

Fortunatus Buyobe @Buyobe
The untold story of Muhammad kirumira of UG. click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
WIZI WA FEDHA ZA PADRE PASCHAL LUHENGO
Kama unakumbuka vizuri, Mwaka jana ilisambaa mitandaoni video ya Padre wa kanisa katoliki akimuomba Rais @SuluhuSamia amsaidie tatizo lake.
Tatizo hilo lilimdababishia vitisho vilivyomfanya arekodi video ile akiwa tayali amekimbia nchi.
Ni tatizo gani?
Kwanza Padre huyo alibaini majaribio kadhaa ya kuingiliwa kwa akaunti yake ya barua pepe.
Akajitahidi kukwepa majaribio hayo kwa kubadilisha nywira (password) ya akaunti yake.
Padre akajua amefanikiwa kuwadhibiti waliojaribu kuingilia akaunti yake ya barua pepe
Hakujua
Baada ya kubadili password mara kwa mara, ulifika wakati akaunti yake ikawa haifunguki kila akiingiza nywira.
Kitendo hicho hakikumshtua kama akaunti yake ya barua pepe imeingiliwa, bali alijua imefungiwa.
Hata hivyo, alibaini kama kuna tatizo Oktoba 27, 2020 baada ya kuomba msaada wa fedha kidogo kwa rafiki yake, Padri LEOPOLD MLIMBO anayeishi nje ya nchi.
Padri Mlimbo alimtumia Dola za Marekani 545.25 (Sh. milioni 1.2) kwa njia ya Western Union.
Namnukuu
“Baada ya Padri kuniambia ameishanitumia, nilikwenda posta Ifakara kuchukuwa fedha hizo. Nilipofika wakaniambia muamala huo haupo mtandaoni,”
Baada ya tukio hilo, siku chache baadaye akapigiwa simu na rafiki yake ambaye ni daktari huko nchini Austria.
Rafiki yake huyo alikuwa anaulizia maendeleo ya matibabu yake ya kubadilishiwa figo.
“Nilishangaa na nikamwambia mimi ni mzima kabisa, sina tatizo lolote la afya, rafiki yangu akaniambia kwamba alipokea barua pepe kutoka kwangu nikiomba msaada wa fedha za matibabu ya kubadilishiwa figo na yeye alikuwa ameishatuma mchango wake, pia baadhi ya marafiki zangu wengi”
Baada ya taarifa hizo, Desemba 5 2020 alikwenda kuripoti katika kituo cha polisi kinachohusika na mambo ya uhalifu wa fedha (Financial Crime Unit) ambacho kipo Kamata, Dar es Salaam.
Akawaeleza askari wa kituo hicho kwamba akaunti yake ya barua pepe imevamiwa na wezi ambao wanaiba fedha kwa njia ya Western Union.
Polisi wa kituo hicho walimwambia aende kuripoti Kituo cha Polisi Msimbazi, Kariakoo, Dar es Salaam.
Wakati anakwenda kuripoti, akapata taarifa nyingine
Kwamba rafiki zake huko Ulaya wanataka kumtumia dola 200,000 (zaidi ya Sh milioni 400) za ujenzi wa kanisa.
Safari hii, rafiki zake walielekezwa na wezi hao walioingilia akaunti yake ya barua pepe, watume fedha hizo kupitia Benki ya BOA.
Akatajiwa taarifa za Account inayotakiwa kutumiwa pesa
Bank Name : BOA Bank
Bank Adress ; NDC Dev’t House, Ohio Street/Kivukoni Front
P.O Box 3054, Dar es Salaam, Tanzania
Branch : Msimbazi Branch
Account Name (Jina la akaunti): LUPIRO MAHENGE PARISH
Account No (Akaunti namba): 01646030005
Swift Code: EUAFTZT
Padre akaona sasa swala linazidi kuwa zito
Akaenda kituo cha Polisi Msimbazi akatoa taarifa za awali pamoja na mpya alizotoka kupata punde.
Akafunguliwa jalada
MS/RB/9245/2016 na MS/RB/9244/2016
Polisi Msimbazi wakawataarifu BOA na wakachukua nyaraka kubaini wamiliki wa akaunti iliyofunguliwa kwenye benki hiyo. Kesi na vielelezo vyote vikapelekwa kitengo cha polisi kinachoshughulika na mambo ya Finance Crime Unit ambacho kipo Kamata jijini Dar es Salaam,
Yakafata mazingaombwe…..
Kama nigepewa kuipeleleza kesi hii, hakika ilikuwa nyepesi kwani ningeanzia na mtu aliyefungua akaunti benki na nyalaka alizotumia
Polisi walifanya hivi
Wakapata hadi picha ya account holder
Alikuwa mmiliki wa shule moja maeneo ya Tabata.
Namnukuu padri
“Wamenipa picha za mtu aliyefungua akaunti BOA Bank na wakaniambia ni mmiliki wa shule ya sekondari huko Tabata, na wameishamwita wakamuhoji, akasema yeye sio mwizi ila akawataja watu wanaohusika na wizi wa aina hiyo, baada ya maelezo hayo polisi WAKAMWACHIA,”
Tukomee kwanza hapa ili tujiulize maswali
(SUBSCRIBE ILI KUPATA MUENDELEZO WA MAKALA HIII NA ZINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA)
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
UKWELI USIOUJUA KUHUSU BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA
Marehemu huwa haongelewi kwa mabaya, Lakini matendo yao hapa duniani hayatufungi mikono kuyajadili kwa ajili ya mafundisho ya vizazi vijavyo.
80% ya Madawa ya kulevya yanayopatikana Tanzania, Si kwa ajili ya watumiaji wa ndani.
Naam!
Madawa haya si kwa ajili ya soko la Tanzania ingawa yanapatikana kwa wingi nchini kwetu.
Tanzania ni kama lango tu(Corridor) kwa ajili ya kupitisha madawa haya mpaka kwenye soko lililokusudiwa (Target Market)
Ni kwa nini yasitumike ndani wakati walaji wapo hapa hapa?
Jibu ni jepesi sana,
Gharama!
Yes , Gharama!
Madawa haya huwa ni very expensive kwa watumiaji wa ndani kuweza kuyamudu. Ni watanzanzia wachache wenye uwezo wa kumudu gharama za madawa haya.
Ni kwa sababu hii walaji wengi wa ndani huishia kula makapi (by products) aka “Ngada”
Makapi haya ndio huwa na madhara makubwa kwa mtumiaji kuliko wale wanaotumia kitu “pure” kabisa.
Ok.Tumejua kuwa Tanzania ni njia tu!
Je “Mzigo” hutoka wapi na kwenda wapi?
Here we are!
Nifatilie taratiiibu nikielezea habari hii kwa kunuu Chanzo.
“Mzigo huwa unatoka either “Kwa Pele” au “Kwa Musharaf”
Ndugu Msomaji, Popote litakapotumika neno “Kwa Pele” jua ni Brazil na “Kwa Musharaf” Jua ni Pakistani.
Hizi nchi huitwa kwa Codes hizo ndani ya Ulimwengu wa wasafirishaji.
Kwa hiyo mzigo unatoka Brazil au Pakistani
“Mzigo ukitoka huko anapewa mbebaji mmoja ambaye husafirisha kwa kuyameza mpaka Dubai.
“Hasafiri bila mipango kuwa imesukwa tangu anakotoka mpaka Dubai”
“Akifika Dubai Safari yake inaishia pale na analipwa kabisa Chake pale pale.”
“Anaishia pale kwa Sababu Passport ikisomeka imegongwa mihuri ya Kwa Pele au Musharaf basi maafisa Ukaguzi viwanja vya ndege huwa makini sana na mzigo wowote uliobeba”
“Ili kuepusha mzigo kudakwa inabidi mtu wa kwa pele au Musharaf aishie Dubai”
“Tangu mzigo unapotoka shambani, tayari anakuwa ameshaandaliwa “punda” mwingine ambaye atameza ule mzigo pale Dubai na kuuvusha mpaka Msumbiji”
“Huyu naye ataishia Msumbiji tu na kulipwa Chake”
“Kutokea Tanzania, Punda mwingine atavuka mpaka Msumbiji kwa kukata passport ya masaa 24 tu”
“Si rahisi maafisa usalama kumshtukia mtu huyu ambaye kavuka tu Kuingia Msumbiji na baada ya Masaa katoka”
“Punda huyu ndiye atakayemeza mzigo wa Msumbiji na kuuingiza Mtwara/Lindi”
So ndugu Msomaji Umeona “Triangle of Custody” ya Mzigo kuanzia shambani mpaka umefika mikoa ya Kusini.
