UMAFIA KIGOMA

In the entire animal kingdom, a human is a very complex animal.

Of all the animals in the kingdom, instead of being equipped with the capabilities of distinguishing good deeds from evil ones, a human can perform very unimaginable mayhem on his fellow without any sense of amnesty.

For swahili audience, Binadamu ni kiumbe kisichotabilika! Ingawa kati ya wanyama wote, binadamu amepewa uwezo wa kutambua mema na mabaya, mnyama huyu anaweza kuishangaza dunia kwa kuyenda kitendo cha kinyama kisichotarajiwa dhidi ya binadamu mwenzake.

Sunday 3rd July, 2022 KAGANZO VILLAGE KAKONKEMWE HAMLET MWANDIGA WARD KIGOMA Wanandoa wawili wanaamka asubuhi hii kwa ajili ya sala ya asubuhi. Wanandoa hawa ni Olida Sauli Mkunze na mumewe Ezekiel Cheche.

Ilikuwa ni kawaida kwa wanandoa hawa kuwa, kabla ya kuanza kwa sala, Olida alikuwa akienda kumuamsha dada yake aitwaye Tilifela Toyi aliyekuwa akiishi nyumba ya jirani tu na kwao, ili wajumuike naye kwenye sala.

Huyu Tilifela, alikuwa akiishi na mtoto wake wa kiume aitwaye January. In a nutshell, January ni kijana shababi mtu mzima ambaye alikuwa ameshaoa hivyo aliishi na mkewe kwenye nyumba ya mama yake.

So, asubuhi hii kama kawaida, Odila akawa ameenda kwenye nyumba ya dada yake ili amuamshe kwa ajili ya sala ya asubuhi.

She only ended into disappointment! Olida alipofika nje ya nyumba akapaza sauti kumuita dada yake.

Hakuitikiwa!

Odila akasogelea mpaka kwenye dirisha la chumba alichokuwa analala dada yake. Akaita tena sana! She only met a dead silence.

Hakuitikiwa tena! Hii haikuwa kawaida! Siku zote Olida alikuwa akimkuta dada yake yuko macho hivyo kutotumia nguvu kubwa kumuamsha

Sasa Olida ikamlazimu asogelee mlango mkuu wa kuingilia ndani ya nyuma

Akakuta mlango ukiwa haujafungwa kwani ulifunguka mara tu alipousukuma. Hapa ndipo Olida akapokelewa na tukio la kuogofya.

Tilifela Toyi, dada wa Olida alikuwa amelala katikati ya dimbwi kubwa la damu huku mwili wake ukiwa bila dalili yoyote ya uhahi.
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

THE LAWYERS

Sometimes March 2013 Wakili Fatuma Karume alisafiri kutoka Dar kwenda mkoani Kilimanjaro.

Wakili huyu alikuwa amesafiri akiwa amebeba nyaraka furani ya muhimu.

Nyaraka ile alikuwa anaenda kumsomea na kumkabidhi mzee fulani aliyefahamika kwa jina la Juma Actually, Mzee Juma naye alikuwa ni wakili ambaye sasa amestaafu akiwa amefanikiwa kurithisha taaluma hiyo pia kwa mwanae ambaye alikuja kuwa ni wakili maarufu sana mkoni Arusha.

Fatma hakujua kama nyaraka aliyobeba ingeleta taflani kubwa ndani ya familia ya Mzee Juma. Fatma aliwasili nyumbani kwa ambako alikuta waombolezaji ambao walikusanyika baada ya kusambaa taarifa za msiba za mmoja wa watoto wa Mzee Juma.

Fatma alitegemea kuikuta hali hii nyumbani pale na hata safari yake ilitokana na yeye kupata taarifa hizi. Fatma alikuwa amebeba nyaraka ambayo ulikuwa ni wosia wa marehemu mtoto wa Mzee Juma aliouandika mbele ya wakili Karume enzi za uhai wake.

Baada ya Fatma kukaribishwa na kutoa pole kwa wafiwa, akafungua wosia ule na kuanza kumsomea mzee Juma.

Hapa ndipo utata ulipoanzia.. Ukiachana na mambo mengine yaliyokuwemo ndani ya wosia, marehemu aliagiza kuwa mauti yakimkuta, azikwe kijijini Momela wilayani Arumeru.

Mzee Juma aliposomewa eneo hili, ghafla akageuka mbogo Akajiapiza kuwa kama mwanae hatazikwa nyumbani kwake Marangu, hatashiriki maziko.

