio hili lilitukia siku ya jumapili. click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

MAUAJI MWANZA

Usiku wa kuamkia jumapili tarehe 29 May 2022, Jamii ya watanzania kwa ujumla hasa wakazi wa Mwanza walishtushwa na habari ya mauaji yaliyofanyika maeneo ya Mbogamboga Buswelu wilaya ya Ilemela jijini humo.

Habari ile iliyosambaa kama moto nyikani ilidai kuwa kijana mmoja aitwaye Said amemuua mkewe kwa kumpiga risasi saba.

Kama ilivyo kawaida ya jukwaa hili ambalo hujihusisha na habari za uchunguzi, ilibidi macho na masikio yetu kuyaelekeza jijini Mwanza ili kuja na habari kamili nyuma ya tukio hilo.

Nilifanikiwa kuchimba kidogo wasifu wa Marehemu aliyedaiwa kuuwawa na mmewe na pia wasifu wa marehemu mmewe ambaye alidaiwa kujiua muda mfupi baada ya tukio hilo.

Mwanamke aliyepigwa risasi aitwaye Swalha Salumu (28) alikuwa ni binti maarufu sana jijini Mwanza aliyezaliwa na kukulia maeneo ya Kirumba.

Wazazi wake ambao ni SALUM PUVA(baba) na TIBAH MOHAMED(mama)walihamia Mwanza wakitokea wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma hivyo Salha alikuwa ni Mrangi.

Alizaliwa katika familia ya kawaida sana mama yake TIBAH MOHAMED akijihusisha na biashara ya genge kwenye soko la Kirumba.

Binti huyu anasemwa mwanzoni alikuwa akifanya kazi ya uhudumu kwenye Bar maarufu ya Villa jijini humo hadi alipopata mwanaume aitwaye Shiwa aliyemuoa na kumbadilishia maisha.

Shiwa alikuwa anajihusisha na biashara ya madini mkoani Geita na anatajwa kuwa aliweza kumjengea nyumba na kumnunulia gari.

Baadaye Sawhla alifungua Saluni ya urembo mtaa wa Uhuru karibu na kituo cha daladala cha Dampo.

Saluni hii ilijihusisha na upambaji wa maharusi.

Haitajwi nini ilikuwa sababu ya Sawla kuachana na Shiwa hadi kuja kuolewa na Said Oswayo lakini katika moja ya mahojiano Marehemu Swahla alinukuliwa akisema kuwa bwana wake alimfungulia duka la nguo akawa anamnyanyasa mara amzuie kwenda dukani, mara amnyang’anye funguo za duka na wakati mwingine akimpekekea michepuko yake pale dukani kuinunulia nguo.

Said Oswayo alikuwa ni kijana mjasiliamali aliyejihusisha na biashara ya uvuvi. Alikuwa akimiliki mitumbwi kadhaa yenye nembo ya OSWAYO na alikuwa na makambi kadhaa ya uvuvi.

Said Oswayo

Kutokana na hili Said alikuwa ni mtu wa kutoka mara nyingi nyumbani kwake na kwenda kwenye shughuri zake za uvuvi alizokuwa akifanyia kisiwa cha Ukerewe.

Wakati anafunga ndoa Sawhla iliyodumu kwa miezi mitano, tayari alikuwa ameshafunga ndoa nyingine aliyofanikiwa kupata mtoto mmoja.

Kwa mujibu wa Mama mzazi wa Said aitwaye TATU OSWAYO ni kwamba alikuwa bado anamtambua mke wa mwanzo kwa kuwa hakuwa amepewa talaka na Said.

Tangu mwanzo mwa mahusino yake Sawhla, Ilishaonekana Saidi alikuwa na dukuduku fulani juu ya Sawhla.

Naomba ninukuu chanzo

“Kuna kipindi mwaka jana aliwahi kumwambia mshikaji wangu kuwa washikaji wanamwambia kwa huyu dem ameingia mkenge.”