Njia unavyokuja haiachi traces zozote kwa yule aliyefanikiwa kuufikisha kwenye point aliyoelekezwa.
Huwa kuna Viapo na binadamu anawezwa kutumika kama “bond” ya kiapo.
Mzigo Ukifika kusini, Sio mwisho wa safari, Mzigo ule hukutana na wakemia wenye uwezo wa kucheza na Molecular formula ya fawa zile kuzifanya zisomeke kama raw materials ya dawa zilizokubalika kwa matumizi ya binadamu. (Refer HYDROCARBONS)
Naam!
Wanageuza nyekundu kuwa Njano.
Kuanzia hapa sasa ndio matawi ya Kusambaza mzigo huu yanapoanzia either kwenda nchi kama Congo, Nigeria, South Africa mpaka kwa watumiaji wenyewe kabisa Marekani, China etc.
Leo nashuka na Mkasa wa mabinti wawili walioingia kwenye biashara hii mwaka 2013.
Katika mkasa huu ndipo ilipoonekana kuwa mapambano dhidi ya biashara hii ni sawa na kujichimbia kaburi lako Mwenyewe.
SUBSCRIBE HAPO CHINI ILI KUPATA MKASA HUU NA MINGINE MINGI KWA MWEZI MZIMA
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
KUTOWEKA KWA WAUZA SIMU CHINA PLAZA
Kuna wakati unaweza unaweza kushindwa kusafiri kwa sababu tu basi ulilopanga kusafiria limekuacha baada ya kuchelewa.
Hupaswi kujilaumu kama hili litakutokea.
Mara nyingine Mungu huwa anaingilia kati ili kukuepusha na baya ambalo lingeweza kukutokea endapo ungekuwa ndani ya basi hilo.
Ni mara ngapi tumesikia watu wakitoa shuuda kuwa gari fulani lilimuacha na kisha mbeleni gari hilo likapata ajali?
Hili ndilo lililomtokea Moses John miaka miwili iliyopita.
kijana huyu ni muuza simu katika jengo la CHINA PLAZA lililoko mtaa wa Aggrey Kariakoo.
Tarehe 26 December mwaka 2021, vijana kadhaa ambao wote wanajishughurisha kuuza simu kwenye jengo hilo, walikubaliana waende wakasherehekee sikukuu ya Christmas katika fukwe za Kigamboni.
Majira ya saa 6 mchana, Kijana mwingine aitwaye Rajab Mdoe aka Choiya akampigia simu mama yake mlezi aitwa Taabu Said Banga (Rajabu ni mtoto wa marehemu mdogo wake na Taabu)
Haya ndio yalikuwa maongezi yao
Rajab: Mama, utatumia gari lako leo?
Bi Taabu: Hapana, Kwa nini unaniuliza hivi?
Rajab: Nataka kulitumia…Leo tunataka kwenda beach Kigamboni na rafiki zangu
Bi Taabu: Hakuna shida. Unaweza kulitumia.
Bi Taabu anaishi Tabata Kinyerezi wakati mwanae anaishi Bonyokwa.
Majira ya saa 8 mchana, Rajabu akafika Kinyerezi akiwa ameambata na rafiki yake aitwaye Tawfiq Mohamed.
Baada ya mazungumzo na mama yake, wakachukua gari aina ya Toyota IST jeusi kwa rangi.
Wakaeleza kuwa wanampitia tena rafiki yao mwingine aitwaye Hemed Abass
Wakaondoka.
Makutano (RV) baina ya vijana hawa na wengine walionuia kwenda Kigamboni, ilikuwa ni Kariakoo wanakofanyia kazi.
Mpaka gari inafika kariakoo waliwakuta vijana wenzao ambao ni Edwin Kunambi na Seif Swala
Ambaye hakuwa amefika ni Moses John ambaye alichelewa kufika walipokubaliana wampitie hivyo wakamuacha.
This was a lucky accident to Moses!
Kwa nini nasema hivi?
Ni kwa sababu vijana wale hawakuonekana tena kwa macho ya kibinadamu as the became microscopic.
Walipotea kama sindano!
Neno la mwisho kutoka kwao ulikuwa ni ujumbe ambao Edwin alimtumia Moses kuwa wamekamatwa wakiwa eneo la Kamata na wanapelekwa kituo cha polisi cha kati.
Rafiki zao wa Kariakoo, wakaenda kuwafatilia central polisi lakini majibu yakawa ni hawajafikishwa pale.
Jitihada zikahamishiwa kwenye vituo vya Oysterbay, Msimbazi, Salender Bridge lakini nako wakaambulia patupu.
Hadi wakati huu, ndugu wa wazazi hawa hawakuwa na taarifa kuwa watoto wao wamekamatwa.
Majira ya saa 4 usiku, Bi Taabu alimpigia mwanae simu kumuuliza kama amesharudi.
Simu ile iliita bila kupokelewa.
Majira ya saa 6 usiku alipojaribu tena kumpigia mwanae, simu ilikuwa haipatikani.
Akaamini labda imeishiwa chaji akaamua kwenda kulala.
Hali hii ilikuwa pia kwa mzee Longili Martin baba wa Edwin Kunambi
Yeye hakujishughurisha kabisa kumpigia mwanae kwani alishaongea na mwanae alipompigia kumtaka ajumuike naye kusherehekea sikukuu ya Noel nyumbani kwake Gongolamboto.
Edwin akamjibu hataweza kufika kwani ametingwa na shuguri lakini akamwambia baba yake atajumuika naye kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya.
Hivyo Mzee Longili naye hakuwa na fununu juu ya yaliyomsibu mwanae Edwin
Siku ikapinduka.
Tarehe 27 Dec 2021 bila fununu
Bi Taabu ndiye alikuwa wa kwanza kupata taarifa.
Majira ya mchana tarehe 27 Dec, walifika nyumbani kwake vijana wawili waliopakiwa mshikaki kwenye bodaboda
Vijana hao walijitambulisha kama Babu Ally na Musa (Moses)
Wakaeleza kuwa kija Rajabu walikamatwa tangu jana lakini wanawatafuta bila mafanikio.
Wakaeleza wamefika pale baada ya kutoka kuwaulizia kituo cha Stakishari bila mafanikio pia.
Kwa mtindo huu taarifa zikawafikia ndugu wa Tawfiq, Seif, Edwin na Hemedi.
Then the men-hunt was launched
Hakuna Hospitali, Vyumba vya maiti na vituo vya polisi ambavyo hawakutembelea jijini Dar bila mafanikio.
Hili lilifanyika kwa wepesi kwa kuwa walijigawa kwa timu tano tofauti.
Habari hii ikaanza kuenea kwenye mitandao ya kijamii “like a bushfire in harmattans”.
Nikawa nausoma mchezo kutokea benchi
Let me declare my Interest…
Kaka wa mmoja wa vijana hawa used to be a friend to me.
Kaka huyu ni maarufu kwa jina la DJ Mario ambaye enzi hizo alikuwa ni DJ wa Club ya Rainbow jijini Dodoma (sijui kwa sasa)
Mdogo wake aliyepotea kama sindano ndiye Tawfiq Mohamed
Niweke angalizo mapema wakati nikiwaletea kisa hiki kuwa mjua mtu aliyekaribu na victims hakunifungi mikono kwa vyovyote kueleza “nothing but truth”
Na pia navikumbusha vyombo husika kuwa kuna watu are being killed softly kwa trauma ambayo imebaki nyuma ya mkasa huu.
Just try to imagine mama wa Tawfiq (Sylvia Quentin) ambaye ni si Mkristu anashiriki misa ya Mwamposa online akiomba Mungu amtendee muujiza mwanae arudi mchungaji huyu akipanda madhabauni.
Hli linafanyika mwaka mzima ukiwa umepita bila mwanae kupatikana.
Anaeleza kuwa anaugua maradhi ya moyo tangu kupotea kwa mwanae anashidwa kutoka kujihangaikia.
Pia Naima Ndyanabo, mama wa Hemed Abass anaeleza kuwa sasa amebaki akimtumaini Mungu pekee ndiye atakayeweza kumrejesha mwanae na imani yake kwa jeshi la polisi imetoweka.