Jambo hili likaibua sekeseke kubwa pale msibani huku minong’ono ikianza kuenezwa. Kuwa marehemu mwanae hakuwa kwenye mahusiano mazuri na baba yake siku za mwisho za uhai wake.

Baba na mtoto wakiwa hawaongei kwa zaidi ya miaka miwili hadi mauti yanamkuta mtoto huyu.

Mzee Juma ambaye alishikilia rekodi ya kuwa wakili wa kwanza kuapishwa baada ya uhuru wa Tanganyika, alikuwa ni mtu wa misimamo mikali ambaye alijijengea heshima kubwa miongoni mwa watu mashuhuri nchini

Nini ilikuwa shida baina ya Mzee huyu na mwanae?

(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

CODE AND DECODE- USIKU WA MISHEMISHE

Wasaidizi wake walishawekwa bayana juu ya Afya ya “Chief” iliyokuwa ikizorota siku hadi siku.

In fact ripoti ya afya yake walishakuwa nayo kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja.

Ikabidi waitane kikao wanandugu.

Kikao hiki kilikuwa kinajadili mirathi because “they saw it coming”

Wanandugu hawakutaka kabisa yule aliyepo kwenye wosia awe mrithi kwani sio mwanaukoo wao.

Vikao hivi viliendelea kwa siri lakini chief alipopata habari hizi alisononeka sana.

Alisononeka kuona hata wale watu wake wa karibu wakijadili mirathi angali yeye bado yuko hai.

Hawa ndio walimuumiza zaidi,

Lakini taarifa za upande wa pili ambao nao walikuwa wanajadili mirathi hazikumuumiza kwani alijua wao ndio walikuwa nyuma ya maradhi yake.

Hapa nisimame kidogo,

Kasheshe ilishaanza tang usiku jamaa alipowaambia wastaafu wanawashwa na kwamba yeye ndiye Chief kwa wakati ule.

Kauli hii kwa mtu mwenye macho matatu ni lazima ajue ujumbe ule alikuwa anaambiwa nani.

Tayari kulikuwa kunatokota baina ya E1 na “Lulu 1”

Kuna siku Diblo dibala alienda kwa kushtukiza pale kwenye “KOJ”. Tangu jioni aliambiwa “meter” iliyokuwa itumike pale haikuwa imefungwa.

Lakini alipoenda kwa kushtukiza akakuta meter imefungwa. Kama mnakumbuka yule dada alipobanwa alieleza kuwa tangu jana yake alishapigiwa simu afunge meter pale.

Hili swala halikuishia pale,

Ilikuja kubainika kuwa kaka mkuu Muombeni Sefu anavujisha mipango ya E1 kwa Lulu 1.

Jambo hili likamgharimu Kaka mkuu, Pamoja na yule aliyekuwa waziri aliyesomea miamba.

Hiki ndio kilikuwa nyuma ya kauli dhidi ya wastaafu na ramani ya vita ikawa imechorwa baina ya wakuu..
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

THE ASSASIN

Kitendo cha mtu huyu kuingia bila kupiga hodi kwenye ofisi yake ya mapokezi,kilimshitua binti huyu.

Mwonekano wa mtu huyo ulimfanya binti huyo aamini huyu si mgeni wa ofisi yake bali amekosea njia kwani ilikiwa ni mara ya kwanza kumuona mtu yule Binti akagundua jambo lingine Sura ya mgeni yule haikuwa ya kiungwana.

Alionekana kutoyafurahia maisha kwa ujumla Binti akabaki akimtazama mgeni huyu akisubiri kuombwa msamaha wa kukosea ofisi Haikuwa vile! "Jimmy yupo?" Aliuliza mgeni yule bila ya salamu Ikawa zamu ya binti kushangaa Mtu anayeuliziwa na mgeni huyu wa ajabu alikuwa ni bosi wake.

Hakufanana na mtu anayeweza kufahamiana na bosi wake hadi kumtaja kwa wepesi kama anamuongelea muhuni tu wa mtaani.

"Jimmy yupo?" Mgeni akauliza tena

Binti:"Kwani wewe nani?"

Mgeni: "Kwa hiyo yupo?"

Binti: "Yupo lakini ana kikao"

Mgeni: "Mwambie Leno yupo hapa"

Binti: "Akiwa kwenye kikao hataki kupigiwa simu wala kufuatwa"

Mgeni huyu mwenye macho mekundu kama aliyechelewa kulala na kuwahi kuamka akamtizama binti machoni kisha akatamka:- "Kwa hiyo huendi kumwambia?"