“Mshikaji akamshauri kuwa kwenye swala la mahusiano yeye ndio anatakiwa kupima anayoambiwa na kujiridhisha kuona kama hamfai.”

Akaedelea

“Ila chakushangaza haikuchukuwa muda wakafunga ndoa”

Tuweke kwanza hapa pause tuchakate maneno haya!

1. Washkaji wananiambia kwa huyu demu nimeingia mkenge(Saidi to a friend)

2. Wewe ndio unatakiwa upime na ujiridhishe juu ya unayoambiwa( A friend to Saidi)

Hapa inaonyesha tangu mwanzo wa mahusiano haya kulishakuwa na nyufa ndani ya moyo wa Saidi,

Saidi alikuwa akipelekewa maneno mengi juu ya mkewe na rafiki yake akamshauri afanye uchunguzi ajiridhishe.

Lakini, click here to unlock the post

Dakika chache baada ya askari kufika kwenye lindo la CRDB Mbande, watu sita waliokuwa wameficha silaha ndani ya hijab wakaanzisha mvua ya risasi. Askari mmoja alipojaribu kujibu mashambulizi, SMG yake ikagoma kufanya kazi—na bunduki nyingine iliyookotwa nayo ikamisfire. Baada ya dakika kumi, askari wanne walikuwa wameuawa, silaha mbili zimeporwa na sare za polisi zimeibiwa; lakini washambuliaji hawakuingia hata ndani ya benki. Kama hawakufuata fedha, lengo lao halisi lilikuwa nini? Na Mbwana, mfanyakazi wa duka la jumla mwenye ratiba zisizotabirika, aliingiaje katika fumbo hili? Soma simulizi kamili ya MAUAJI POLISI MBANDE kwa kusubscribe hapo chini click here to unlock the post

In Every Crime,there is always a trail of evidence that is left behind.

Fatilia mkasa huu wa mauaji ya kutisha yaliyotokana na kifo cha mtu mmoja tu.

"A CHAIN OF MURDER CRIMES"

UZI
#simulizizabuyobe
Tweet image 1
2 / 4
Usiku wa manane kuamkia 26 july 2013,ndugu WILLY MUSHI ONESMO anapigwa risasi na kufariki akiwa kazini
Tweet image 1
3 / 4
WILLY MUSHI ONESMO alikuwa ni mfanyakazi wa mgodi wa madini TANZANITE ONE huko MIRERANI Simanjiro. Kulikuwa kuna tabia ya wachimbaji wadogo wanaouzunguka mgodi huo,kuingia chini kwa chini na kwenda kuiba madini mgodi wa Tanzanite(Wenyewe wanaita "MTOBOZANO" au "KUTEKA NJIA")
Tweet image 1
4 / 4
Siku ya tukio bwana WILLY ONESMO MUSHI akiwa na wafanyakazi wenzake KENEDY na LEONARD walishuka shimoni kufanya patroal ndipo akakutana na wateka njia ambapo alifyatuliwa risasi kifuani na kufikwa na mauti.(inasemekana aliombwa "suruhu wayamalize" akakataa).Soma simulizi kamili ya **DEATH AT FUNERAL** kwa kubofya hapo chin click here to unlock the post