Kwa hiyo however how serious the crimes these youngsters have committed, kitendo tu cha kuwaona mahakamani huku wakinyimwa dhamana kitawapa relief ndugu zao.
Yafuatayo ndio yamechipuka nilipoanza kuufatilia mkasa huu.
Katika kuchunguza maisha binafsi ya watu hawa, imesemekana vijana hawa walikuwa watu wa “bata” sana!
Walikuwa wanapenda kujirusha kidimbwi, Small planet etc ambako huko pombe zinaletwa huku ukiwa umewashiwa mishumaa inayotoa cheche ndongo kama baruti
Gharama za vinywaji na chakula maeneo haya huwa zimechangamka sana.
Kwa “winga” wa kuuza simu tu pale China Plaza, kumudu kufanya haya mara kwa mara kuna “invite a strong suspicion” ingawa unaweza unaweza kuwa na kipato kingine kukuwezesha
Wengine wakidai nje ya kuuza simu, walikuwa pia ni madalali wa kuuza magari Ilala.
Katika kuchimba zaidi, likaibuka swala la IMEI za simu
Hapa ndipo picha zikaanza kufunguka
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA )
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
License to kill
Baada mashambulizi ya September 11, 2001 nchini Marekani, mkurugenzi wa idara ya ujasusi Marekani (CIA) bwana George Tenet alikuwa kwenye kitimoto.
Hii ni baada kubainika uzembe mkubwa mkubwa ambao idara yake iliufanya.
Kuna mambo watendaji wa chini yake walikuwa wanayajua na hayakuwa yamefikishwa kwake hadi tukio linatekelezwa.
Alipobaini jinsi taarifa zile zilivyo nyeti, mkurugenzi huyu aligonga kwa nguvu meza yake na kutukana;
“We’re Fu..ed”
Mkuu wa idara ya kupambana na ugaidi CIA (counter-terrorism Center) ampako lilikuwepo dawati maalumu la Osama bin Laden ilimbidi awe akilala ofisi ya CIA kwa siku tano mfululizo akijibu hoja juu ya uzembe ule.
Mkuu huyu bwana Coffer Black alijiona na hatia ya kushusha hadhi ya shirika hilo.
Pengine CIA wangefanya kazi yao kwa kushirikiana na FBI, mashambulio haya yasingeweza kutokea baada ya kuzuiliwa mapema.
Lakini kulikuwa na mahusiano mabovu sana baina ya idara hizi mbili kutokana na kila idara kujiona ni ya muhimu kuliko nyingine.
CIA waliamini FBI ndio waliokuwa wanawajibika kuwapatia taarifa zao zote za kiintelejensia na wao kuzichakata, wakati wao CIA wakichagua nini cha kuwapa au kutowapa FBI
Ingawa CIA walikuwa sahii, lakini walikuwa wanajikuta wanamzigo mkubwa wa taarifa ambazo ziliwashinda kuchakata zote.
Hivyo wangeshirikiana vizuri na FBI inawezekana sambulio la September 11 lingeweza kuzuilika.
Kwa nini naandika haya?
Nisome!
Baada ya shambulio la sept 11, wataalamu wa tehama walipopitia taarifa mbalimbali ndani ya mifumo ya makao makuu ya CIA jijini Virginia, walibaini taarifa za kushtua.
Ni kwamba kumbukumbu mbalimbali zilibainisha kuwa, CIA walikuwa wanawafatilia kwa muda mrefu watu wawili.
Watu hao walikuwa ni kati ya waliohusika na shambulizi la september 11
Ni kwamba CIA ilikuwa inawafatilia watu wale tangu walipotoka hadi walipoingia Marekani lakini mwaka 2000 wakaachana na swala hilo.
Naam!
Kwa zaidi ya mwaka mmoja watendaji wa CIA walikuwa wanafahamu watu hawa walikuwa ndani ya Marekani lakini hawakuwajulisha FBI
Issue inaanzia mbali tangu wakati wa shambulizi za balozi za Marekani Tanzania na Kenya mwaka 1998
Balozi hizi ziliposhambuliwa, ilitumwa timu ya FBI kuja kupeleleza.
Jijini Nairobi, mmoja ya watu waliohusika na ulipuaji wa ubalozi alikamatwa siku 20 tu baada ya tukio.
Huyu alikuwa ni Mohammed Rashed Daoud al-Owhali.
In fact alipaswa kujitoa mhanga kwenye tukio lile, lakini alipofika kwenye ubalozi alishuka na kumrushia mlinzi kitu kama bomu la kurushwa kwa mkono na kukimbia.
Dereva aliyebaki kwenye gari lenye bomu ndio akajilipua na bomu badala yake.
Hata hivyo mtu huyu anayekimbia aliweza kuunguzwa mgongoni na mkononi kwa bomu lililolipuka nyuma yake.
Mtu huyu akakimbilia hospitali za uchochoroni kutibiwa ambapo madaktari waliompokea waliyashuku majeraha yake wakatoa taarifa polisi.
Polisi wakamkamata na kumkabidhi kwa FBI
So the guy was now going to help the FBI with investigations.
The phrase “helping with investigations” doesn’t necessarily mean that yo sit with the FBI on a sofa coach, sipping juice while giving your views to what might’ve actually transpired on the crime scene
Totally wrong,
You will simply see one colorless and clueless person approaching your hairy tennis balls with a ‘burdizzo’ ready to perform a free testicles surgery on your balls if you are uncooperative.
It is in this way, Afisa wa FBI bwana Daniel J Coleman alimfanyia mtu huyu ‘a gentle interrogation’
Mtu huyu akaanza kurap
Jinsi alivyosafiri kutoka Pakistan mpaka Kenya
Hadi jinsi alivyotoroka kuwa tarishi wa Mungu (rasul Allah) kwa kujilipua kwa bomu na kwenda kutibiwa hospitali.
Akaeleza hadi alivyoficha bafuni funguo za kufuli la gari lililokuwa na bomu kwenye hospitali aliyokuwa akitibiwa pamoja na risasi moja.
Kuna kosa kubwa sana mtu huyu alilifanya…
Ni kwamba, alipokuwa hospitali alipiga namba moja Yemen kuomba atumiwe pesa ili ajitibie na nauli ya kuondoka Nairobi
Naam
Namba 967-1-200578
Namba hii alipiga kabla na baada ya tukio la ulipuaji wa ubalozi wa Nairobi.
Aliwapa FBI namba hii baada ya FBI kukubali ombi lake la kuomba akashitakiwe Marekani na sio nchini Kenya
(I think he believed that Kenyans would’ve brought him back to circulation of beatings like a rented mule)
All in all FBI got the number
Pamoja na haya mtu huyu hakuacha kuwaambia FBI kitu cha muhimu sana
Aliwaa mbia hivi;
“We have a plan to attack th U.S., but we’re not ready yet.”
“We need to hit you outside the country in a few places so you won’t see what is going on inside”.
“The big attack is coming. There’s nothing you can do to stop it.”
Kuwa wana mpango mkubwa wa kuishambulia Marekani lakini mpango bado haujakamilika.
Kuwa kwa wakati ule wanaishambukia Marekani kwenye sehemu chache nje ya nchi ili wasijue kinaendelea ndani
Kitu kikubwa kitawafata na hawataweza kukizuia.
FBI hawakupuuzia taarifa ile.
Wakampatia namba ile station chief wa CIA Nairobi na pia wakaituma NSA (National Security Agency) Marekani
Kama kuna msomaji hajui kazi za NSA hawa wanausika na maswala mazima ya ujasusi wa Tehama.
Idara hii ina radar kubwa sana ya ardhini nchini Austaria iitwayo Pine gap ambayo hufanya kazi ya kukusanya habari za mitandao ya simu, satelite nk na kuachunguza kama kuna habari yoyote hatarishi kwa Marekani.
Kifupi idara hii ndio kinara wa kuvunja sheria ya faragha kwenye mawasiliano kwani ndio inafanya udukuzi wa hali ya juu.
Snowden, aliyekuwa contractor wa Computer wa CIA na NSA alishatoa siri hii kwenye Wiki leaks.
Tuendelee,
NSA walitumia mwaka mzima na miezi nane kuidukua namba ile ya simu.
NSA kazi yake huishia kudukua na kutuma “Transcripts” kwa CIA ili wao ndio wachakate kilichomo.