Swali lile lilimtisha binti aliamini kuna hatua atakayochukua mgeni yule endapo atashindwa kwenda kumuita bosi wake

Binti: Ngoja nikamwambie

Msichana yule akaelekea ilipo ofisi ya bosi wake Jimmy Kizota, mkurugenzi mtendaji wa kampuni ilipo ofisi ya binti huyu alikuwa amemaliza kuongea na simu wakati binti huyu anaingia ofisini mwake.

Akampasha juu ya mgeni wa ajabu aitwaye Leno Sura ya Jimmy ilajenga Nuru Akamwambia binti huyu aitwaye Zakia kuwa alimtarajia Jimmy akamuagiza Zakia akamuandalie chai mgeni yule na amwambie amsubiri.

Zakia akarudi na kumkuta yule mgeni kasimama palepale

Zakia: Anasema umsubiri

Leno: Atatoka baada ya muda gani?

Zakia: Nadhani hatachelewa, nikuandalie chai au kahawa?

Mgeni akamshangaza tena Zakia

Leno:Nataka urudi tena ofisini kwake!

Zakia:Si nimekuambia ana kikao?

Leno akaongea kwa utulivu "Ni juu yako kuamua, kwenda au kutokwenda, nataka ajue tu zikipita dakika tano kama hajatoka, naondoka"

Zakia bila kupenda akarudi ofisini kwa bosi wake na kumpasha habari hii mpya Zakia alitegemea bosi wake angetoa jibu la kifedhuli alirudishe kwa mgeni huyu asiye muungwana Akashangaa bosi wake anajibu:- "Sawa nimeelewa, huyu mtu namjua mwenyewe" Akamuamuru Zakia amruhusu aingine ofisini kwake.

Jimmy Kizota na Leno Kanaga walijuana tangu utotoni jijini mwanza.

Wakasoma darasa moja shule ya msingi Nyegezi Jimmy ambaye ni mpole ndiye aliyenufaika kuwa rafiki wa Leno mwanafunzi nunda Wanafunzi manunda waliogopa kumgusa Jimmy kwa sababu ya ukaribu wake na Leno Walipomaliza shule ya msingi wakapotezana

Jimmy alipofaulu na Leno kufeli Miaka ikasogea Jimmy akajiunga chuo kikuu cha Dar es salaam Huku akisikia Leno alijiendeleza kielimu mkoani Shinyanga hadi kidato cha nne

Baadae akasikia ameajiriwa na JWTZ mkoani Tabora Miaka ikasogea Jimmy akafungua kampuni ya dawa za kusafisha maji

Akasikia Leno alifukuzwa jeshi akihusishwa na uporaji Fedra katika benki moja Tabora Tukio hilo lilitikisa na kuwa Habari ya mjini Leno akakutwa na hatia na kufungwa miaka 15 Miaka ikakatika Jimmy akafiwa na baba yake Mwanza Msibani akakutana na Leno.

Jimmy akaambiwa Leno amekuwa jambazi aliyekubuhu akishirikiana na wanajeshi waasi wa Burundi wakiteka mabasi na kupora abiria Miezi michache baadae Jimmy akasikia Leno amekuwa muuaji wa kukodi jijini Kampala

Ikapita miaka miwili bila Jimmy kupata habari za Leno Haikumsumbua kwa kuwa hakuwa na mpango nazo Ni mpaka Jimmy alipopata shinikizo fulani ndio akaanza kumtafuta Leno Jimmy akamtafuta Leno hadi akakaribia kukata tamaa Ndipo akatonywa Leno kaonekana Mwanza Jimmy akapata mawasiliano ya Leno Akampigia simu kumtaka afanye hima kuja Dar kwani kuna kazi ya donge nene anataka kumpatia

Jimmy hakumweleza ni kazi gani na aliahidi kufanya hivyo Leno akifika Dar Jimmy akamtumia Leno nauli Pia akampangia hoteli atayofikia maeneo ya Mwenge Leno alifika Dar kwa basi usiku bila kumuona Jimmy stand kumpokea Akampia simu Jimmy Jimmy akamuelekeza akodi Taxi aende Mwenge kwenye hoteli aliyompangia Akamtajia majina mawili aliyoaandikisha ayataje apewe chumba Katika majina yale hakukuwa na hata jina moja la Leno Jimmy akamsisitiza Leno asitaje jina la Leno popote.