Akiwa na miaka 29 pekee, alialikwa Gaborone kwenye kongamano la Forbes Under 30 Africa—ishara kwamba ndoto zake zilikuwa zimeanza kutimia. Lakini aliporejea Afrika Kusini, maafisa wa uhamiaji walimzuia na kumrudisha Kongo, nchi aliyokuwa ameikimbia tangu akiwa na miaka tisa. Alipotua Kinshasa usiku, alituma ujumbe kuwa amewasili… kisha akatoweka. Saa chache baadaye, familia yake ikapokea video ya kutisha iliyogeuza safari yake kuwa fumbo la kifo. Nini hasa kilimtokea baada ya kutoka uwanja wa ndege? Soma simulizi kamili ya **DEATH AT FUNERAL** kwa kusubscribe hapo chini click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE A SHADOW OF DEATH
Natumaini Kila mmoja wetu humu ameshawahi kusikia
mkasa ulioanza kama tukio la Kupotea kwa mtu.
Tarehe 15 May 2019 Bwana Khamis Luwogo alifika
katika kituo cha Polisi Kigamboni na kutoa taarifa za
kupotelewa na mkewe NAOMI OREST MARIJANI
maarufu kama SANDRA
Baadae mume huyu aliwajulisha ndugu wa mkewe (Kith
and kins) juu ya taarifa hizi ambao nao walienda kutoa
taarifa katika kituo cha polisi Chang,ombe.
Tangazo la kupotea kwa naomi zikasambazwa kwenye
mitandao ya kijamii.
Watu walilipokea taarifa zile kwa mitazamo tofauti.
Wengine wakibeza na kusema haiwezekani mtu mzima kama Naomi tena akiwa “pisi kali” anaweza kupotea kirahisi.
Wakatoa maoni kuna sehemu atakuwa kafichwa na kidume na atapatikana tu baada ya muda.
Hawakujua Abadani!
Baadae zikaibuka taarifa zikimuhusisha mume huyu huyu kuhusika na kumuua mkewe, kumchoma moto kwa magunia mawili ya mkaa, Kuchukua majivu yake na kwenda kuyafukia kwenye shamba lake Mlogoro mkoani pwani na kisha kupanda mgomba juu yake.
Leo sitaki kukiingia kisa hiki kwa undani. Bado Tuko Kigamboni.
Nalazimika kurudi nyuma miaka mitatu kabla ya tukio nililolielezea juu.
Tarehe 25 May 2016
Siku hii anauwawa tena Msichana mrembo nyumbani kwake maeneo ya Kibada, Kigamboni.

Si vibaya tukipata wasifu wake kwa ufupi mrembo huyu aliyesifika kuwa na akili nyingi sana za darasani.
Alizaliwa Machame Kilimanjaro, Akasoma shule ya Msingi Msaleni
O level Akasemea St. Dorcas Moshi na akaibuka na Divison one ya Point 8
On her High school at Junior Seminary in Morogoro, she kept on her habit of giving capital punishments to NECTA exams as she emerged a victor with Division 1 with 4 Points on scoreboard.
Then she Joined the University of Dar Es salaam. Sorry for my alternating language.
Pale chuoni akasomea Uchumi na kuibuka best student katika darasa lao, Jambo lililoivutia wizara ya fedha kumpa scholarship ya kusomea Uzamili palepale mlimani.
Alipohitimu akaajiriwa directly na wizara ile kama mchumi pale BOT

Akaolewa, Akazaa mtoto mmoja na baada ya mwaka ndoa yake ikafa kifo cha asili.
Tangu kuachana na mumewe hakuoneka kuwa na mahusiano mengine na kama yalikuwepo aliyafanya kwa usiri mkubwa.
Ndipo siku moja akiwa ametoka kwenda kazini, ukafika ugeni kwa siri nyumbani kwake.
Ni kwamba tarehe 18 May 2016, Ilionekana gari moja ya kifahari (Range Rover)rangi ya blue Ikiwa imepaki jirani na nyumba yake huku waliokuwemo ndani yake wakiwa hawajashuka ndani.
Mfanyakazi wake wa ndani alipotoka ili kwenda dukani ndio watu wale wakashusha vioo vya gari na kumuita.
Mfanyakazi huyu aliyeitwa Getrude Mafuru ,anamfahamu mmoja wa aliyemuita ambapo anakabidhiwa simu ya mkononi asiitumie kuwasiliana na mtu yeyote isipokuwa huyo aliyempa simu.