CIA wakagundua mmiliki wake anaitwa Ahmed Al Hada raia wa Yemen
Pia CIA wakafanikiwa kujua kupitia namba ile kuwa kulikuwa kuna mkutano wa Alqaeda uliopangwa ufanyike January 5, mwaka 2000 mjini Kuala Lumpur Malyasia.
Afisa wa CIA aliyechakata taarifa hii akaandika kimemo kikisema;
‘Something more nefarious was at foot”
Akimaanish kuna harakati za kihalifu zilikuwa zinawanyemelea
Kimemo hiki alikituma kwa bosi wake pamoja na taarifa alizochakata
Kwa wakati ule CIA walikuwa na majina ya kwanza tu bila ubini wa Alqaeda watatu ambao wangeshiriki mkutano ule.
Lakini haikuwachukua muda kujua majina kamili ya mmoja wao kuwa ni Khalid Al Mihdhar
CIA wakabaini huyu ni mkwe wa mmiliki wa namba ile ya simu
CIA wakafanikiwa kumfatilia tangu anatoka Yemen hadi Dubai ili aunganishe ndenge ya kwenda Kuala Lumpur kwenye kikao
Maafisa wa CIA makao makuu wakawajulisha watu wao wa Dubai station.
CIA Dubai wakawaomba maafisa usalama wa uwanja wa ndege wa Dubai wawasaidie kumkagua vizuri abiria huyu akifika dubai.
Alipofika wakati anatacheck inn ili kupanda ndege ya Malaysia, begi lake likakaguliwa kwa siri na passport yake ikatolewa copy
Copy hii wakapewa CIA wa Dubai Station
Maafisa wa CIA walipopata passport ile walishtushwa kukuta ilikuwa na Visa hai inayomwezesha kuingia Marekani na ilionesha safari yake ya mwisho kwenda marekani itakuwa ni jijini New York.
Maafisa wa CIA dubai wakarudisha taarifa zile makao yao makuu Virginia kwenye dawati maalumu la Osama bin Laden
Wale nao wakawaomba maafisa usalama wa Malyasia wawasaidie kupeleleza nini kinazungumzwa kwenye mkutano wao.
Wakawapatia na tarehe ya mkutano
Lakini Malyasia walishindwa kupandikiza microphone kwenye eneo walilokutania ili kuwasikiliza (eavesdropping)
Hivyo hawakusikia lolote lakini walifanikiwa kuwapiga picha kwa siri.
Picha zile zikatumwa CIA
Baada ya kikao, watu watatu baina yao wakapanda ndege kwenda Bangkok Thailand
Mmoja wao akiwa yule Khalid Al Mihdhar aliyetoke Yemen
Makosa yalianzia hapa!
Ni kwamba CIA walichelewa kuwajuza watu wao wa Thailand station
Hadi wanawapa taarifa hii, tayari nyayo zao zilishafutika Thailand kwani walitafutwa bila mafanikio.
Hadi kufika hapa CIA walikuwa wanamjua mtu mwingine kwa jina moja tu la Hazmi.
Mwezi March mwaka ule ule wa 2000 ikimaanisha baada ya miezi miwili tangu CIA wapoteze nyayo za watu hawa, kituo cha CIA Malyasia wakawaambia CIA Thailand wapanue wigo wa msako
Haikuchukua muda kujua kuwa huyu Nawaf al Hazmi na Khalid al Mihdhar, wote kwa pamoja waliondoka kwa ndege ile ile, siku ilele waliyofika Thailand
Ndege ile ilikuwa inaelekea Los Angels.
Hii inamaanisha nini?
Inamaanisha kuwa magaidi hawa walifanikiwa kujipenyeza Marekani kwa zaidi ya mwaka na miezi nane kabla ya shambulizi la september 11
Muda wote huu, CIA hawakuwajulisha lolote idara ya uhamiaji ambao wangeweza kufatilia taarifa zao za kusafiri viwanja vya ndege wala FBI ambao waliwajibika na kuzuia ugaidi ndani ya Marekani.
Hata hivyo ndani ya muda huu, kuna wakati idara ya CIA ya kupambana na ugaidi iliazima maafisa kadhaa wa FBI wawasaidie kazi fulani.
Pale CIA akaenda special agent Doug Miller akitokea FBI
Afisa huyu alipokuwa anafanya kazi zake, akafanikiwa kuona nyaraka zinazoelezea uwepo wa magaidi wawili ndani ya Marekani.
Taarifa hii ilimshtua na akaandaa ripoti ili aitume kwa wenzake wa FBI
Lakini alipoomba ruhusa kwa aliyekuwa msimamizi wake pale CIA aliishia kuambiwa aache kwani bado ni ‘classified’ ndani ya CIA
Wakati haya yanaendelea, ndani ya Marekani Nawaf Al Hazmi aliweza hadi kununua gari kwa jina lake
Ni muda huu ndipo CIA wakawa kama wameamka kutoka usingizini na kuanza kutuma taarifa kwa Rais Bush na mshauri wake wa mambo ya ulinzi Condoleza Rice kuwa Marekani ipo kwenye hatari kubwa ya mashambulizi ya kigaidi.
Kama walivyopuuzia wao, rais Bush naye akapuuzia taarifa zile
Ni mpaka ambapo gari hili alilolinunua Hazmi lilipokuja kukutwa limepaki uwanja wa ndege wa Dulles jijini Boston ndani yake kukiwa na risiti ya kuegeshwa saa 1 na Dk 25 asubuhi ya tarehe 11 september 2001
Ndani yake kukiwa na notices za masomo ya urubani aliokuwa akifanya Nawaf al Hazmi nchini Marekani
It was already too late to catch a flight!
Lakini wakati hii hakikuwa habari kwa wakati huo..
Uliihisi nimemaliza?
Story ndio inaanzia hapa!
Sanaa, Yemen
17th September 2001
Tupo ndani ya chumba chenye kuta kuta chakavu ndani na mahabusu moja kitongoji cha Al-Ghaydah nchini Yemen katika mji mkuu wa Sanaa.
Chumba hiki ni kojawapo ya vyumba vingi vya mahabusu za siri za CIA maarufu kwa jina la Black sites.
Wanaoshikiliwa katika mahabusu hizi, hawapewi nafasi ya kuwasiliana (incommunicado) na mtu yeyote isipokuwa na anayewachukua maelezo.
Pembeni yake mtu huyu anayewahoji washukiwa anakuwa amezungukwa na askari wenye silaha madhubuti wakiwa wamefunika nyuso zao.
Kuta za mahabusu hizi hazina maandishi yoyote au kalenda ambayo itamfanya mahabusu walau kujua yuko wapi.
Kulikuwa na njia mbalimbali za kuwaharibu kisaikolojia wanaoshikiliwa ndani ya mahabusu hizi ili kukusanya taarifa za intelejensia kutoka kwao.
Mojawapo ya njia hizi ilihusisha mateso kama waterbody, kunyimwa usingizi kwa kulazwa vyumba vyenye spika zinazotoa sauti kubwa kwa usiku mzima huku taa za vyumba vyao zikiwaka muda wote.
Haya yalifanyika washukiwa wakiwa uchi wa mnyama kwenye vyumba vyenye baridi kali.
Don’t forget the free testicles surgery with the famous burdizzo
Mahabusu hii baadae ilikuja kuwa makazi ya mtu mmoja aliyekamatwa Tanzania Muhamad Al Asad aliyekamtwa jijini Dar es salaam
Leo ndani ya chumba hiki cha mahabusu, kimepata ugeni wa Ali H. Soufani
Huyu ni chotara wa kilebanoni na kimarekani na ni kachero mwandamizi wa FBI anayehusika na kesi kubwa za ugaidi.
Kachero huyu yupo hapa kufanya mahojiano na mahabusu aliyekaa kwenye kiti cha chuma
Kinachowayenganisha ni meza pana ya pembe nne
Pembeni yake yupo komandoo wa kimarekani aliye tayari tayari ‘kutoa dozi’ kwa maabusu anayetakiwa kuhojiwa na kachero huyu
Mahabusu huyu ni Nasser Al-Bahri raia wa Yemen mwenye asili ya Saudia
Mwenyewe alipenda kujiita jina la mtu aliyekuwa karibu na Mtume Mohammed la Abu Jandal (Ibn Suhayl)
Abu Jandal inamaanisha “Baba wa Kifo”
Nasser Al-Bahri alikuwa ni mlinzi wa Osama bin Laden alipokuwa Afghanistan.