Leno alipofika Mwenge na kupewa chumba akampigia tena simu tena Jimmy kumtaarifu amefika Jimmy: "Kesho saa nne asubuhi tuonane ofisini kwangu" akamwelekeza ilipo Hii ndio ilikuwa sababu ya mgeni huyu kufika ofisini hapa Leno aliingia ofisini kwa Jimmy wakatazamana usoni Mwonekano wa Leno ulimshtua Jimmy Leno aliyemwangalia siye yule aliyesoma naye darasa moja Nyegezi Primary school

Huyu alikuwa ni Leno mwingine Sura yake ilijieleza kila kitu Sura ya jambazi na muuaji aliyekubuhu! Leno aliupongeza uamuzi wa waliomtuma kumtafuta Leno Kuwa Leno alikuwa ni mtu sahii aliyehitajiwa. "Karibu kiti Leno" Jimmy akavunja ukimya Leno akaketi

Jimmy: Karibu Dar

Leno: Nimekuja Dar kwa ajili ya wito wako, hebu nieleze umeniitia?

Jimmy akajua Leno hapendi Blah Blah "Nina taarifa zako Leno" Jimmy akavunja ukimya

Leno: Taarifa zipi?

"Umekuwa Assasin" Jimmy akampasukia Leno Tofauti na alivyotarajia kuwa kauli ile ingemshitua Leno,

Leno alibaki akimkodolea macho bila tashwishwi yoyote "Nieleze ulichoniitia"

Leno akamwambia Jimmy

Jimmy: Naitaji taaluma yako ya uuaji kuna donge nono ukiitumia taaluma hiyo hapa Leno akaendelea kumtazama bila dalili ya kujibu lolote

Jimmy: Kuna milioni 20 ziko mezani zikikusubiri ufanye kazi hiyo Leno akamtazama Jimmy kisha akauliza "Unataka nifanye nini?"

Jimmy: Kuna mtu nataka azimishwe

Leno: Yuko wapi?

Jimmy: Hapahapa Dar

Leno: Anahusika na nini?

Jimmy: Ni mfanyabiashara

Leno: Mkubwa?

Jimmy: Si sana ila maarufu

Leno:Anatembea na ulinzi

Jimmy: Ndiyo Leno:Anajihusisha na siasa?

Jimmy: Hapana Usaili ukaendelea

Leno: Anaonekana adharani

Jimmy: Hapana

Leno: Anajua anawindwa auwawe?

Jimmy: Kwa hili hajui

Leno: Anajua kama ana adui?

Jimmy: Anajua ndio maana anatema na ulinzi

Leno: Ni adui yako?

Hapa Jimmy akasita kisha akajibu "ndiyo" Kusita huku kukaonekana na Leno

Leno: Anajua ipo siku utakuja kumuua?

Jimmy: Ndiyo

Leno: Unadhani ipo siku anaweza kukuua?

Jimmy: Ndiyo Leno akatafakari kwa muda kisha akasema "Nahitaji milioni 30, 15 kabla na 15 baada ya kazi"

Jimmy: Nyingi sana Leno:(Huku akiinuka) Tafuta mtu mwingine

Jimmy: Subiri Jimmy: Sawa nimekubali

Leno akaomba apewe wiki moja arudi Mwanza akirudi atakuwa tayari kwa kazi Wakakubaliana atachukua advance akirudi ila apewe nauli ya kwenda na kurudi Mwanza Leno akamtaka Jimmy akirudi awe na taarifa zote kumuhusu anayetakiwa kuzimishwa

Baada ya wiki Leno akarudi Dar bila kumtaarifu Jimmy Safari hii alijitafutia hoteli nyingine tofauti na aliyopangiwa na Jimmy Hata jina aliloandikisha hotelini lilikuwa bandia Akaenda kwa kushtukiza ofisini kwa Jimmy

"Umekuja lini" Jimmy aliuliza

Leno: Tuanzie tulipoishia Jimmy kwanza alimpigia simu Zakia kumwambia kutoruhusu mtu yeyote aingie ofisini kwake Kikao kikaanza Jimmy akampa Leno picha ya mtu anayetakiwa kuuwawa, Leno akaitazama na kuitia mfukoni Usaili ukaanza tena

Leno: Analindwa na walinzi wangapi?