Kisha watu wale wanaondoka na kurudi tarehe 23 May 2016 ikiwa ni siku mbili kabla ya utekelezaji wa mipango yao.
Siku hiyo msichana yule anakabidhiwa kiasi fulani cha pesa.
Baadae akapigiwa simu kuwa ahakikishe asiwepo pale nyumbani tarehe 25 May 2016
Kwamba akishaondoka atupe simu ile na asiitumie tena wala SIM Card yake.
Muda wote huu Huu dada wa watu alikuwa akiendelea kwenda kazini na kumuachia nyumba Mfanyakazi wake bila kujua kuwa kuna ramani ya vita iliyoanza kuchorwa arusha na kuletwa site nyumbani kwake Kigamboni.
Huku Architects wa ramani ile wakiwa ni watu wake wa karibu.
Mdada yule akaanza kuwa anashangaa anapigiwa simu mara tofauti.
Akipokea wanaoongea ni watu wenye sauti ya Kiume. Walikuwa wanauliza swali moja tu, UKO WAPI? Akiuliza mpigaji ni nani?
Simu zinakatwa!
Lakini huyu mrembo ni nani?

Mrembo huyu si mwingine bali ni Aneth Msuya dada wa Marehemu Erasto Msuya aka Bilionea Msuya ambaye aliuwawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 22 mwezi August mwaka 2013 maeneo ya KIA kati ya Moshi na Arusha.
Baada ya kifo cha kaka yake kulitokea mgogoro mkubwa wa kugombea mali za marehemu kati ya familia ya Msuya na mjane wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Miriam Mrita.
Actually,marehemu aliacha wosia kuwa akifariki basi 40% ya mali zake wapewe wazazi na dada zake na 60% wapewe mke na watoto.
Familia ya Msuya limteua mjane wa Msuya kusimamia mirathi na walikubaliana wafungue mirathi mahakamani mke awe msimamizi lakini atumie wakili atakayeteuliwa na familia ya Msuya.
Lakini badaye zikaanza kusambaa taarifa kuwa usiku mmoja mjane wa marehemu amehamisha nyaraka mbalimbali na kupeleka kusikojulikana baada ya kuivunja ofisi ya marehemu mmewe.
Kuwa alihamisha pia madini yote aliyokuwa nayo pale ofisini na kawa ameanza kuhamishia umiliki wa documents mbalimbali kwa jina lake.
Kuwa alishaanza kuuza baadhi ya mali mojawapo ikiwa ni kiwanja cha marehemu huko Njiro bila ridhaa ya wanandugu.

Familia ya marehemu Msuya wakajipa jukumu la kufunga nyumba sita za marehemu.
Mgogoro baina ya mjane wa marehemu kwa upande mmoja na wakwe na dada wa marehemu sasa haukuwa siri tena hadi kufikia hatua ya Mama wa marehemu Msuya kutomtaka mkwewe kufika kwake hata siku atakayokufa.
Mgogoro huu kuna wakati uliingiliwa na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Arumeru Jery Muro.
Wakati watu wakiamini swala lile limemalizwa, huku nyuma ndugu wa Msuya wakawa wanapata misukosuko.
Dada wa Msuya akitwaye Antuja Msuya alinusurika jaribio la kuuwawa kwa kumwagiwa kimiminika kidhaniwacho kuwa sumu akiwa amelala na mtotopekee wa Aneth.
Kama haitoshi dada wa Msuya aitwaye Ester Msuya, akiwa na mmewe maeneo ya Hongera Bar Sinza, walinusurika kuuwawa baada ya mtu asiyejulikana kuwamiminia risasi vifuani na mgogoni na kutokomea kusikojulikana.
Sasa safari hii ndio Ikawa zamu ya Aneth.
Ilikuwa imeshafika tarehe 25 May 2013 siku ya mauji kwa mujibu wa kalenda ya wauaji wale.
Aneth aliamka kama kawaida na kwenda kazini kwake.