Mtu huyu alikamatwa na CIA kupitia gaidi mwingine aitwaye Fahd Al Quso ambaye alihusika kushambulia manowari ya kivita ya Marekani USS Cole ilipokuwa ikijaza mafuta kwenye ghuba ya Yemen mwaka 2000
Katika mahojiano baada ya kukamatwa, Al Quso alioneshwa picha ya mtu fulani kama anaitambua.
Akakili kuitambua picha ile kuwa ni ya Marwani Al- Shehhi aliyekuwa mmmoja wa marubani wa ndege zilizotekwa kwenye shambulio la September 11
Kwa kuwa mahojiano yaliambatana na kibano, akakili tena kuwa rubani yule alikuwa akiifadhiwa Afghanstan kwenye nyumba inayomilikiwa Abu Jabal (Nasser Al-Bahr) huyu ambaye sasa hivi ndio yupo hapa kwa ajili ya kuhojiwa.
Viongozi wa juu wa Marekani walikuwa wakisubiri kwa hamu kusikia taarifa za kiintelejensia zitakazopatikana toka kwa gaidi huyu.
Macho yao yote yalikuwa Yemen
Kwenye mahojiano Nasser akamwambia kachero yule wa FBI ifuatavyo
“You can’t stop the mujahideen”
Kachero yule akamwangalia komandoo aliye pembeni yake.
Komandoo yule akampiga kope akitabasamu huku akimwangalia Abu Jabal
Ni mafunzo tu ya kijeshi waliyopitia maafisa hawa ndio yaliwafanya waonekane hawajapanic
Really jibu hilo liliwapandisha hasira,
“You’ll find that you have underestimated America,” (utakuja kufahamu kuwa ‘umeichukulia Marekani poa’ tofauti na ilivyo)
Kachero akamjibu kwa kiarabu
Kisha kachero akaongeza , “but tell me, why do you think you’ll be victorious?” (Kwa nini mnafikiri mtaishinda Marekani)
“You want to know why?” Aliuliza Abu Jandal
“Sure,” akajibiwa
I’ll tell you why,” Jandal akajibu na kuendelea..
“The hadith says, : “‘If you see the black banners coming from Khurasan, join that army, even if you have to crawl over ice; no power will be able to stop them”
Ndugu msomaji, Hadith ni kitabu cha kiimani ambacho kilijumuisha yote ambayo Mtume Mohammed SAW alielekeza na kuyatenda katika siku zake duniani. Kitabu hiki kiliandikwa miaka zaidi ya 100 baada ya kifo chake na ni kitabu kikubwa baada ya Quran tukufu.
Kwa hiyo hapa Abu Jabal ananukuu maneno kutoka kwenye Hadith ambayo yanaelezea ishara zitakazotokea nyakati za mwisho wa ulimwengu zitakapowadia.
Kuwa wataona ishara ya watu wakiwa na bendera nyeusi (bendera nyeusi ilikuwa ni bendera aliyobebwa na Mtume na wafuasi wake kwenye uwanja wa mapambano)
Watu hawa wenye bendera nyeusi watatokea Khorasan ambako ni sehemu ya kiistoria mashariki mwa Irani kati ya Magharibi (europe) na Central Asia ambako ndio jua huchomoza.
Kwa hiyo Hadith inaeleza wakionekana watu hao inabidi waungane nao hata kwa kutambaa juu ya barafu kwani hakuna atakayewashida…(Kwa kuwa watu hawa ni ma Khalifa wa Mtume)
Haya ndio maneno aliyoyasema Abu Jandal kisha akapumzika ili kuvuta pumzi ili amalizie kunukuu..
Kabla Abu Jandal hajaanza kuongea kumalizia kunukuu Hadith, yule kachero wa FBI akamalizia kipande kilichobaki kwa lugha ya kiharabu..
“…and they will finally reach Baitul Maqdis [Jerusalem], where they will erect their flags.’”
Kuwa mwishoni wataufikia mji mtakatifu wa Yerusalemu na kusimika bendera yao
Abu Jandal akashindwa kuficha mshangao wake na kuuliza…
“You know the hadith? Do you really work for the FBI?”
Akajibiwa
“Of course I know that hadith. It’s narrated by Abu Hurairah, although it’s questionable whether that actually was said by the Prophet,”
(Najua huo mstari ulielezewa na Abu Hurairah ingawa bado kuna mashaka kama kweli hayo yalisemwa na mtume”
Kachero akaendelea ..
“and I know lots of hadith. As I told you before, the image you have of America and of her people, like me, is all wrong.” (Najua sura nyingi za hadith na kama nilivyokuambia mwanzo.. nyinyi taswira mliyonayo juu ya Marekani ni tofauti kabisa)
Mmarekani akamwambia haya yote anayoyaeleza yapo ndani ya vitabu vitakatifu vya Kiyahudi kwenye agano la kale na jipya kama ilivyo kwenye Quran
Lakini vita vinavyoongelewa ndani ya vitabu hivi vilikuwa ni vya kihistoria kabla hata ya Mitume Mohammed na Isa bin Mariam
Kachero akamuuliza gaidi,
“naweza kukuuliza swali”
Akajibiwa “Sawa”
“Let me first ask you whether Christians and Jews are allowed in Mecca and Medina.” (Wakristu na wayahudi wanaruhusiwa kukanyaga Makka na Madina)
Abu Jandal akajibu
“Of course not, that’s a silly question. Everyone knows they’re forbidden. Even the Saudi Arabian monarchy, which welcomed infidels into the Arabian Peninsula, wouldn’t dare allow them in Mecca and Medina.” (Haiwezekani, hilo ji swali la kipuuzi.. kila mtu anajua hawaruhusiwi.. Hata falme za Saudi Arabia ambao wamewaruhusu makafiri kwenye ardhi yao hawataweza kuwaruhusu wafike Makka na Medina)
“Kwa nini hawaruhusiwi”? Akaulizwa
“Kwa sababu ni mahali patakatifu”
Abu Jandal akajibu
“Are you familiar with the hadith where the Prophet has dealings with
his Jewish neighbor?” (Unajua kuwa kwenye Hadith inasemwa Mtume alikuwa anashirikiana na majirani wa Kiyahudi?) Akaulizwa tena
Akajibu “Ndiyo”
Alikutana nao wapi? Akaulizwa tena
Abu Jandal akajibu “Meddina”
“Je mtume alitenda dhambi kwa kuruhusu wayahudi wakae jirani naye Medinna”?
Gaidi huyu akapiga makelele makubwa
“Mtume hajawahi Kutenda dhambi”
Akawa anavuta minyororo iliyoshika mikono na miguu yake kutaka kumvaa kachero wa FBI
Ni katika muda huu umeme ulizimika ndani ya chumba kile huku king’ora cha hatari kikilia.
Zikaanza kusikika kelele za mlango wa chumba cha mahojiano ukigongwa kwa nguvu.
Abu Jandal akafanya kitendo cha ajabu sana…
Punde tu Kachero Ali Soufani alipogeuka kupokea simu ikiyokuwa ikiita kwa fujo wakati ule..
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
KELVIN OMWENGA
BY FORTUNATUS BUYOBE
Ilikuwa ni vigumu, kumuanisha mkazi wa Sirari, mpaka wa Tanzania na
Kenya, kuwa Kevin sio mtanzania wa kabila la wakulya.
Lakini alikuwa ni Mkisii kutokea Kenya ambaye alinufaika na utambulisho
wa ukulya.
Kelvin Omwenga alikuwa na umri mdogo tu wa miaka 28 wakati jeraha la
risasi lilipoupokonya uhai wake usiku wa August 21, 2020
Taarifa za kifo chake, ziliibua hisia mbalimbali mitandaoni huku wengi
wakikihusisha na kudhulumiana kwenye biashara.
Wengi waliohoji maisha ya Kelvin ambaye hakuwa na kazi inayojulikana
hata ghafla kuishi maisha ya kimilionea
Zaidi ya kuwa dalali wa magari wa kampuni ya Lystra Motors huko
Lavington, Nairobi, kwa malipo ya commissions ndogo Kevi aliwashangaza
watu alipoiacha ghafla kazi hiyo.
Naam!
Kevi akahamia barabara ya Galana na kwenda kupanga kwenye
appartement ya kifahari namba 703 ghorofa ya Saba akinayokadiliwa
kugharimu malipo ya Ksh 150,000/= kwa mwezi.