Jimmy: Wanne (Dereva anayemwendesha na mlinzi mwingine mmoja ambao wanakuwa kwenye gari lake, wengine wawili ni dereva na mlinzi wanaokuwa kwenye gari inayowasindikiza)

Jimmy akampa picha ya hali ya ulinzi nyumbani kwa target

Leno: Nani atanipeleka kwenda kuona nyumba anayoishi?

Jimmy: Nitakupeleka

Leno: Nahitaji pia kumuona binasfi huyu mtu

Jimmy: Hilo usijali, nitakupeleka mwenyewe kukuonesha

Leno alamwangalia Jimmy kisha akamuuliza "Nani yuko nyuma ya mpango huu?"

Jimmy: Unamaanisha nini?

Leno: Namaanisha aliyeamuru mtu huyu auwawe

Jimmy: Ni mimi mwenyewe

Leno akatoa tabasamu la karaha kisha akasema "Huonekani kutoa amri hiyo!

Mambo kadhaa yanathibitisha unatumiwa"

Leno: Unakumbuka uliniambia kuwa wewe na mtu huyu ni maadui?

Jimmy: Ndiyo Leno: Na uadui wenu ndio unaopelekea kutaka huyu mtu auwawe?

Jimmy: Ndiyo

Leno: Kama ni adui yako, unakuwa vipi tayari kwenda kunionesha, ina maana hakujui?

Jimmy akawa bubu Leno akaongeza swali, "Lakini pia, inakuwaje mwenzio ajitambue ana adui akajiwekea ulinzi na wewe adui wake usiwe na ulinzi wowote?

Jimmy akatoa macho kama anasoma talaka Leno akazidi kumpasukia Jimmy

Leno: Huna ulinzi wowote hapa ofisini na naamini hata nje hapa. Usiniambie hujui hatari inayokukabili kama kweli huyu ni adui yako.

Huwezi kukubali kunilipa milioni 30 alafu ukafanya ujuha huu. Huonekani kuchezwa na machale yotote. Mtu anayewindwa haishi hivyo" Leno akapasuka

Leno: Nina hakika unatumika katika mpango huu na anayekutuma hataki ajulikane. OK hilo si tatizo langu, nilichotaka kukuonesha ni kwamba mimi sio mtu niliyezubaa, mkawa na wazo baadae mnizike pesa yangu ya kumalizia. Sitajali kujuana kwetu, nitakushukia na kukushughulikia! Ingawa ofisi ile ilikuwa na kiyoyozi, Kijasho chembamba kilimtoka Jimmy Akajitutumua na kujibu "Hakuna atakayekudhulumu, Inaonekana huniamini?"

Leno: Kwenye pesa simwamini mtu yeyote hata mimi mwenyewe

Jimmy: Kwa hiyo utafanya kazi ?

Leno: Ukinipa advance nafanya

Jimmy akafungua kabati na kutoka mkoba uliojaa mabunda ya pesa

Leno akaufungua akawa anahesabu mabunda

Leno: Lini utanipeleka kwenye nyumba ya target pamoja na kumwona yeye mwenyewe?

Jimmy: Leo usiku nitakupeleka ukamwone

Leno: Wapi Jimmy: Kwenye casino yake maarufu nadhani unaifahamu

Leno: Inaitwaje? Jimmy: Casino Afrikando

Leno: Naisikia, Yeye ndiye mmiliki?

Jimmy: Ndiyo, Nakuonya usimchukulie poa kwa kuwa mmiliki. Ni mtu hatari na mafia wa kutupwa

Leno: Anaitwaje?

(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY BUYOBE
THE CUT CHAIN: "MAUAJI MLINZI WA TEMBO"
Imagine this,
Unamaliza Chuo
Mungu anakuona unapata kazi Benki.
Maisha yako yanabadirika unahama kwenye nyumba ya familia Temeke Ulikokuwa unaishi na Mama,Dada na Kaka yako na Unahamia Mikocheni B.
Mungu anazidi kukuona,
Unanunua gari IST ili atumie mama na kaka yako ambaye ni mlemavu.
Yes!

Wewe si mbinafsi, Una upendo wa mshumaa kwa familia yako.
Unawapa gari watumie wakati huna gari nyingine.
Yote hii ni kwa sababu mama yako anahitaji kupelekwa hospitali mara kwa mara.
Pia kaka yako ni mlemavu wa mguu kwani anatumia mguu wa bandia.
Shukrani za Punda!