Binti wa kazi Getrude akamuandaa mtoto wa Aneth kwa ajili ya kwenda shule ambapo gari la shule lilimpitia mtoto akaenda shule.
Huku nyuma Getrude akakusanya kila chake, akafunga nyumba na kuifadhi ufunguo wa kuingilia ndani chini ya zuria lililokuwepo kwenye mlango ule.
Getrude akatoka nje ya geti ambapo alifunga geti kwa funguo na kwenda kukabidhi funguo ile kwa jirani.
Kisha akampigia simu Aneth kumweleza amepata dharula hivyo anasafiri akamwelekeza alipoacha funguo na alipoficha ufunguo wa ndani.
Getrude akaitupa simu yake baharini wakati anavuka na kivuko kutoka Kigamboni kwenda kwa boyfriend wake aishie maeneo ya Chanika.
Upande mwingine Simu ya Getrude kwenda kwa Aneth ilimaanisha kuwa Aneth awahi kurudi nyumbani kumpokea mtoto atakapotoka shule kwani hakuna mtu wa kumpokea.
Hili lilikuwa ni tukio lililokuwa limepigiwa hesabu tayari na wanampango ule ambao tayari walishafanikiwa kudurufu funguo za nyumba ya Aneth baada ya kupewa na Getrude.

So Aneth akanasa kwenye ule mtego, akawahi kurudi nyumbani.
Inaonekana muuaji wake alishafika muda mrefu katika nyumba yake na kwenda kujificha ndani ya chumba cha Aneth.Soma simulizi kamili kwa kusubscribe hapo chini click here to unlock the post