Kevi akabadili pia marafiki na kuonekana akishirikiana na marafiki wapya
wa hadhi yake.
Haikuchukua muda mrefu Kevi ikasambaa mtandaoni video ikimuonesha
Kevi akipongezwa na mtu wa kampuni iliyomuuzia Kevi gari la kifahari
aina ya Porsche Panamera wiki tatu kuelekea ya kifo chake.
Kwenye Video ile Kevi akanukuliwa akisema:-
“Asante.. Hii ni motisha kwa vijana wote watafutaji”
Gari hilo lilisemekana kumgharimu Kevi si chini ya shilingi za Kenya
milioni 14.
Swali likiwa, dalali aliyefanya kazi kwa commissions kwa miezi michache,
alipiga wapi mshindo uliompatia pesa hizi?
Nje ya hapo, Kelvin akawa mtu wa matanuzi na kujipostisha.
Akijirusha na mastaa mbalimbali jijini Nairobi na akiandaa party
mbalimbali kwenye appartement ya kifahari aliyokuwa akiishi.
Wakati bado wambea wakiyafatilia maisha ya Kevi bila majibu, ikafahamika
kuwa Kevi anatarajia kwenda Dubai, for a business trip.
Laiti angejua....
Kuwa marafiki wapya anaojihusisha nao ni watu wa aina gani, hakika
asingethubutu kucheza nao.
Marafiki hao walikuwa ni wakora haswa, wenye kesi nzitonzito kwenye
vituo mbalimbali vya polisi lakini kesi zao zilikuwa zinaisha kimyakimya.
3rd March 2011
Jomo Kenyatta International Airport
Nairobi, Kenya
Alhamisi mchana wa siku hii, rais wa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo,
Joseph Kabila alionekana akishuka kwenye dege lake katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Aliingia nchini Kenya kwa dharula bila hata kutoa taarifa ya awali juu ya
ujio wake.
Tangu anakwea dege lake, nchini Kongo, hakuna msaidizi wake yeyote
aliyejua anapoelekea.
Rubani pekee ndiye aliyekuja kufahamu anapotaka kwenda bosi wake
baada ya walinzi wake kumtaka kuomba clearance ya kutua kwenye uwanja
wa Jomo Kenyatta.
Wakati anashuka, sura yake ilionekana kuvimba kwa hasira karibu kuangua
kilio akiwa mbali kabisa na mzaha wa aina yoyote.
Kabila akapokelewa na waziri wa mambo ya ndani na moja kwa moja akaongozwa hadi Ikulu ya Mwai Kibaki. Kisha waziri mkuu Raila Odinga akatakiwa kufika pale Ikulu na watatu wale wakajifungia kwenye ofisi ya rais kwa zaidi ya masaa mawili.
Mle ndani kabila alikuwa akimlalamikia rais Kibaki juu ya kuibiwa kwa dhahabu zake zaidi ya kilo 400 na kuingizwa nchini Kenya. Akionekana kuwa anajua anachokiongea, akamtajia orodha ya majina 15 ya wanaotorosha dhahabu kutoka Kongo kuziingiza Kenya.
Katika list ile walikuwemo raia wa Kongo waishio Kenya ambao ni mmiliki WA timu ya Sofapaka Elly Mboni Kalekwa, Benoit Muke Katumbi na muasi wa Kongo Jean Mundeke Kabamba aka General Dako. In fact huyu General Dako alikuwa ni mshirika wa Johnbosco Ntaganda, mwanajeshi wa zamani wa Rwanda na kamanda wa kikosi cha waasi wa M23 kilichokuwa kinaendesha vita Kivu kaskazini.
Eneo hili la Kivu Kaskazini kuna migodi mingi ya dhahabu hivyo waasi huuza kwa magendo madini haya ili kununua silaha. Mwezi January 2011, rais Kabila alishapiga marufuku uchumbaji na uuzaji wa dhahabu kutoka maeneo hayo. Lakini kabila akaeleza biashara hiyo inaendelea kinyemela huku raia hao wa Kongo wakipewa msaada mkubwa na raia wa Kenya ambae saa nyingine hujitambulisha kama mkongoman.
Huyo hakuwa mwingine zaidi ya Paul Kobia aka Paul Ilunga Ngoei ikitokea anatakiwa awe mkongo kazini. Vijiweni akijulikana kama Paul Choma Mtanzania hakukosa kuingia pichani.. Kabila akasema Paul Kobia anashirikiana bega kwa bega na mtanzania Abunuwasi T Lubambura. Taarifa hii ya Kabila, Ikawalazimu Kibaki na Odinga kufanya ufatiliaji wa haraka.
Yumkini ukawa unajiuliza, Kabila alitoa wapi taarifa hizi, Kaa kwa kutulia, hapa ndio mwisho wa magari mabovu... Inatulazimu kurudi nyuma muda wa mwezi mmoja kisha tusafiri mpaka kwenye mbuga ya Virunga nchini Kongo 3rd Feb 2011 Goma International Airport Norh Kivu Province, DRC Majira ya jijini, ndege aina ya Gulfstream V Jet yenye namba za usajili N886DT inaonekana ikishuka chini la anga na kukamata runway ya uwanja wa Goma.
Ndani ya ndege Ile, ukimuondoa rubani, kuna abiria wawili raia wa Marekani. Mmoja ni Mukaila Lawal mwenye uraia pacha wa Marekani na Nigeria. Huyu ni kaka wa Kase Lawal rafiki wa karibu wa rais Obama. In fact Kase ni mfanyabiasha mkubwa na mwanasiasa wa Marekani ambaye amehudumu kama mshauri wa marais Bush na Clinton kuhusu ukanda wa Afrika.
Hata leo hii wakati ndege hii anayoimiliki kupitia kampuni ya CAMAC ambayo kaka yake ni mmoja wa abiria, Kase alikuwa akihudumu kama mshauri wa Obama ambaye alimteua kuwa mjumbe wa kamati ya biashara na majadiliano. Abiria mwingine ndani ya ndege hii ni Edward Carlos St.Marry, mhitimu wa chuo cha kijeshi cha West point pia mmiliki wa kampuni ya Axiom Trading company limited.
Pale uwanjani ikaonekana gari moja aina ya Land cruiser pickup mkonga ikiisogelea ndege ile. Siti ya mbele ya gari ile upande wa abiria, ilikuwa imekaliwa na Johnbosco Ntaganda. Mambo ya Kongo yanastaajabisha sana. Huyu kiongozi wa waasi ina maana alikuwa yupo kwenye uwanja wa ndege ambao pia hutumiwa na wanajeshi wa Kongo pamoja na MONUSCO bila wasiwasi wowote. Ndio maana unaona vita haviishi kwani watu wazito kama abiria hawa wapo ndani ya biashara hiyo.
Gari ile ilipoifikia ikafungua body ya nyuma na kuanza kushusha mzigo fulani. Naam! Zilikuwa kilo 475 za dhahabu safi kabisa. Kutoka kwenye ndege ukashushwa mzigo wa dola za kimarekani yapata milioni 22.5 Pesa ile akaichukua Ntaganda na gari lake likatokomea haraka. Huku nyuma wakati ndege ile ikijiandaa kutua, ikavamiwa na wanajeshi wa serikali ikiwa bado haijamaliza runway. Wazungu wale wakasachiwa na kukutwa na ule mzigo. Wakapelekwa Kinshasa kwa kabila. Kule wakaeleza kila kitu.
Kuwa walitua uwanjani pale baada ya mtu mmoja aitwaye David kuwashawishi kuwa kuna biashara nzuri ya dhahabu wanaweza kuifanya nchini Kenya. Ushawishi ukazidi baada ya wamarekani hawa kutua Kenya na kukutanishwa na mtu aliyejitambulisha kwao kama Michelle D Malonga Mtu huyu aliwaambia anaweza kuwauzia kilo 475 ya dhahabu kutoka Kongo yenye thamani ya dola za Marekani milioni 23.
Ili kuwaonesha kuwa hatanii, akawapeleka mpaka kwenye moja ya godown akawaambia wachukue sample moja wakaipime. Majibu yakatoka mazuri. Wamarekani wakalipia pesa za usafiri, bima, vibari na kodi ya mzigo ule kuingia Kenya. Naam! Wakalipa dola laki 5 mbele ya mwanasheria Punit Vadgama wa kampuni ya mawakili Shapley Barrett and Co. Advocates ya nchini Kenya Bila kujua kuwa Paul Choma alikuwa behind the scene akiuchora mchezo wote.