Je, Ungeweza kubashiri kuwa wema wote huu ungekuja kukuingiza katika kesi mbaya kabisa?
Unashtukia tu Askari polisi anakuja nyumbani kwako Masaki.
Kwenye maegesho ya magari ipo gari yako.
Of course huwa sometimes unaitumia.
Askari anakuuliza hili ni gari lako?
Unajibu YES!
Kinachofuata ni gari yako kukamatwa na wewe pia kupelekwa Oysterbay Police ambako unaambiwa unashitakiwa kwa kesi ya mauaji.
Unabaki kwenye mtanziko.
Baadae unagundua dada na kaka yako pia wako pale kituoni Accused of the same Crime
Watu wengi wamefurahi baada ya kutolewa kwa hukumu iliyowakuta watu 11 na hatia ya kula njama na kutekeleza mauaji ya aliyekuwa Mkurugenzi mwenza wa PAMS foundation ndugu WYNE DEREK LOTTER
Lakini hawakubaini kuna mnyororo fulani wa Ushaidi ulikatwa kwa manufaa ya walioukata.
Lakini huyu Wayne Lotter ni nani hadi asukiwe genge la kupokonya uhahi wake?
Alizaliwa nchini Afrika Kusini na alijihusisha na biashara ya uwindaji (Ranger)
Baadae mapenzi yake kwa wanyama, yakamfanya afungue taasisi ya kuwalinda wanyama dhidi ya majangili
Akaja Tanzania mwaka 2009 ambako kulikuwa na visa vingi vya biashara haramu ya meno ya tembo na faru.
Akafungua taasisi ya PAMS foundation.
Kama mnakumbuka kile kisa cha rubani kupotea akiwa angani, Basi ndege hii ilikuwa ni ya shirika hili la PAMS
Wyne Lotter kwa kushirikiana na Task force maalum (NTFAP) ya kupambana na ujangili waliweza kuukata mtandao wa wawindaji haramu na kufanikisha kumkamata raia wa China Yang Fenglan maarufu kama malkia wa Tembo.
Huyu alitajwa kama kiungo kati ya majangili na wateja wa meno hayo.
Mama huyu wa kichina ambaye aliingia nchini tangu 1970’s na akajifunza kiswahili, alikuja kutumika sana kama mkalimani wakati wa Ujenzi wa reli ya Tazara.
Akarudi China baada ya reli kukamilika mwaka 1975 akaajiliwa na serikali yake Idara ya biashara ya china na nchi za kigeni.
Akarudi Tz mwaka 1998 akapanga nyumba ya ghorofa moja ambapo chini alifungua mgahawa wa kichina na Juu akafungua kampuni ya BEIJING GREAT WALL INVESTMENT
Hapa ndipo connection zote za bishara nzima ya ujangili sio kwa East Africa tu bali Wordwide zilifanyika.
Mwanamke huyu akaja kuwa gumzo katika dunia ya uifadhi wa wanyapori kila nchi ikimnyooshea vidole huku kelele zikipazwa kuwa wanaokamatwa ni vidagaa tu huku huyu mama akitamba mtaani.
In fact hakukuwa na ushaidi wa kumuunga kwenye kesi ingawa alikuwa akifatiliwa na mamlaka zetu.

Sasa bwana Wyne Lotter akafanikisha kumnasa mama huyu.
Tukio hili lilimfanya aliyekuwa Producer wa filamu ya “IVORY GAME” mwigizaji na muaandaaji filamu LEONARDO DE CAPRIO kumuomba awe muhusika mkuu kwenye filamu hiyo lakini Lotter akaomba wapewe nafasi Rangers wake badala yake.
Kwa hiyo Lotter aligeuka kuwa mwiba kwa majangili.

Alitoa mafunzo ya Ulinzi kwa vijana zaidi ya 900 Tanzania nzima kulinda Tembo.
Akafadhili task Force ya serikali kidhibiti ujangili
Hakujua kwa kumkamata Queen of Ivory alikuwa ameng’oa kilaka kwenye jeans ya bishoo.
Naam!
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY BUYOBE

UGAIDI TANZANIA

Nimepokea maoni mengi watu wakitaka kujua kwa undani habari za magaidi waliopata kusumbua sana hapa nchini kwetu. Wengi waliuliza maswali ya kina kutaka kujua magaidi wale walifikaje huku kwetu, walianzia wapi, walikuwa na motive gani, nani alikuwa nyuma yao,Viongozi wao, operations za kuwatoa zilikuwaje nk.