MAUAJI YA KAGANZO: Asubuhi ya Jumapili, tarehe 3 Julai 2022, Olida alikwenda kumuamsha dada yake Tilifela kwa ajili ya sala kama ilivyokuwa kawaida yao—lakini hakuitikiwa. Alipousukuma mlango na kuingia ndani, alikuta tukio lililokuja kuitikisa Kigoma na Tanzania nzima: watu sita wa familia moja walikuwa wameuawa, huku mtoto wa miaka mitatu akipambania maisha na mwingine wa miezi sita akiwa hai katikati ya maafa. Siku mbili baadaye, idadi ya waliopoteza maisha ilifikia saba. Nani alifanya mauaji haya ya kutisha, na nini kilikuwa chanzo chake? Soma simulizi kamili kwa kusubscribe hapo chini click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
ROOM No. 348
Jioni ya jumatano, tarehe 15 September 2010 ilimkuta mfanyabiashara wa mafuta na gesi
ndugu Gregory Joseph Fleniken akiwa amejipumzisha katika chumba namba 348 cha
hoteli ya MCM Elegante Hotel kitongoji cha Beamont, Texas.
Alikuwa kajilaza kitandani akivuta sigara huku akiangalia filamu ya Iron Man 2
Jioni ilionekana nzuri sana kwake siku hiyo.
Mfanyabiashara huyu alijiwekea utamaduni wa kuianza week yake ya kazi kwa kuendesha
gari kila jumatatu asubuhi kutoka nyumbani kwake Lafayette Illinois mpaka Beamont,
Texas ilipo kampuni ya OGM Land Company
Kampuni hii aliimiliki kwa ubia na kaka yake aitwaye Michael
Bwana Gregory angekaa kitongoji cha Beamont mpaka Weekend ndio angerudi nyumbani
kwake.
Alijijengea pia utamaduni wa kuwasiliana na mkewe kila asubuhi kwa ziku zote ambazo
alikuwa mbali Texas kikazi.
Kwa hiyo Jumatano hii mfanyabiashara huyu alikuwa ametoka kazini na sasa ndio
amejipumzisha chumbani.
Mle chumbani majira ya saa 1 jioni alikuwa ametoka kusoma E-mail ya mkewe ambayo
ilihusu ripoti ya maswala ya kodi kwenye kampuni yao.
Alipomaliza naye akamjibu mkewe “You are doing good baby”
Baada ya hapo akawa anatizama filamu ya “Iron Man 2”
Hakuimaliza,
Kesho yake asubuhi, mfanyabiashara huyu hakuwa amempigia simu mke wake kama ilivyo
kawaida yake
Mke huyu akaamua kuwapigia wafanyakazi katika kampuni ya mmewe ili wamsaidie
azungumze naye.
Hili halikufanikiwa kwa kuwa mmewe hakuwa amefika kazini.
Hali hii ikawalazimu wafanyakazi hawa wawashe gari na kwenda kwenye hoteli aliyokuwa
akifikia.
Kule wakakuta na gruesome and electrifying news.
Ni kwamba waligonga mlango wa chumba chake bila mtu yeyote ndani ya chumba kile
kuitikia.
Ikabidi wafanyakazi hawa wamtafute Manager wa Hoteli ambaye aliwathibitishia kuwa bosi
wao hajatoka chumbani tangu alipoingia jioni ya siku iliyopita.
Wakamtaka Manager yule afungue chumba kwa ufunguo wa ziada
Hilo likafanyika!
Baada ya kuingia wote wakashituka walipomkuta mfanyabiashara yule amelala sakafuni bila
uhai.
Chumbani kulionekana hakukuwa na purukushani zozote kwani kila kitu kilikuwa kwenye
mpangilio mzuri.
Simu yake ya Blackberry,ashtray, packet ya sigara, rimoti ya Tv, chocolate na kiberiti vyote
vilipangwa vizuri
Iliaminika kuwa mfanyabiashara yule alipata mshtuko fulani wa maumivu, hali hiyo
ikamnyanyua kutaka kuelekea mlangoni lakini akashindwa na kuanguka chini
Swali likawa nini kilimuumiza?
Je alikuwa ni mhanga wa tukio la uvamizi na uporaji?
Lakini hakukuwa na dalili zozote za vurumai kwenye mwili wake
Hata damu hazikuonekana kwenye eneo la tukio.
Wallet yake ilikutwa na $ 1000
Hakukuwa na alama yoyote ya chumba kuvunjwa na mvamizi
Hata waliposachi mizigo ya marehemu hawakukuta dawa zozote labda waseme amejiua.
Polisi wakaishia kuhitimisha kwa kuwa marehemu alikuwa anavuta sana sigara kifo chake
kilikuwa ni cha kawaida na sio kilisababishwa na mtu yeyote.
Baada ya polisi kuwahoji wafanyakazi wa hoteli na baadhi ya wateja pale hotelini,
hawakupata lolote.
Hivyo wakaruhusu mwili ule uchukuliwe na madaktari ili waandae taarifa za chanzo cha kifo
(Autopsy)...SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MAKALA KAMILI click here to unlock the post

SAFARI YA KIRIKUU ILIYOGEUKA KUWA MTEGO

Saa 12 jioni, watu wawili walifika kwenye kijiwe cha Mshamu wakitaka kukodi kirikuu chake ili awabebee mbao hadi Mbagara Kongowe. Bei ikapangwa, mzigo ukapakiwa na safari ikaanza bila tatizo—mpaka walipoingia kwenye pori lenye giza na Mshamu akakataa kuendelea. Ndani ya sekunde chache, pikipiki ikaziba njia, Mshamu na rafiki yake wakashambuliwa, wakafungwa kamba na kutupwa porini huku mmoja wa watekaji akipendekeza wauawe. Kwa bahati, Mshamu alijifungua kamba kwa meno na kuanza kufuatilia gari lake. Walipolipata, yowe la “mwizi” lilianzisha msako uliogeuka kuwa vurugu kubwa. Lakini wakati kila mtu akiamini tukio limekwisha, kijana mwingine akakimbia kuelekea Chamazi—na muda huo huo, simu ikapigwa kutoka kwenye nyumba moja: “Nyumbani kimeumana!”Kijana huyo alikuwa nani, na nini kilikuwa kinaendelea ndani ya nyumba hiyo?Subscribe hapo chini kusoma makala kamili.. click here to unlock the post