Baada ya malipo haya wamarekani wakarudi nchini kwao kusubiri mzigo. Mzigo haukutumwa. Walipouliza ni kwa nini ? Wakajibiwa mazingira ya kuutoa ni magumu. Kukaibuka mabishano baina yao wakitaka wapelekwe ulipo mzigo. Hii ndio ilikuwa sababu ya ndege hii kutua hapa leo baada ya kuunganishwa na watu wa Goma.
Baada ya wiki tatu (Mwezi February mwishoni 2011) ukapigwa mzigo mwingine kwenda Kenya. Safari hii ilikuwa ni tani mbili na nusu ambao ulipitishwa kwa gari mpakani mwa Uganda na Kenya kwenye miji ya Busia na Malaba. Hakukaa sawa naye mzigo wake wa kilo 400 ukapigwa.
KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA).
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE
BARKE RASHID PESA
Huyu nimuongeleaye hapa mama yake alishafariki mwaka mmoja tu uliopita.
Akabaki na mzazi mmoja tu mzee Rashid Pesa ambaye ni baharia huko Afrika ya Kusini.
Hata wakati amepotea na ikiwa haijulikani yuko wapi, Zilishaanza kutengenezwa nadharia huenda alienda Afrika Kusini kwa baba yake.
Hii ni kwa sababu wakati anatafutwa, hati yake ya kusafiria nayo haikuonekana.
Barke Pesa alikuwa ni mwenyeji wa Ilala jijini Dar es Salaam lakini baadaye akaenda kupanga Tabata Bima.
Ungana nami katika mkasa huu wa kusisimua.
If I would be a cop, I would have investigated this case deeper.
BARKE RASHID PESA alikuwa amepanga Chumba huko Tabata bima lakini nyumbani kwao Ikiwa ni Ilala.
Mwishoni mwa mwaka 2021 alisafiri kwenda Zanzibar.
Pichani ni BARKE
Alirudi jioni Dar tarehe 31 Dec 2021
Akaenda kutua mizigo yake kwa rafiki yake aishie Buguruni.
Rafiki huyu anaitwa AISHA JATA (Pichani)
Barke alifikia hapo badala ya kwake Tabata, Ili usiku huo aunganishe kwenda Magomeni.
Naam!
Alikuwa na ratiba ya kwenda Magomeni Usiku ule kushiriki Birthday party ya rafiki yake aitwaye FATUMA DUSHU (Pichani)
Huyu rafiki wa Buguruni hakuweza kutoka kwa dharula fulani hivyo Barke akaenda peke yake Magomeni.
Barke alifanikiwa kufika kwenye tafrija ya kumbukumbu ya kuzaliwa shoga yake FATUMA DUSHU ambayo iliendelea mpaka “mida mibovu”
Pia wakisherekea kuukaribisha mwaka mpya
Baadae Barke akataka kutoka tena kuendeleza “bata”
Akamuomba rafiki yake FATUMA DUSHU watoke wote.
Rafiki huyu akasema hawezi kutoka kwa muda ule.
Hata hivyo akampa dada mmoja aitwaye NURU atoke naye.
Wakatoka
Wakaanzia Bar fulani ambayo haikutajwa
Kisha
Wakahamia Forty Forty Tabata
Lengo likiwa ni kulala kwa Barke Tabata baada ya bata lile.
Lakini wakati wapo kwenye ile bar ya kwanza,
Kuna mtu alimpiga picha Barke kwa siri.
Picha zile zikatumwa kwa mmama fulani aitwaye ASHA JITU (Pichani)
Huyu Asha Jitu alikuwa ni rafiki wa zamani wa Barke
Asha Jitu akiwa tayari kaolewa.
Barke akafanya mapinduzi kama ya Zanzibar.
Akazaa na mme wa Asha Jitu.
Uhasama wao ukaanzia hapo.
Kukiwa na ahadi nyingi za “Kuonyeshana”
In fact hakuna rangi ambayo Barke aliacha kuiona baada ya kuingia kwenye uhasama na Asha Jitu.
Akawa anapata mikasa ya ajabu asijue ilipotokea
Mkasa mmojawapo ni kushikiliwa kwa muda mrefu kituo cha polisi Msimbazi kwa kupakaziwa kesi ya unga
Sasa ndipo “vichomi” wapendao violence wakawa wana kazi ya kuyaandama maisha ya Barke na kumpa ripoti hasimu wake Asha Jitu.
Hivyo hata Barke alipokuwa anamwagilia moyo, Asha akatumiwa picha aone jinsi mkemwenza anavyojiachia.
Lengo la kumfatilia likiwa halijulikani
Wakiwa pale Forty Forty, Barke akatoka kwenda kusikojukikana.
Yule mwenzake (NURU) akaamua kuondoka Kwenda Kitambaa Cheupe Tabata Liwiti.
Baadae wawili hawa wakawasiliana kwa simu
Nuru akamwelekeza Barke amfate Kitambaa Cheupe.
Mida hiyo kulishaanza kupambazuka.
Sasa pale kitambaa cheupe Kamera za usalama zilimnasa NURU akiongea na kaka fulani kabla Barke hajafika.
Hakujulikana ni kwa nini hii CCTV footage ilikuja kufutwa baadae ikimuonyesha Nuru akiwa na huyu kaka pamoja.
Mida ya saa Mbili Asubuhi Barke akafika pale Kitambaa cheupe.
Hakuwa mgeni wa Sehemu ile kwani hata page ya mtandao wa kijamii ya Kitambaa Cheupe ilishawahi kumpost Barke akiwa pale Kitambaa cheupe
Mwenye nguo ya Orange ni Barke akiwa Kitambaa cheupe.
Barke alipofika, Nuru anahama meza ya yule kaka na kwenda kumfata Barke alipokaa.
Yule kaka anawafa lakini yanaonekana majibizano na Kina Barke wanahamia kaunta ya ndani.
Kule ndani Camera haifiki.
Yule kaka anawafata tena ndani.
Barke alipofika, Nuru anahama meza ya yule kaka na kwenda kumfata Barke alipokaa.
Yule kaka anawafa lakini yanaonekana majibizano na Kina Barke wanahamia kaunta ya ndani.
Kule ndani Camera haifiki.
Yule kaka anawafata tena ndani.
Baadae Barke, Nuru na yuke kaka wanatoka ndani na kuhamia nje.
Lakini safari hii Barke anaonekana akiwa hakiwezi kwa kilevi.
Hii ni ghafla sana kwa kuzingatia jinsi alivyoingia na sasa anavyotoka.
Hapo Pichani mwenye nguo ya kijani ni Nuru na Mwenye nguo ya Orange ni Barke.
Sasa wakawa wamekaa pamoja tena nje
Baadae Nuru anatoka,
Ni muda mfupi tu Tangu Nuru atoke Inakuja Boda boda.
Anaanza kuipanda Barke
Yule mkaka akiifata nyuma yake.
Kisha kaka yule naye anapanda kwa nyuma mtindo wa Mshikaki
Uelekeo Ukiwa ni Nyumba ya Wageni iitwayo MARIDADI iliyoko njia panda ya barabara ya Segerea na barabara ya Kuelekea Vingunguti.
Ndugu Msomaji, Lazima hawa walishakuwa wameagana na Nuru.
Ndipo utata wa mkasa unapoanza
Yule kaka ambaye jina lake maarufu ni John Cena Bouncer alikuwa pale kikazi zaidi.
Naam!
Alikuwa kwenye mkataba wa kumtafuta, Kumtongoza na kumpata Barke.
Kuna utata mkubwa kwa anayetajwa kuwa ndiye alimtuma.
Zilongwa mbali, Zitendwa Mbali
Maiti ya Barke ilikuja kugundulika na wahudumu wa Guest tarehe 2 Jan 2022.
Mwili wake ukapelekwa Muhimbili
Ndugu wa Barke wakiwa hawajui lolote.
Yule dada wa Buguruni ambapo Barke aliacha mizigo yake akashangaa siku zinapita Barke hafati mabegi yake.
Ndugu zake pia wakashangaa Barke hapatikani na hashiriki matukio muhimu ya kifamilia.
Kulikuwa na wagonjwa kwao Ilala ndugu wakakutana, Barke hakwenda.