Nikijibu kwa ufupi magaidi wale walikuwa na mlengo wa “Jihad”na mafadhili wao mkubwa ilikuwa ni NGO moja ya nchini IRAN na hata nchi ya Kuwait ilihusika kwani nchi hii ilikuwa ikitoa matamko mengi wakati nchi yetu ilipoanza kuwashughurikia.

kwa mara ya kwanza waliingia nchini kwetu kupitia ZANZIBAR

Walipoingia zanzibar walijifanya ni watu wa kutoa sana misaada kama kuchimba visima vya maji, misikiti na pia kuwachukua vijana kwenda kuwasomesha nje ya nchi lakini masomo waliyokuwa wakiishia kufundishwa ni ya ujasiri na kujitoa mhanga.

Walipofanikiwa kuweka mizizi ndani ya visiwa vya Zanzibar lengo lao kuu lilikuwa ni kukamata majiji yote makubwa kama ARUSHA, MWANZA, DAR ES SALAAM na pia kuweka ngome katika maeneo yote ya pwani ya bahari ya hindi

Kwa ukanda wa Tanzania kiongozi wao mkubwa alikuwa ni SHEIKH MZUZURI. Sponsor wa wakati ule alikuwa akipewa taarifa zote za kiintelejensia lakini alikuwa hatilii maanani kwani alipumbazwa na misaada ya nje ambao watu hawa waliitoa. Ilikuwa vigumu kuhisi kama watu hawa ni magaidi

Wakaja kuwapata baadae SHEIKH FARID HAMAD AHMED(aliyekuwa kwenye kesi ya uamsho) na mwingine akiitwa MSELLEM

Watu hawa waliwatafuta maagent kwenye kila kanda na kuwapa uongozi wa kanda.

Isingekuwa tukio la kuuwawa mmoja wa gaidi aitwaye KAPELA maeneo ya chanika, Tusingekuwa na fununu kabisa ya mipango yao.

Mawakala kama nilivyowataja walisambaa maeneo ya mkuranga, kibiti,rufiji na ngome yao kubwa ilikuwa Amboni Tanga(kwa kupitia mtiririko wa matukio nitafafanua hili)

Sasa kwa kuwa jamaa waliingia kwa mbinu kama wahisani, Maajenti wao walikuwa wanawashawishi vijana kuwa kuna kazi za kulima mikoa ya bara ambapo kwa wiki malipo ni Elfu hamsini. Kwa kuwa vijana hawakuwa na ajira walivutika na offer hii.

Naomba nimnukuu mmoja wa Askari “who set his foot in battlefield” ambaye alinipa mtiririko wa matukio “on anonymity conditions”

“Kwanza ilikua ni kimanzi chana kabla ya kwenda amboni ndio watu wakashtuka kumbe mambo sio mambo tulijua ni vibaka wamevamia kituo na kuua askari”

“tukaitwa kikosi maalum Cha ...section...hapa ...,tukaungana na FFU hapahapa...na section...CID pamoja na Askari wa kikosi Cha CYBER tukafunga safari na kwenda kimanzichana mkuranga kituoni palee tukapata ABC tukaenda kituoni pale kimanzichana tukakagua eneo lote pale kituoni”

“Kulikuwa na nyumba ya raia ipo jirani Sana na Kituo ambapo askari mmoja alipata hifadhi na akajifungia mule muda wa uvamizi. wenzake wakati nao wanatoka kituoni kutafuta hifadhi wakauwawa

(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
UNAJUA MWANAO ALIPO?
Swali hili linaweza likawa kama vile ni la Kipumbavu kwako.
Kwa wale wa kishua inawezekana jibu lao likawa hivi;
Mwanangu anafatwa na school-bus Asubuhi kupelekwa shuleni, ambalo litamrudisha nyumbani,
Atashinda na dada/houseboy/Uncle mpaka tukakaporudi
Tena kwa wengine anaweza kuendeleza ratiba kwa kusema kuwa baadaye atakutana na mwalimu anayekuja kumfundisha nyumbani/ataenda swimming class/football class
Naam
Let’s hope that, this routine is safe.
But I am sure you will be hyper vigilant as you will continue reading.
Yumkini Kwa Mzazi wa Kikistro utasema namlea mwanangu awe na hofu ya Mungu hivyo huwa nampeleka Sunday School.
Lakini je ni mara ngapi tumesikia kesi za Makasisi kulawiti?
Yameshatokea sana huko Moshi na Iringa
Pia Kwa Mzazi wa Imani ya Kiislamu atasema mimi mwanangu nampeleka Madrasa apate hofu ya Mungu.