Ukatokea msiba kwao, Barke hakwenda.
Zikaanza kuwashwa taa za Full.
Jitihada za kumtafuta kwa marafiki hazikuzaa matunda.
Nuru (aliyekuwa naye mara ya mwisho) akiwa hapatikani.
Wakaelekezwa kwa rafiki yake aishiye Kigogo aitwaye ANJELA (Pichani)
Pale Ukatokea mkanganyiko kidogo,
Anjela akasema hajui hata kama Barke alisharudi kutoka Zanzibar
Na hata Nuru hajui alipo
Lakini ni tarehe 18 Jan huyu anjela aliwajulisha ndugu kuwa maiti ya Barke iko Muhimbili
Ikiandaliwa kuzikwa na Jiji.
Ndugu wakashangaaa mbona katika vituo vya polisi walipokuwa wanaulizia kama kuna maiti yoyote hawakupewa taarifa?
Ndugu wakaanza kuulizia kama mwili ulipogundulika kama kuna jalada lolote la uchunguzi lilifunguliwa polisi.
Wakaambiwa na Uongozi wa nyumba ya wageni ya Maridadi ulipopatikana mwili wa Barke kuwa walitoa taarifa ile kituo cha polisi Tabata.
Walipofika Tabata wakabaini mpelelezi aliyefatilia sakata lile hakuwa amefungua jalada lolote. Na hakukuwa na hata jitihada za kuanzisha uchunguzi nyuma ya mauaji wale.
Ndugu wakaenda Kituo cha Buguruni ambapo angalau waliopata ushirikiano mdogo lakini sio sana.
Hii ni kwa sababu Manjagu waliogopa kuumbuana kwa uzembe ambao tayari ulishafanyika mwanzoni wa Kesi hii.
Ikabidi ndugu watumie mpelelezi wa kujitegemea (Mind you nchini hakuna mpelelezi wa kujitegemea ajulikane rasmi)
Katika kupeleleza Ikajulikana kuwa ni John Cena ndiye aliondoka naye.
Taarifa hizi zilipatikana pale pale Kitambaa Cheupe ambapo walitoa Video za mwisho za marehemu akiwa pale.
Cha ajabu mara ya kwanza kabisa zilionyesha Video Msichana Nuru akiwa na John Cena.
Lakini baadaye ndugu alipoenda kunyonya video ile kwa matumizi ya kipelelezi wakakuta footage Inayomwonyesha Nuru akiwa na John Cena Imefutwa. Sababu za kufanya hivi hazikubainika mpaka leo. (Polisi walipaswa kuchimba hapa zaidi kwani kuna lead ya kikachero)
John Cena hakuwa mgeni wa maeneo yale, alikuwa akifahamika hivyo alitambulika kwa urahisi.
Watu walikuwa hadi na namba yake ya simu hivyo namba yake Ikatolewa.
Namba ilikuwa ikizimwa na kuwashwa kwa nyakati tofauti.
Baadae namba ile ikasomeka Banana, Kisha Gongo la mboto
Kisha Chanika ambako kulikuwa na Show ya Mziki Mnene ya EFM
John Cena akakutwa akiwa kwenye Show
Akakamatwa.
Sasa hapa ndipo Tunaanza,
Usifikiri tumemaliza.
Aliyetajwa kuwa ndiye Contractor wa haya mauaji akaunti yake inaonekana active mpaka leo ikimaanisha yupo Kitaa,
Hakuwahi kumpangia Chumba Barke kama ilivyoelezwa
Who Exactly was behind this.
Kwa nini picha zitumwe?(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA).
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
*_ASKARI MSTAAFU ALIYEKUWA ANANYONGA WATU GEREZA LA ISANGA -DODOMA._*
Kifo kinatisha; kifo hakina huruma; kifo hutenganisha wapendanao, lakini kwa bahati mbaya, siku ikifika hakuna anayeweza kukikwepa.
Akionyesha hofu ya kifo alipokuwa na bendi ya Orchestra Makassy, Remmy Ongala aliimba kibao kinachoitwa “Siku ya Kufa”. Maudhui ya kibao hicho yalirejewa na Remmy mwenyewe japo kwa mahadhi tofauti alipojiunga na bendi ya Super Matimila. Huko alitunga kibao kiitwacho “Kifo Hakina Huruma”.
Kana kwamba ana uwezo wa kufanya majadiliano na kifo aliimba: “Kifo, kifo, siku yangu ikifika eeh, kifo niarifu mapema, niage wanangu, niage familia yangu yote, pesa zangu nizigawanye, zimebaki nizile mwenyewe, kifo nakusubiri kwa hamu.”
Mwanamuziki huyo, aliyefahamika zaidi kwa jina la Dk Remmy, alifariki dunia akiacha kifo kikiendelea kuchukua uhai wa mamilioni ya watu duniani katika mazingira tofauti. Baadhi hufa ghafla ajalini, wapo wanaofariki dunia baada ya kuugua, wengine huuawa na wenzao kwa hasira au kisasi au kwa bahati mbaya au bila kujua, lakini kuna wanaouawa kwa hukumu inayotolewa na vyombo vya haki; huhukumiwa kunyongwa hadi kufa.
Wanaopatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia huhukumiwa kifo. Japokuwa kila nafsi itaonja mauti, wanaohukumiwa kifo ndio huweza kujua siku na aina ya kifo.
Hivi mtu akihukumiwa kifo na mahakama, je, wanaofanya kazi hiyo ni nani? Kitanzi kikoje? Hali inakuwaje kabla? Je, hupata fursa ya kuaga ndugu na jamaa? Wanaotekeleza hukumu ya kunyonga wenzao hadi kufa pia wanakuwa wametenda kosa la kuua, je, huchukuliwa hatua gani kisheria? Je, wanaoajiriwa kufanya kazi hiyo wanapatikanaje? Wanajisikiaje kukatisha uhai wa wenzao?
Lakini pia katika utumishi wao, ufanisi wao unapimwaje? Je, hupata utulivu wa moyo na amani kiroho?
Kwa kawaida kazi nyingi hutangazwa wazi magazetini na wale wanaojiona wana sifa zinazohitajika, huandika barua za kuomba na kusubiri kuitwa kwa mahojiano. Lakini, ni vigumu kukutana na tangazo la kazi hii ngumu kuliko zote.
Pia, najua kwamba baadhi ya kazi huhitaji wasomi wa kiwango cha juu, nyingine watu wenye ujuzi fulani lakini zipo zinazohitaji wenye nguvu.
Binafsi nadhani kazi hii inahitaji watu wenye moyo wa ujasiri ambao hawawezi kukosa utulivu wa moyo wala amani kiroho wakitekeleza jukumu lao kwa watu waliohukumiwa kifo.
Maswali hayo na mengine mengi nimekuwa nikijiuliza kwa siku nyingi na katika kufuatilia nililazimika kufunga safari hadi mkoani Dodoma ambako nilifanikiwa kumshawishi mtekelezaji wa hukumu hizo afanye mahojiano nami.
Saa 12.00 jioni, nikiwa na mwenyeji wangu wa Dodoma tulifika nyumbani kwa mtu tuliyekuwa tukimtafuta, Anangisye (siyo jina lake halisi). (SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA).
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
MAUAJI YA POLISI MBANDE.
By, Fortunatus Buyobe
Mbwana ni mfanyakazi wa duka la jumla mali ya Tariq Makame maarufu kwa jina la "Mpemba"
Duka hili lipo maeneo ya Mbagala Zakhiem wilayani Temeke
Mbwana ni mtu wa kuzingatia sana swala
Naam!
Kila ufikapo muda wa kuswali hufunga duka na kwenda masjid
Ingawa Mbwana anaishi Mbagala Kuu, mara chache, majira ya usiku henda Mkuranga mkoani Pwani kijijini Kisiju "kwa Mnyabudu"
Ilikuwa ni vigumu sana kutabiri tabia za Mbwana
Mara nyingine saa 12 jioni angeenda Mbande kwa bodaboda kuangalia ratiba fulani inayojurudia.
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA).
click here to unlock the post

Fortunatus Buyobe @Buyobe
LICENSE TO KILL .
By Fortunatus Buyobe
(SUBSCRIBE HAPO CHINI KUPATA MUENDELEZO WA MKASA HUU NA NYINGINE NYINGI KWA MWEZI MZIMA).
click here to unlock the post