Je ni mara ngapi pia tumesikia mikasa ya Maimamu na walimu wa Madrasa kulawiti au kubaka watoto?

Tuhame hapo, tuamie kwingine

Tuangaze ratiba ya Mtoto wa Uswahilini anayetoka familia yenye Baba Ngariba, Mama Nyakanga na Mjomba dobi.

Huyu atatembea/kupanda daladala kwenda shuleni, wakati wa mapumziko ataenda kula mihogo au visheti vinavyouzwa eneo la shule (kama hana hela ni mashaka zaidi)

Baada ya masomo atarudi mwenyewe nyumbani.

Je, Hapo ofisini au kokote ulipo kwa sasa, umeshajiuliza mwanao yuko wapi kwa sasa?

Read this story!

The story is itself already Very Sad.

Kwa kuwa mhusika ni mtoto, nitatumia jina la Kubuni la MAJUTO kumlinda ingawa mkasa ni halisi.

MAJUTO alikuwa ni mwanafunzi katika shule ya Msingi Mwangaza wilaya ya Temeke.

Mwaka 2016 Majuto alikuwa na umri wa miaka 12.

Kulingana na maelezo ya Mwalimu wake aitwaye KHADIJA MAKURU, alianza kuwa na wasiwasi juu ya mabadiliko ya tabia za Majuto.

Majuto alianza ghafla kuwa anachelewa shuleni,

Akawa anasinzia darasani

Na zaidi Majuto uwezo wake darasani ukaporomoka wakati alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi “vipanga”

Mabadiliko haya ndiyo yakavuta “attention” ya Mwalimu Khadija kwa Majuto.

Sio Mwalimu Khadija pekee aliyeanza kumuwashia “Full lights” Majuto.

Swala la Majuto liligunduliwa na walimu wengine na hadi likafika kwa Makamu Mwenyekiti wa “School Baraza” ndugu JUMA SALUMU TETERE

Majuto akaitwa kuhojiwa

And here is where the heart of this story centers

Majuto alipohojiwa ni kwa nini kashuka kitaaluma akatoa maelezo yanayoweza kukufanya msomaji “upige ukunga”

Majuto akaeleza hivi namnukuu

“Tangu shule ilipofunguliwa mwezi January hadi July 2016 kuna mkaka mmoja aliyekuwa ananivizia njiani nijapo au kutoka shule”

Majuto akaendelea

“Huyu mkaka alikuwa ananilazimisha nimuite “uncle” na alikuwa ananikamata na kunipeleka kwake au vichakani”

“Nikifika huko alikuwa anatoa mdudu wake na ......(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post

SAKATA LA TEGETA ESCROW

Najua wengi wanalijua swala hili kwa juu juu kwa kuwa linazungumziwa kwa lugha ya kipigaji ya kitaalamu kiasi cha kuwatoa kwenye reli wanaotaka kulielewa sakata hili.

Makala yangu itajitahidi sana kuongelea hili sakata kwa lugha nyepesi ili wote tuelewe.

Picha linaanza kwa Kijana mmoja wa kamamo wa Kihaya kuacha kazi benki kuu ya Tanzania

Kijana huyu japo umri umesogea kidogo anajiunga chuo kikuu cha Dar Es salaam kama “mature student)

Kijana huyu analiza chuo kile kwa kuibuka na “First class” ya biashara.

Kijana huyu baadaye anakuwa mmoja wa shareholders kampuni ya kwanza ya mawasiliano Tritel.

Anamiliki shares kupitia kampuni yake ya VIP Engineering and Marketing

Huyu kijana ni mtu mwenye akili nyingi sana,

Ni bingwa wa lobbying na negotiations.

Enzi zile ukiwa na deal yako yako kubwa ya biashara ambayo inahitaji ushawishi basi isingekuwa ajabu kuelekezwa uonane na kijana huyu ili mambo yako yakunyookee.

Kama umeangalia series ya “The Godfather” basi si vibaya ukimuita kijana huyu “le Conciliale”

Baadaye mzee huyu kupitia kampuni yake ya VIPEM (VIP Engineering and Management) akaingia ubia na kampuni ya Malaysia iitwayo MECHMAR.

(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUSOMA MAKALA KAMILI NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA ) click here to unlock the post